Monday, April 22, 2013

DROGBA VS ETOO KUWANIA TUZO GUU LA DHAHABU
WASHAMBULIAJI bora  barani Afrika, Didier Drogba na Samuel Eto’o
wameingizwa kwenye orodha ya kuwania tuzo ya Guu la Dhahabu mwaka 2013, kufuata nyayo za mshambuliaji wa Paris Saint Germain ya Ufaransa, Zlatan Ibrahimovic, aliyeshinda mwaka jana.
Manahodha hao wa Ivory Coast na Cameroon ni Waafrika pekee katika orodha ya wachezaji tisa walioingizwa kwenye kinyang’anyiro cha tuzi hiyo, inayotolewa kwa wachezaji wenye mafanikio makubwa na mwonekano mzuri.
Wawania tuzo hiyo wengine ni Mfaransa David Trezeguet, Mjerumani Miroslav Klose, Mtaliano Andrea Pirlo, Waspanyola Andres Iniesta na Iker Casillas na Waingereza Franck Lampard na David Beckham.
Tuzo huyo Guu la Dhahabu inatolewa kwa mchezaji aliye uwanjani ambaye angalau ana umri usiopungua miaka 29 na hawezi kushinda zaidi ya mara moja
Washindi wa awali wa tuzo hiyo ni; 2003: Roberto Baggio (Italia, Brescia) 2004: Pavel Nedved (Jamhuri ya Czech, Juventus) 2005: Andryi Shevchenko (Ukraine, AC Milan) 2006: Ronaldo (Brazil, Real Madrid) 2007: Alessandro Del Piero (Italia, Juventus) 2008: Roberto Carlos da Silva (Brazil, Fenerbahçe) 2009: Ronaldinho (Brazil, AC Milan) 2010: Francesco Totti (Italia, Roma) 2011: Ryan Giggs (Wales, Manchester United) na 2012: Zlatan Ibrahimovic (Sweden, Paris SG).

TAZAMA MECHI WALIZO CHEZA NA MAGOLI WALIOFUNGA
 Didier Drogba Games/Goals
2009/10 Chelsea 21/17
2008/09 Chelsea 24/5
2007/08 Chelsea 19/8
2006/07 Chelsea 36/20
2005/06 Chelsea 29/12
2004/05 Chelsea 26/10
2003/04 Marseille 35/19
2002/03 Guingamp 34/17
2001/02 Guingamp 10/3
2001/02 Le Mans 21/5
2000/01 Le Mans 11/0
1999/00 Le Mans 30/7
1998/99 Le Mans 2/0
TOTAL: 298/123

Samuel Eto
'o Games/Goals
2009/10 Inter 19/8
2008/09 Barcelona 36/30
2007/08 Barcelona 18/16
2006/07 Barcelona 17/11
2005/06 Barcelona 34/27
2004/05 Barcelona 37/25
2003/04 Mallorca 32/17
2002/03 Mallorca 29/14
2001/02 Mallorca 29/6
2000/01 Mallorca 25/11
1999/00 Mallorca 9/6
1999/00 R Madrid 2/0
1998/99 R Madrid 1/0
1997/98 Leganes 28/3
TOTAL: 316/174
  

BONDIA wa uzito wa juu wa Uingereza, Dereck Chisora amefanikiwa kumchakaza Hector Alfredo Avila katika raundi ya tisa likiwa ni pambano lake la kwanza toka alipopata kipigo kutoka kwa David Haye Julai mwaka jana. Chisora mwenye umri wa miaka 29 alikuwa akipigana pambano lake la kwanza toka aliporejeshewa leseni yake Machi mwaka huu baada ya leseni hiyo kuzuiwa kufuatia vurugu za nje ya ulingo alizofanya na Haye mapema mwaka huu. Akihojiwa mara baada ya kumpiga Avila ambaye ni raia wa Argentina Chisora amesema lilikuwa pambano gumu kwasababu mpinzani wake alikuwa amempania lakini anashukuru amemaliza kwa ushindi na anasubiri mpinzani mwingine. Chisora anasubiri pambano linguine dhidi ya bondia mwingine wa uzito wa juu wa Uingereza David Price ambaye kabla ya kupambana na Chisora atapigana na Tony Thompson katika pambano la marudiano Julai mwaka huu.

NUSU FAINALI UEFA CHAMPION LIGI KESHO WANAUME DIMBANI
[Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku, Bongo Taimu]
Jumanne Aprili 23
Bayern Munich v Barcelona
Jumatano Aprili 24
Borussia Dortmund v Real Madrid
MARUDIANO
Jumanne Aprili 30
Real Madrid v Borussia Dortmund
Jumatano Mei 1
Barcelona v Bayern Munich
FAINALI
25 Mei 2013
UWANJA wa WEMBLEY, Londo
SUAREZ BADO AENDELEZA VITUKO KATIKA SOKA WADAU WAMSHANGAA
BOSI wa Liverpool, Brendan Rodgers, amekiri kutoona tukio la Straika wake mahili Luis Suarez  wakati akimng’ata Beki wa Chelsea Branislav Ivanovic bila Refa Kevin Friend kuona, FA imesema itapitia Mkanda huo na Ripoti ya Refa ili kutoa mwelekeo huku Wachambuzi wa Soka huko England wakilaani vikali kitendo hicho.
Brendan Rodgers ameahidi kupitia Mkanda wa Video wa tukio hilo na kutoa tamko lakini Meneja wa zamani wa Liverpool, Graeme Souness, amelaani vikali tukio hilo na kusema umefika wakati wa Mchezaji huyo kutoka Uruguay kuondolewa Liverpool.
Souness ameng’ang’ania kuwa Liverpool ni Klabu kubwa yenye hadhi kama Barcelona, Real Madrid a Manchester United, na Mchezaji huyo anatia dosari sifa ya Klabu.
Tukio hilo la Suarez kumng’ata Ivanovic lilitokea kwenye Mechi ya BPL, Barclays Premier League, iliochezwa Anfield na Liverpool kutoka sare 2-2 na Chelsea huku Suarez akishika makusudi na Chelsea kupata Penati waliyofunga na ni yeye Suarez ndie alieisawazishia Liverpool katika Dakika za majeruhi.

 MATUKIO YA MAKALI YA SUAREZ KATIKA  SOKA LA DUNIA:
Novemba 2007
Akiwa Nahodha wa Ajax alifungiwa na Klabu yake baada ya kupigana na mwenzake Albert Luque wakati wa Haftaimu kwenye Mechi.
Julai 2010
Afrika na Dunia nzima itamkumbuka Suarez, ambae ni Mchezaji wa Uruguay, kwa kuikatili Ghana huko Afrika Kusini kwenye mechi ya Robo Fainali ya Kombe la Dunia alipoushika mpira kwa makusudi kwenye mstari wa goli dakika ya mwisho ya muda wa nyongeza na kuwanyima Ghana goli la wazi la ushindi.
Kwa kitendo hicho, Suarez aliwashwa Kadi Nyekundu na Ghana kupewa penati lakini Asamoah Gyan, ambae aliwahi kuwa Ligi Kuu England na Timu ya Sunderland, alikosa kufunga penati hiyo.
Novemba 2010
Alipata Kifungo cha Mechi 7 akiwa huko Uholanzi  na Klabu ya Ajax baada ya kumng’ata meno Mchezaji wa PSV Eindhoven Otman Bakkal kwenye mechi ya Ligi huko Uholanzi.
Octoba 2011
Wakicheza na Everton, alivunga amechezewa faulo na Jack Rodwell na kujidondosha na Rodwell akapewa Kadi Nyekundu.
Octoba 2011
Suárez alimkashifu Kibaguzi Patrice Evra wa Manchester United na kufungiwa Mechi 7 na kupigwa Faini Pauni 40,000.
Decemba 2011
Akiwa kwenye mashitaka ya kumkashifu Kibaguzi Patrice Evra wa Manchester United na kabla hajahukumiwa alionekana kutoa ishara ya matusi kwa Mashabiki wa Fulham kitendo ambacho kilimpa Kifungo cha Mechi 1.
Februari 2012
Man United na Liverpool walikutana tena Old Trafford kwa mara ya kwanza tangu tukio la Suarez kumkashifu Kibaguzi Evra na Suarez, bila kutarajiwa, aligoma kumpa mkono Evra.
October 2012
Alishangilia Goli lake kwa kujirusha mbele ya Meneja wa Everton, David Moyes, ambae kabla ya Mechi hiyo na Liverpool alitamka Wachezaji wadanganyifu kama Suarez wnaohadaa Marefa wanafanya Mashabiki waikatae Soka ya England.
Januari 2013
Alipoza mpira kwa mkono na kufunga Bao la ushindi kwa Liverpool kwenye Mechi ya Raundi ya 3 ya FA CUP dhidi ya Timu ya Daraja la chini Mansfield.
Machi 2013
Akiichezea Nchi yake Uruguay kwenye Mechi ya Mchujo ya kuwania kuingia Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwaka 2014, Suarez alionekana kumtandika ngumi Beki wa Chile Gonzalo Jara bila Refa kuona.
FIFA wanachunguza tukio hili.
  
RATIBA- BPL, BARCLAYS PREMIER LEAGUE:
Jumatatu Aprili 22
[Saa 4 Usiku]
Man United v Aston Villa
MSIMAMO==BPL, BARCLAYS PREMIER LEAGUE
NA TIMU P GD PTS
1 Man Utd 33 40 81
2 Man City 33 29 68
3 Arsenal 34 30 63
4 Chelsea 33 31 62
5 Tottenham 33 17 61
6 Everton 34 13 56
7 Liverpool 34 19 51
8 West Brom 33 -1 45
9 Swansea 33 1 42
10 West Ham 34 -7 42
11 Fulham 34 -8 40
12 Southampton 34 -7 39
13 Norwich 34 -20 38
14 Sunderland 34 -7 37
15 Stoke 34 -11 37
16 Newcastle 34 -17 37
17 Aston Villa 33 -24 34
18 Wigan 33 -23 31
19 QPR 34 -27 24
20 Reading 34 -28 24

 YANGA INANAFASI KUBWA KUTWAA UBINGWA POINT 1 TU
Vinara wa ligi kuu vodacom tanzania bara yanga sasa imefikisha pointi 56 baada ya kuitandika bao 3-0 Jkt ruvu  wakifuatiwa na Azam FC wenye Pointi 47 na waliobakisha Mechi 3.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
MECHI WALIZOBAKISHA YANGA:
Mei 1: YANGA v COASTAL UNION [UWANJA wa TAIFA]
Mei 18: YANGA v SIMBA [UWANJA wa TAIFA]
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Lakini ikiwa Azam FC watatoa sare au kufungwa Mechi yao inayofuata huko Mkwakwani hapo Aprili 27 dhidi ya Coastal Union, basi Yanga watachukua Ubingwa bila ya kucheza Mechi yao inayofuata.
RATIBA:
Jumatano Aprili 24
African Lyon v JKT Ruvu
Alhamisi Aprili 25
Simba v Ruvu Shooting
Jumamosi Aprili 27
Coastal Union v Azam FC
Jumapili Aprili 28
Simba v Polisi Moro
MSIMAMO:
NA TIMU P W D L GD PTS
1 Yanga 24 17 5 2 31 56
2 Azam FC 23 14 5 4 22 47
3 Kagera Sugar 23 11 7 5 8 40
4 Simba SC 22 9 9 4 11 36
5 Mtibwa Sugar 24 9 9 6 3 36
6 Coastal Union 23 8 9 6 3 33
7 Ruvu Shooting 22 8 6 8 0 30
8 JKT Oljoro 24 7 7 10 -5 28
9 Prisons FC 24 6 8 10 -7 26
10 Mgambo Shooting 23 7 4 12 -7 25
11 JKT Ruvu 23 6 5 12 -18 23
12 Toto African 25 4 10 11 -12 22
13 Police M 23 3 10 10 -10 19
14 African Lyon 23 5 4 14 -19 19

Saturday, April 20, 2013

WENGER AKATAAA KUFUNGUKA KUSUHU MAN U
BOSI wa Washika bunduki wa jiji la london Arsenal, mzee Arsene Wenger, amegoma kuzungumza lolote kuhusu kuipa Man United heshima wanayostahili ikiwa watatwaa Ubingwa na wakati huo huo Jumapili, Meneja wa zamani wa Liverpool, Rafael Benitez, atarudi tena Anfield kwa mara ya kwanza tangu atimuliwe na safari hii anaiongoza Chelsea, Timu ambayo baadhi ya Washabiki wake hawamkubali kabisa hasa kwa sababu ya uhasama wake na Chelsea alipokuwa Liverpool.

PATA HABARI KAMILI:
RATIBA- BPL, BARCLAYS PREMIER LEAGUE:

Jumamosi Aprili 20
[Saa 11 Jioni]
Fulham v Arsenal
Norwich v Reading
QPR v Stoke
Sunderland v Everton
Swansea v Southampton
West Brom v Newcastle
West Ham v Wigan
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
WENGER NA MAN UNITED
Wakati Arsene Wenger akimsifia Straika wake Olivier Giroud kwa kuwa na Msimu mzuri wa kwanza na Arsenal, Meneja huyo aligoma kujibu hoja ya Wanahabari ya uwezekano wa Manchester United, ikiwa na Straika wake wa zamani Robin van Persie, kutua Emirates Jumapili ijayo Aprili 28 na kutwaa Taji la Ubingwa wa BPL, Barclays Premier League, Uwanjani hapo.
Upo uwezekano kwa Man United kutwaa Taji lao la 20 Jumatatu Usiku kwa kuifunga Aston Villa na katika Mechi inayofuata huko Emirates dhidi ya Arsenal, Klabu hiyo ya London itawajibika kuweka Gwaride la misitari miwili ya Wachezaji wake kabla Mechi kuanza na kuipigia makofi Timu ya Man United ikiingia Uwanjani kama Bingwa.
Kitendo hicho, huku Staa wao wa zamani Robin van Persie akiwemo Man United baada ya kuihama Arsenal mwanzoni mwa Msimu huu, bila shaka kitawakera sana Arsenal.
Wenger alikataa kuzungumzia hilo na kusema mkazo wake ni Mechi yao ya leo na Fulham na si Mechi ijayo na Man United.
Alisema: kikubwa  ni ushindi dhidi ya Fulham Jumamosi. Sioni sababu ya kuzungumzia Man United leo. Niulize tena Wiki ijayo"
MENEJA WA CHELSEA RAFAEL BENITEZ USO KWA USO NA LIVERPOOL"
BOSI wa muda wa  club ya Chelsea Rafael Benitez anategemea mapokezi mazuri kutoka kwa Mashabiki wa Liverpool wakati atakapotua Anfield kwa mara ya kwanza tangu atimuliwe huko Mwaka 2010 hapo Jumapili wakati Chelsea itakapocheza na Liverpool Mechi ya BPL.
Akiwa na Liverpool kwa Miaka 6, Benitez alimudu kutwaa UEFA CHAMPIONZ LIGI na FA CUP.
BENITEZ NA LIVERPOOL:
Juni 2004 - Aondoka Valencia kwenda Liverpool kumbadili Gerard Houllier
Mei 2005 - Liverpool waitoa AC Milan kwa Penati, watwaa UEFA CHAMPIONZ LIGI
Mei 2006 - Liverpool waitoa West Ham kwa Penati, watwaa FA Cup
Mei 2007 - Liverpool wafungwa 2-1 na AC Milan Fainali UEFA CHAMPIONZ LIGI
Mei 2009 - Liverpool wamaliza Nafasi ya 2 BPL nyuma ya Manchester United
Mei 2010 - Liverpool wamaliza Nafasi ya 7 BP –ikiwa nafasi ya chini kabisa tangu 1999
3 Juni 2010 - Benitez atimuliwa Liverpool
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
KOCHA huyo ametamka: “Nina Marafiki wengi huko lakini safari hii mkazo ni Soka tu. Ni kweli nilikuwa na Liverpool kwa Miaka 6 na kutwaa Mataji mengi lakini nadhani Mashabiki wataelewa sasa ni mpinzani na wao wataishabikia Timu yao!”
Akiwa na Liverpool, Benitez aliongoza Liverpool kuifunga Chelsea kwenye Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na hatimae kutwaa Kombe Mwaka 2005 na pia kutwaa FA CUP na vilevile kuifunga tena Chelsea kwenye Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI Mwaka 2007.
Matokeo hayo yalileta ushindani mkubwa kati ya Benitez na Chelsea na hasa Meneja wao wa wakati huo, Jose Mourinho.
Matukio hayo yamewafanya baadhi ya Mashabiki wa Chelsea kutomkubali Benitez kama Meneja wao tangu alipoteuliwa Meneja wa muda Mwezi Novemba Mwaka jana ili kumbadili Roberto Di Matteo.
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
RATIBA- BPL, BARCLAYS PREMIER LEAGUE:
Jumapili Aprili 21
[Saa 9 na Nusu Mchana]
Tottenham v Man City
[Saa 12 Jioni]
Liverpool v Chelsea
Jumatatu Aprili 22
[Saa 4 Usiku]
Man United v Aston Villa
MSIMAMO==BPL, BARCLAYS PREMIER LEAGUE
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
MAN UNITED
33
26
3
4
75
35
40
81
2
MAN CITY
32
20
8
4
58
27
31
68
3
CHELSEA
32
18
7
7
64
33
31
61
4
ARSENAL
33
17
9
7
64
35
29
60
5
TOTTENHAM
32
17
7
8
55
40
15
58
6
EVERTON
33
14
14
5
51
37
14
56
7
LIVERPOOL
33
13
11
9
59
40
19
50
8
WBA
32
13
5
14
42
43
-1
44
9
SWANSEA
32
10
11
11
43
42
1
41
10
FULHAM
33
10
10
13
44
51
-7
40
11
WEST HAM
33
10
9
14
38
47
-9
39
12
SOUTHAMPTON
33
9
11
13
47
54
-7
38
13
NEWCASTLE
33
10
6
17
42
59
-17
36
14
NORWICH
33
7
14
12
31
52
-21
35
15
SUNDERLAND
33
8
10
15
37
45
-8
34
16
STOKE CITY
33
7
13
13
28
41
-13
34
17
ASTON VILLA
33
8
10
15
36
60
-24
34
18
WIGAN
32
8
7
17
37
58
-21
31
19
QPR
33
4
12
17
29
54
-25
24
20
READING
33
5
9
19
36
63
-27
24

NANI MKALI KATI YA MESSI' VS NEYMA VS C.RONALDO


Friday, April 19, 2013

SIMBA YAPELEKA MKATABA WA NGASA TFF
Club ya Simba SC imeupeleka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) mkataba wake mpya na mshambuliaji Mrisho Khalfan Ngassa, ambao unaonyesha ataitumikia klabu hiyo na msimu ujao pia, kwa mujibu wa blogu ya bin zubeiry.
Chanzo cha habari kutoka ndani ya Simba SC, kimesema; “Tumeupeleka mkataba ambao Ngassa alisaini na sisi na TFF wamegonga muhuri wa kuupokea,”.
Kikifafanua, chanzo hicho kimesema; “Sisi tuliununua mkataba wa Ngassa uliokuwa umebaki Azam FC kwa shilingi Milioni 25, kwa hivyo, haki za mchezaji huyo zote zikahamia kwetu,”. “Lakini alipokuja kwetu, tukazungumza naye, akasaini mkataba wa msimu mmoja zaidi kutoka ule mkataba wake uliobaki Azam FC na tulimpa shilingi Milioni 30.

Fedha taslimu Milioni 12 na gari aina ya verosa yenye thamani ya Sh. Milioni 18, akasaini kila sehemu na kuweka dole gumba,”kilisema chanzo hicho.
Hata hivyo, chanzo hicho kimesema kwa sasa Mrisho amekuwa akilalamika kwa uongozi wa Simba kwamba alidhani alipewa Milioni 12 na Verosa ili akubali kuja Simba.
Ikumbukwe awali Ngassa aligoma kupelekwa kwa mkopo Simba SC, hadi alipofanya mazungumzo na viongozi wa klabu hiyo na kufikia makubaliano ndipo akajiunga na klabu hiyo.
Mrisho NgassaLakini chanzo hicho kimesema kwa sasa Mrisho anataka kufanya tena mazungumzo na Simba SC kwa ajili ya kusaini rasmi mkataba mwingine. “Sisi bado tunajiuliza, huyu mtu alikwishasaini na sasa anasema alidhani alipewa fedha na gari ili akubali kuja Simba SC. Inawezekana kwa sababu wachezaji wetu wana  matatizo, wakishaona fedha wao wanasaini tu bila hata kuisoma mikataba,”.

“Bado tunatafakari, tunaweza kurudi naye mezani, ili aitumikie klabu kwa moyo bila kinyongo, au tu tukaamua autumikie mkataba ambao tayari tumekwishausajili na TFF,”kilisema chanzo.
Siku zote, Mrisho mwenyewe amekuwa akisistiza hakusaini mkataba mwingine Simba SC akitokea Azam, bali anajua alikuja kumalizia mkataba wake wa klabu yake ya zamani.

Mrisho Ngassa alipelekwa kwa mkopo Simba baada ya kuonyesha mapenzi kwa klabu yake ya Zamani ya yanga.
IBF YATEUA REFA PAMBANO LA CHEKA VS MASHALI
SHIRIKISHO la Ngumi la Kimataifa (IBF) limeteua refarii na majaji wa pambano la kutetea ubingwa wa Afrika kati ya anayeushukilia ubingwa huo Francis Cheka wa Tanzania na mpinzani wake Thomas Mashali ambaye ni bingwa wa uzito wa Middle ukanda wa Afrika ya Mashariki na Kati (ECAPBA). Refarii wa mpambano huo wa kukata na shoka atakuwa ni John Shipanuka kutoka nchini Zambia mbaye alilisimamia pambano kati yaFrancis Chaka na Mada Maugo mwaka jana kwa ustadi mkubwa. Shipanuka ni Afisa Ugavi katika jeshi la Jamhuri ya Watu wa Zambia na ana ujuzi mkubwa wa kusimamia mapambano ya ngumi ya kimataifa.
Aidha, majaji wa mpambano huo ni Daudi Chikwanje kutoka Malawi ambaye ndiye Katibu Mkuu wa Chama Cha Ngumi Cha Malawi na ambaye anakuwa jaji namba moja. Steve Okumu wa Kenya ambaye anakuwa jaji namba mbili na Ismail Sekisambu wa Uganda ambaye anakuwa jaji namba tatu.
Msimamizi mkuu wa mpambano huo ni Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Mtanzania Onesmo Ngowi.Hata hivyo Ngowi amemwagiza Mwenyekiti wa Kamati ya Viwango  na Ushindi wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Nchini (TPBC)Boniface Wambura amshikie nafasi hiyo ili Ngowi apate nafasi nzuri ya kusimamia mapambano matatu ( moja la ubingwa wa dunia kwa vijana,, lingine la ubingwa wa mabara kwa wanawake na lingine ubingwa wa Afrika) yatakayofanyika nchini Ghana tarehe 3 mwezi Mei.        
Nayo Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa nchini TPBC imeshateua maofisa watakaosimamia mapambano ya awali pamoja na kutoa kibali kwa kampuni ya Mumask Investment and Gebby ili iendeshe mpambano huo"                          
Hii ni mara ya pili kwa bondia Francis Cheka kutetea ubingwa wake tangu amsambaratishe kwa TKO bondia machachari Mada Maugokatika mpambano uliofanyika mwaka jana mwezi wa Aprili katika ukumbi wa PTA jijini Dar es Salaam.
MURRAY ASHINDWA KUSONGA MBELE
MCHEZAJI nyota tetenesi namba moja wa Uingereza, Andy Murray ameshindwa kusonga mbele katika hatua ya nane bora baada ya kukubali kipigo cha 6-1 6-2 kutoka kwa Stanislas Wawrinka katika mzunguko wa tatu wa michuano ya Monte Carlo Masters inayoendelea huko Monaco. Murray ambaye ameshinda mara nane katika mechi 12 walizokutana Wawrinka wa Switzerland katika mchezo huo alionekana kucheza chini ya kiwango chake cha kawaida nafasi ambayo ilitumiwa vyema na mpinzani wake kuhakikisha anaibuka kidedea. Kupoteza mchezo huo ni pigo kubwa kwa Murray ambaye alikuwa akitumia michuano hiyo kujiandaa kwa ajili ya kutetea taji lake la michuano ya wazi ya Ufaransa. Kwa upande mwingine Novak Djokovic na Rafael Nadal wao walifanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo baada ya kushinda mechi zao.


RAIS wa klabu ya fc Barcelona, Sandro Rosell amebainisha kuwa amepanga kugombea nafasi hiyo kwa kipindi kingine pindi atakapomaliza kipindi cha kwanza mwaka 2016. Rosell alichaguliwa kuwa rais wa klabu hiyo ya Hispania mwaka 2010 ambapo hapo kabla alikuwa mjumbe wa bodi katika uongozi wa aliyekuwa rais wa klabu hiyo Joan Laporta kabla ya kujiuzulu mwaka 2005. Chini ya uongozi wa Rosell Barcelona imefanikiwa kushinda taji moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya, taji lingine moja la Ligi Kuu nchini Hispania na moja la Kombe la Mfalme ambapo msimu huu wako katika nafasi ya kunyakuwa taji lingine la ligi huku wakiwa katika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. 
Barcelona inamilikiwa na maelfu ya wanachama ambao huchagua rais na kamati ya utendaji, uchaguzi ambao hufuatiliwa kwa karibu na mashabiki wa soka wa mji huo na nchi nzima kwa ujumla.