Wednesday, April 24, 2013

MUNICH YAITANDIKA BARCA 4-MTUNGI ANGALI MAMBO YA JANA
MABINGWA wa Ujerumani maarufu BUNDASLIGA, Bayern Munich wamejiweka katika nafasi nzuri ya kutinga hatua ya fainali ya michuano ya klabu bingwa barani Ulaya baada ya kuitandika Barcelona 4-0 katika mchezo wa kwanzawa nusu fainali nchini Ujerumani. Mabao mawili ya Thomas Müller, na yale ya Mario Gomez na Arjen Robben yaliizamisha Barcelona ambayo ilikuwa na nyota wake wote wakutegemewa, akiwemo Messi ambaye alikosa michezo kadhaa kabla ya kuanzishwa usiku huu. Hii imekuwa mara ya kwanza kwa Barcelona kufungwa mabao 4-0 tangu mwaka 1997 walipofungwa na Dynamo Kiev ya Urusi mwaka 1997 kwenye hatua ya robo fainali ya michuano ya klabu bingwa barani ulaya. Bayern Munich wametoka kutawazwa kuwa mabingwa wa Ujerumani wiki chache zilizopita na iwapo watafanikiwa kuiondosha Barcelona na kutinga hatua ya fainali ya michuano ya klabu bingwa, itakuwa fainali yao ya tatu kushiriki ndani ya miaka minne. Michuano hiyo itaendelea tena leo usiku ambapo mahasimu wa Barcelona, Real Madrid watakuwa na kibarua kizito pale itakapokaribishwa katika Uwanja wa Signal-Iduna-Park kukwaana na wenyeji Borussia Dortmund kwenye mchezo unaotaajiwa kuwa mgumu na wa kusisimua.
TAIFA STARS KUCHEZA MICHUANO YA COSAFA

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itashiriki michuano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA) itakayofanyika Julai mwaka huu nchini Zambia. Taifa Stars inashiriki michuano hiyo ya timu za Taifa za nchi wanachama wa COSAFA ikiwa timu mwalikwa. Nchi wanachama wa COSAFA ni Afrika Kusini, Angola, Botswana, Comoro, Lesotho, Madagascar, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Namibia, Shelisheli, Swaziland, Zambia na Zimbabwe. Michuano hiyo itafanyika kuanzia Julai 6 hadi 21 mwaka huu katika miji ya Lusaka, Ndola na Kabwe. Ratiba ya makundi ya michuano hiyo itapangwa Mei 3 mwaka huu jijini Lusaka. Mara ya mwisho michuano hiyo ilifanyika miaka mitatu iliyopita. Hii itakuwa mara ya pili kwa Tanzania kushiriki michuano hiyo baada ya kucheza ya kwanza iliyofanyika mwaka 1996 nchini Zimbabwe. Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inatarajia kuingia kambini mwishoni mwa mwezi ujao kujiandaa kwa mechi ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech. Juni 16 mwaka huu Taifa Stars itacheza na Ivory Coast jijini Dar es Salaam katika mechi nyingine ya mchujo ya Kombe la Dunia wakati Juni mwishoni na Julai mwanzoni itacheza mechi ya Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) dhidi ya Uganda. Wakati huo huo, waandishi wa habari wanaotaka kuripoti michuano hiyo wanatakiwa kuwasilisha majina yao TFF kabla ya Aprili 27 mwaka huu ili maombi yao yatumwe COSAFA kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho (Accreditation).

Tuesday, April 23, 2013

KOCHA KIM ATANGAZA YOUNG TAIFA STARS
Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametangaza timu ya pili ya Taifa (Young Taifa Stars) atakayoitumia kuangalia wachezaji ambao baadaye anaweza kuwajumuisha kwenye timu ya wakubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo (Aprili 23 mwaka huu) kabla ya kutaja kikosi hicho, Kim amesema timu hiyo ni sehemu ya Mpango wa Maendeleo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) uliozinduliwa Aprili 4 mwaka huu ukilenga kuendeleza wachezaji.

Amesema timu hiyo inajumuisha wachezaji ambao wamepita umri wa kuchezea timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) na wakubwa ambao hawajapata fursa ya kuingia Taifa Stars, lakini atatumia Young Taifa Stars kuangalia uwezo wao.

“Timu hii ni kiungo kati ya vijana na wakubwa. Wengi wa wachezaji watakuwa vijana, lakini wakubwa wachache watapata fursa ya kuwemo ili kuangalia uwezo wao hata kama uko nyuma waliwahi kuchezea Taifa Stars. Lakini timu hii vilevile ni changamoto wa wachezaji wa Taifa Stars kuwa wapo wanaosubiri wazembee ili wachukue nafasi zao,” amesema.

Young Taifa Stars yenye wachezaji 30 itakuwa na kambi ya siku tano jijini Dar es Salaam kuanzia Mei 2 hadi 6 mwaka huu.

Wachezaji walioitwa ni Aishi Manula (Azam), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) na Ali Mustapha (Yanga) ambao ni makipa. Mabeki ni Kessy Hassan (Mtibwa Sugar), Kennan Ngoma (Barnsley FC, Uingereza), Himid Mao (Azam), Ismail Gambo (Azam), David Mwantika (Azam), Miraji Adam (Simba), Mohamed Hussein (Kagera Sugar), Waziri Salum (Azam), Samih Nuhu (Azam) na Emily Mgeta (Simba).

Viungo ni Haruna Chanongo (Simba), Edward Christopher (Simba), Mudathiri Yahya (Azam), William Lucian (Simba), Jonas Mkude (Simba), Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Jimmy Shoji (JKT Ruvu), Abdallah Seseme (Simba), Ramadhan Singano (Simba), Farid Mussa (Azam) na Vicent Barnabas (Mtibwa Sugar).

Washambuliaji ni Hussein Javu (Mtibwa Sugar), Jerome Lambele (Ashanti United), Zahoro Pazi (JKT Ruvu), Twaha Hussein (Coastal Union), Abdallah Karihe (Azam) na Juma Luizio (Mtibwa Sugar).

AFRICAN LYON, JKT RUVU KUUMANA CHAMAZI
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaendelea kesho (Aprili 24 mwaka huu) kwa mechi moja kati ya wenyeji African Lyon na JKT Ruvu.

Mechi hiyo namba 165 itachezwa Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam chini ya usimamizi wa Kamishna Hamisi Kisiwa wa Dar es Salaam. Waamuzi wa mechi hiyo itakayoanza saa 10 kamili jioni ni Hashim Abdallah, Omari Kambangwa, Abdallah Selega na Said Ndege wote wa Dar es Salaam.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
VAN MAGOLI JEZI 20 APIGA TATU NA KUILETEA UBINGWA WA 20 MAN U:
Katika mechi ya jana Robin van Persie, amefanya kile ambacho wadau na mashabiki wa man u ambao waliondoa imani naye kuwa haufumanii nyavu lakini aliweza kudhihilisha kuwa yeye ni bora zaidi baada ya kutupia Bao Dakika za 2, 13 na 33 na, kufuatia kazi nzuri ya Nguli Ryan Giggs na Wayne Rooney, na kuwatwanga Aston Villa Bao 3-0 Uwanjani Old Trafford na kuipatia Manchester United Ubingwa wa BPL, Barclays Premier League huku wakiwa na Mechi 4 mkononi.
HISTORIA:
.Hii ni mara ya 4 kwa Man United kutwaa Ubingwa Uwanjani kwao Old Trafford
.Mara nyingine walizotwaa Ubingwa Old Trafford ni Mwaka 1999, 2002 na 2009
.Mwaka 2001 walitwaa Ubingwa wakiwa na Mechi 5 mkononi
.Msimu wa 1999/2000 walitwaa Ubingwa kwa pengo la Pointi 18
kwa sasa Van Persie  anaongoza Ufungaji Bora BPL akiwa na Bao 24 kwa mtukutu Luis suarez akiwa na mabao 23.
Huu ni Ubngwa wa 13, chini ya Sir Alex Ferguson, katika Miaka 21 ya Historia ya Ligi Kuu England.
MSIMAMO==BPL, BARCLAYS PREMIER LEAGUE
NA
TIMU
P
GD
PTS
1
Man Utd
34
40
84
2
Man City
33
29
68
3
Arsenal
34
30
63
4
Chelsea
33
31
62
5
Tottenham
33
17
61
6
Everton
34
13
56
7
Liverpool
34
19
51
8
West Brom
33
-1
45
9
Swansea
33
1
42
10
West Ham
34
-7
42
11
Fulham
34
-8
40
12
Southampton
34
-7
39
13
Norwich
34
-20
38
14
Sunderland
34
-7
37
15
Stoke
34
-11
37
16
Newcastle
34
-17
37
17
Aston Villa
34
-27
34
18
Wigan
33
-23
31
19
QPR
34
-27
24
20
Reading
34
-28

24

PFA KUMPA USHAURI MZEE WA MENO
CHAMA cha Wanasoka wa Kulipwa-PFA kimesema kuwa mshambuliaji nyota wa Liverpool, Luis Suarez atapatiwa ushauri wa namna ya kuzikabili hasira zake kufuatia tukio lake la kumg’ata beki wa Chelsea Branislav Ivanovic. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uruguay tayari ameshamuomba radhi Ivanovic kwa tukio hilo alilofanya katika mchezo wa ligi baina ya timu hizo ambao uliisha kwa sare ya mabao 2-2 lakini klabu yake imeshamtoza faini na kunauwezekano mkubwa FA nao wakatoa adhabu baadae. Suarez mwenye umri wa miaka 26 alifungiwa kucheza mechi saba baada ya kufanya tukio kama hilo wakati akiwa katika klabu ya Ajax Amsterdam ya Uholanzi kipindi cha nyuma ambapo alimng’ata Otman Bakkal wa PSV. Nyota huyo asiyetabirika pia alishawahi kufungiwa mechi nane katika Ligi Kuu nchini Uingereza baada ya kumfanyia vitendo vya kibaguzi Patrice Evra wa Manchester United. Ofisa Mkuu wa PFA Gordon Taylor amesema hakuna shaka juu ya kiwango bora alichonacho nyota huyo lakini inasikitisha kwa vitendo vya ambavyo amekuwa akivifanya ndio maana wameamua kumsaidia ili aweze kuzikabili hasira zake.


Monday, April 22, 2013

FA USO KWA USO SUAREZ HUKU CLUB YAKE PIA IKIMTWANGA FAINI

 Chama cha Soka cha England "FA" kimetangaza kumfungulia Mashitaka Straika wa Liverpool Luis Suarez, kwa Kosa la kuleta vurugu Uwanjani kwa kumng’ata meno Beki wa Chelsea Branislav Ivanovic.


Tukio hilo lilitokea Uwanjani Anfield Liverpool ilipotoka sare ya 2-2 na Chelsea katika Mechi ya BPL, Barclays Premier League lakini Refa Kevin Friend hakuliona kama ilivyothibitishwa na FA kufuatia Ripoti ya Refa na hivyo wao kupata fursa kumfungulia mashitaka kwa kutumia ushahidi wa Mikanda ya Video.
Mara baada ya tukio hapo Uwanjani Ivanovic alionekana akimuonyesha Refa Friend alama za meno mkononi mwake.
SUAREZ_KIDOLEFA pia imetamka kuwa kawaida makosa kama hayo ni Kifungo cha Mechi 3 lakini kwa tukio hilo Adhabu hiyo haitoshi.
Suarez amepewa had Aprili 23 Saa 2 Usiku mwaka huu awe amejibu Mashitaka hayo na
 Jumatano Aprili 24, Jopo Huru la FA litaketi kusikiliza Kesi hiyo.
Tayari Suarez ameshaomba radhi kwa kumuuma meno Ivanovic na kuongea na Beki huyo wa Chelsea.
Liverpool pia imetangaza kumpiga Faini lakini imesisitiza ataendelea kubakia kuwa Mchezaji wao.

OLIVIER GIROUD: ARSENAL KUPAMBANA KADI NYEKUNDU

Washika bunduki wa jiji la london  Arsenal chini ya meneja wenger" wamewasilisha Rufaa yao kupinga Kadi Nyekundu aliyopewa Straika wao mahili  Olivier Giroud Juzi Jumamosi Arsenal walipoifunga Fulham Bao 1-0 Uwanjani Craven Cottage kwenye Mechi ya Ligi.
Giroud alitolewa kwa kumchezea Rafu Stanislav Manolev.
Akielezea tukio hilo baada ya Mechi, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, alisema: “Giroud aliniambia aliteleza wakati akifuata Mpira na hilo limethibitishwa na Mikanda ya Video.”
Jopo Huru la FA litatoa uamuzi wake Siku ya Jumanne.
Ushindi huo wa Arsenal dhidi ya Fulham ulikuwa ushindi wao wa 5 katika Mechi 6 za Ligi na umezidi kuwaimarisha katika azma yao ya kumaliza kwenye 4 Bora.
Arsenal sasa wapo nafasi ya 3 wakiwa na Pointi 63.
Tangu ajiunge na Arsenal kutoka Montpellier mapema mwanzoni mwa Msimu huu, Giroud amepachika Bao 17 katika Mechi zake 46 na Arsenal.
ARUDI TENA NDANI YA STAMFORD BRIDGE"
CLATTENBURG1
REFA Mark Clattenburg anatajiwa kurudi katika dimba la Stamford Bridge kuichezesha Chelsea kwa mara ya kwanza tangu asafishwe suala la Ubaguzi dhidi ya John Obi Mikel na huko Emirates, Arsenal i
CLATTENBURG NA CHELSEA
JUMAPILI, Refa Mark Clattenburg atarudi Uwanja wa Stamford Bridgekuichezesha Chelsea kwa mara ya kwanza baada ya Miezi 6 baada ya kusafishwa kutumia Ubaguzi dhidi ya Kiungo wa Chelsea John Obi Mikel.
Chelsea walilalamika kuwa Clattenburg alitumia lugha isiyofaa dhidi ya Mikel wakati wanachapwa Bao 3-2 na Manchester United Mwezi Oktoba Mwaka jana Uwanjani Stamford Bridge.
Baada ya uchunguzi wa FA, Refa huyo, ambae alitamka jambo hilo limemtisha, Clattenburg alisafishwa kuhusu tuhuma zote.
Baadae Klabu ya Chelsea ilitoa tamko la kusikitika kuhusu walivyochukulia suala hilo na kutaka radhi na sasa, Miezi 6 baadae, Clattenburg ataichezesha Chelsea watakapocheza na Swansea City 

RAIS TENGA ATOA MIPIRA YA DOLA 30,000

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga ametoa mipira zaidi ya 1,200 yenye thamani ya dola 30,000 za Marekani kwa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Tanzania Bara na vituo 21 vilivyo hai vya kuendeleza vijana (academies).

Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) lilimpa Rais Tenga fedha hizo ikiwa ni shukrani kwake kwa kushughulikia mgogoro wa uongozi wa mpira wa miguu nchini Kenya uliodumu kwa miaka miwili; ambapo nchi hiyo kutokana na mgogoro huo ilikuwa na vyama viwili (KFF na FKL).

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi mipira hiyo kwenye ofisi za TFF, Dar es Salaam leo (Aprili 22 mwaka huu), Rais Tenga amesema amefanya hivyo kwa vile anaamini kuwa mipira ndiyo kitu muhimu katika kuinua mchezo huo mahali popote.

“Dhamira yangi si kushukuru kwa hafla hii, bali kutoa sababu kwa nini nimefanya hivi. Ninaamini kwa kuanzia mipira ndiyo muhimu, pili kwa kufanya hivi itaonekana kweli mipira imegawiwa,” amesema Rais Tenga.

Amesema amesema mpira wa miguu kwa Tanzania unahitaji sana watu wa kujitolea, na yeye amefanya hivyo kwa kujitolea kutokana na ukweli shughuli anazotumwa na FIFA ni za kujitolea.

Rais Tenga ambaye pia alitumwa na FIFA kutatua matatizo ya uongozi wa mpira wa miguu katika nchi za Uganda, Zambia na Sudan Kusini amesema anaamini anapata fursa hizo kutokana na kuwa kiongozi wa TFF, na kwa kuwakumbuka waliomchagua ndiyo maana hakusita kupeleka fedha hizo kwenye mipira.

Amesema moja ya ndoto zake wakati anaingia kuongoza TFF mwaka 2004 ameshindwa kutimiza ni kusaidia mipira, kwani uwezo wa kununua mipira kwa wanaocheza katika ngazi ya chini hasa watoto haupo.
“Hizi kelele zote za maendeleo ya mpira wa miguu ni kwa sababu shuleni hakuna vifaa. Nia yangu ilikuwa shule zote zipate mipira, lakini hiyo ni moja ya ndoto nilizoshindwa kutekeleza. Vipaji haziwezi kupatikana kama watoto hawachezi.

“Tunashukuru sana kwa Serikali kurejesha mpira shuleni. Hata nitakapoondoka madarakani nikipata nafasi nitaendelea kuomba mipira kwa ajili ya shule,” amesema Rais Tenga.

Vyama vya mikoa ambavyo jumla ni 32 (Tanzania Bara na Zanzibar) kila kimoja kimekabidhiwa mipira 25 (kumi saizi namba tano, 15 saizi namba nne kwa ajili ya vijana). Kwa academies ambazo ni 21 kila moja imepewa mipira 25 (minane saizi namba tano, na 15 saizi namba nne).

Viongozi waliohudhuria hafla hiyo ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) Almasi Kasongo, Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) Nassib Mabrouk na Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) Riziki Majala.

Kwa upande wa shule alikuwa Kanali mstaafu Idd Kipingu ambaye ni mmiliki wa shule ya Lord Baden ya Bagamoyo mkoani Pwani.

COASTAL, AZAM KUCHEZA SIKU YA MUUNGANO
Timu za Coastal Union ya Tanga na Azam zitapambana Aprili 26 mwaka huu katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) itakayofanyika kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Awali mechi hiyo namba 168 ilikuwa ichezwe Aprili 27 mwaka huu, lakini imerudishwa nyuma kwa siku moja ili kuipa fursa Azam kujiandaa kwa mechi ya marudiano ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho dhidi ya AS FAR Rabat ya Morocco.

Mechi hiyo itachezeshwa na Andrew Shamba kutoka mkoani Pwani akisaidiwa na Abdallah Mkomwa (Pwani), Vicent Mlabu (Morogoro) wakati mwamuzi wa mezani atakuwa Mohamed Mkono wa Tanga. Charles Komba wa Dodoma ndiye atakayekuwa Kamishna wa mechi hiyo ya raundi ya 24.

Baada ya mechi ya Tanga, Azam itarejea Dar es Salaam siku inayofuata tayari kwa safari ya kwenda Rabat itakayofanyika Aprili 28 mwaka huu. Mechi hiyo itachezwa wikiendi ya Mei 3, 4 au 5 mwaka huu.

Keshokutwa (Aprili 24 mwaka huu) kutakuwa na mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya African Lyon na JKT Ruvu itakayochezwa Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam.
Iwapo Azam itafanikiwa kusonga mbele katika michuano ya Kombe la Shirikisho kutakuwa na marekebisho ya ratiba ya VPL. Hiyo ni kutokana na raundi inayofuata ya Kombe la Shrikisho kuchezwa wikiendi ya Mei 17, 18 na 19 mwaka huu ambapo bado haijajulikana Azam itaanzia wapi (nyumbani au ugenini) iwapo itavuka.

Mechi nyingine za VPL mwezi ni Aprili 25 (Ruvu Shooting vs Simba- Uwanja wa Taifa), na Aprili 28 (Simba vs Polisi Morogoro- Uwanja wa Taifa).

MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI
Kocha Mkuu wa Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager, Kim Poulsen atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kesho (Aprili 23 mwaka huu).

Mkutano huo utafanyika saa 5 kamili asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

WAMOROCCO WA AZAM WAINGIZA MIL 50/-
Mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho kati ya Azam na AS FAR Rabat ya Morocco iliyochezwa juzi (Aprili 20 mwaka huu) imeingiza sh. 50,850,000.

Fedha hizo katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa timu hizo kutoka suluhu zimetokana na watazamaji 8,268 waliokata tiketi.

Viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 10,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000 ambacho kilikuwa kiingilio cha juu kwa jukwaa la VIP A. Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo walikuwa 7,354.

Mgawo ulikuwa kama ifuatavyo; gharama za tiketi sh. 5,575,500, asilimia 15 ya uwanja sh. 6,791,175, asilimia 10 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 4,527,450 na asilimia 75 iliyokwenda kwa klabu ya Azam ni sh. 33,955,875.

Mechi iliyopita ya Azam katika michuano hiyo dhidi  ya Barrack Young Controllers II ya Liberia iliingiza sh. 44,229,000 kutokana na watazamaji 17,128 waliokata tiketi. Viingilio vilikuwa sh. 2,000, sh. 5,000, sh. 10,000 na sh. 20,000 ambacho kilikuwa kiingilio cha juu kwa jukwaa la VIP A.

MECHI YA JKT RUVU, YANGA YAINGIZA MIL 66/-
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya JKT Ruvu na Yanga iliyochezwa jana (Aprili 21 mwaka
huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 66,568,000 kutokana na watazamaji 11,864.

Viingilio katika mechi hiyo namba 106 iliyomalizika kwa Yanga kutoa dozi ya 3-0 kwa wenyeji wao vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 15,702,752.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 10,154,440.68.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,984,450.40, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 4,790,670.24, Kamati ya Ligi sh. 4,790,670.24, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,395,335.12, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) sh. 931,519.21 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 931,519.21.
 Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)