Kampuni ya DIS
inayomiliki maduka makubwa nchini Brazil na ambao wanamiliki asilimia 40
ya haki za usajili wa Neymar wametishia kwenda mahakamani kuhusiana na
mgao wao kwa nyota huyaa o katika usajili wake kwenda Barcelona. Kampuni
hiyo inayoendeshwa na Idi Sonda imedai kuwa na haki ya kupata fedha
zaidi juu ya makubaliano ya ziada kati ya klabu ya Santos na Barcelona
ambayo yako nje ya ada ya uhamisho wake ambayo ilifikia kiasi cha euro
milioni 57. Mkurugenzi
Mtendaji wa DIS, Roberto Moreno ameomba kupewa taarifa kamili ya hati
ya uhamisho wa Neymar kwenda Barcelona ili kupata ufafanuzi kuhusu
malipo ya baadae watakayopewa Santos. Moreno
amesema mpaka kipindi hicho hawajaonyeshwa hati yoyote, hivyo atafunga
safari kwenda makao makuu ya Santos kufuatilia hati hiyo na baada ya
hapo wataamua kama watahitaji kwenda mahamani. Hatua
ya kampuni hiyo imekuja kufuatia taarifa zilitolewa na vyombo vya
habari nchini humo kwamba Santos watapata nyongeza ya euro milioni mbili
kama mchezaji huyo atakuwemo katika orodha ya wachezaji watatu kwenye
tuzo ya Ballon d’Or kwenye kipindi cha miaka mitano ijayo.Friday, July 12, 2013
KAMPUNI YA MADUKA NCHINI BRAZIL WATISHIA KWENDA MAHAKANI KUHUSU USAJILI NEYMAR
Kampuni ya DIS
inayomiliki maduka makubwa nchini Brazil na ambao wanamiliki asilimia 40
ya haki za usajili wa Neymar wametishia kwenda mahakamani kuhusiana na
mgao wao kwa nyota huyaa o katika usajili wake kwenda Barcelona. Kampuni
hiyo inayoendeshwa na Idi Sonda imedai kuwa na haki ya kupata fedha
zaidi juu ya makubaliano ya ziada kati ya klabu ya Santos na Barcelona
ambayo yako nje ya ada ya uhamisho wake ambayo ilifikia kiasi cha euro
milioni 57. Mkurugenzi
Mtendaji wa DIS, Roberto Moreno ameomba kupewa taarifa kamili ya hati
ya uhamisho wa Neymar kwenda Barcelona ili kupata ufafanuzi kuhusu
malipo ya baadae watakayopewa Santos. Moreno
amesema mpaka kipindi hicho hawajaonyeshwa hati yoyote, hivyo atafunga
safari kwenda makao makuu ya Santos kufuatilia hati hiyo na baada ya
hapo wataamua kama watahitaji kwenda mahamani. Hatua
ya kampuni hiyo imekuja kufuatia taarifa zilitolewa na vyombo vya
habari nchini humo kwamba Santos watapata nyongeza ya euro milioni mbili
kama mchezaji huyo atakuwemo katika orodha ya wachezaji watatu kwenye
tuzo ya Ballon d’Or kwenye kipindi cha miaka mitano ijayo.FIFA YA FUATILIA KWA KARIBU KASHFA YA UPANGAJI MATOKEO
SHIRIKISHO la Soka
Duniani-FIFA linafuatilia kwa karibu kashfa ya upangaji matokeo
inayozikabili vilabu viwili vya soka vya ridhaa nchini Nigeria
iliyotokea wiki iliyopita. Katika
matokeo ambayo yanaonekana kama ya mchezo wa kriketi, klabu ya Plateau
United Feeders iliibugiza Akurba FC kwa mabao 79-0 wakati Police Machine
wao waliitandika Bubayaro FC kwa mabao 67-0 mwishoni mwa wiki
iliyopita. Hatua uchunguzi kwa vilabu hivyo imekuja kutokana na timu hizo kuhitaji matokeo ya aina hiyo ili waweze kupanda daraja. Ambapo
katika taarifa yake FIFA imedai kuwa inafuatilia tukio hilo la tmu hizo
za Nigeria kwa karibu ili kuona jinsi gani Shirikisho la Soka la nchi
hiyo, NFF litatatua tatizo hilo. FIFA
inafanya hivyo kwa kutambua kuwa suala hilo ni la ndani hivyo NFF ina
wajibu wa kufanya uchunguzi na kuchukua hatua zinazostahiki kama
ikigundulika aina yoyote ya udanganyifu katika mechi hizo.
TAIFA STARS SASA MMEIVA KUPAMBANA- TENGA
Rais
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amesema
kikosi cha Taifa Stars sasa kina uwezo wa kushindana katika mashindano
yoyote, kwani tayari kimeiva.
Akizungumza
na wachezaji wa timu hiyo kambini kwao hoteli ya Tansoma, Dar es
Salaam, Rais Tenga aliwaambia kuwa kiwango walichoonesha kwenye mechi
zilizopita za mchujo za Kombe la Dunia dhidi ya Morocco na Ivory Coast
kimethibitisha hilo.
“Kiwango
mlichoonyesha katika mechi hizo kila Mtanzania anayewafuatilia
amekiona, hivyo hatuna shaka kuwa mtatuwakilisha vizuri kwenye mechi ya
kesho dhidi ya Uganda,” amesema Rais Tenga na kuwataka kupigana kwa
ajili ya Tanzania.
Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kesho (Julai 13 mwaka
huu) saa 9 kamili alasiri Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itacheza na
Uganda (The Cranes) katika mechi ya kwanza ya raundi ya mwisho kuwania
tiketi ya kucheza Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika
Kusini.
Rais
Tenga amesema TFF, mdhamini Kilimanjaro Premium Lager, Kamati ya
Ushindi na Watanzania kwa ujumla wanawaunga mkono kwani wamekuwa
wakiboresha kiwango chao kila wanavyozidi kucheza mechi tangu wake chini
ya Kocha Kim Poulsen, Mei mwaka jana.
Wakati
huo huo, Rais Tenga ameahidi kumpatia tiketi ya kwenda Uganda kwenye
mechi ya marudiano mshabiki Wiseman Mwakyusa Luvanda anayetembea kwa
miguu kutoka Mbeya kuja Dar es Salaam kushuhudia mechi ya kesho.
“Kama
ni kweli anakuja kwa kutembea, huyu ameonyesha kiwango kikubwa cha
uzalendo kwa timu ya Taifa, nitampatia tiketi ya kwenda Kampala
kuishangilia Taifa Stars kwenye mechi ya marudiano,” amesema Rais Tenga.
POULSEN, MICHO WATABIRI MECHI KALI
Makocha
wa timu hizo Kim Poulsen wa Taifa Stars na Sredojvic Micho wa The
Cranes wamesema mechi ya kesho itakuwa ngumu kwa vile kila mmoja
amejiandaa kuhakikisha anafanya vizuri.
Wakizungumza
na Waandishi wa Habari leo, makocha wote waliezea ubora wa wapinzani
wao, lakini wakasisitiza kuwa wanaingia uwanjani kuhakikisha wanashinda
ili kujiweka katika mazingira mazuri kwa ajili ya mechi ya marudiano
itakayochezwa Kampala wiki mbili zijazo.
Kim
alisema Uganda ndiyo inayoongoza kwa ubora wa viwango vya FIFA katika
ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati, hivyo ni changamoto kwao ingawa
wachezaji wake tayari wamejipanga vizuri kwa ajili ya mechi hiyo.
Naye
Micho aliyefuatana na nahodha wake Hassan Wasswa alisema Taifa Stars
imekuwa ikifanya vizuri tangu iwe chini ya Kim, na itakuwa na wachezaji
tisa wa kikosi cha kwanza kinachocheza mechi za mchujo za Kombe la Dunia
wakati kwa upande wake atakuwa na wachezaji wawili tu.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Subscribe to:
Posts (Atom)
