Friday, April 26, 2013

MBOMA AWANIA UKOCHA TUIMU YA TAIFA CAMAROON
Ancien du PSG Aristide Arthode Deuhla-Patrick Mboma.JPGCHEZAJI wa zamani wa kimataifa wa Cameroon, Patrick Mboma ameonyesha nia yake ya kuifundisha timu ya taifa ya nchi hiyo na anakusudia kutuma maombi yake Shirikisho la Soka la Cameroon-Fecafoot siku moja baada ya Waziri wa Michezo Adoum Garoua kulitaka shirikisho hilo kufanya mchakato wa kupata kocha mpya. Mshambuliaji huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 42 alikuwemo katika kikosi cha nchi hiyo ambacho kilinyakuwa Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2000 na 2002 na pia kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika. Hata hivyo Mboma hajawahi kufundisha timu yoyote na wadau wa soka nchini humo wamedai kuwa mshambuliaji huyo wa zamani wa Paris Saint Germain na Parma hana uzoefu wa kutosha wa kumuwezesha kupewa nafasi ya kuinoa timu hiyo. Lakini pamoja na wadau kuponda uwezo wake Mboma amesema haimkatishi tamaa na atatuma maombi yake kuiwinda nafasi hiyo.

Kuhusu yeye
Full nameHenri Patrick M'Boma Dem
Date of birthNovember 15, 1970 (age 42)
Place of birthDoualaCameroon
Height1.85 m (6 ft 1 in)
Playing positionStriker
Timu alizocheza
YearsTeamApps(Gls)
1990–1992Paris Saint-Germain0(0)
1992–1994Châteauroux48(22)
1994–1995Paris Saint-Germain8(1)
1995–1996Metz17(4)
1996–1997Paris Saint-Germain8(1)
1997–1998Gamba Osaka34(29)
1998–2000Cagliari40(15)
2000–2001Parma24(5)
2002→ Sunderland (mkopo)9(1)
2002–2003Al-Ittihad28(12)
2003–2004Tokyo Verdy 196935(17)
2004–2005Vissel Kobe10(2)
Total261(109)
Timu ya taifa"
1995–2004Cameroon57(33)
TUZO-AWARDS
3.African Nations Cup top scorer: 2002
Cameroon national team
YearAppsGoals
199510
199611
1997106
199881
199943
200099
200194
2002105
200310
200444
Total5733

[edit]

RUVU SHOOTING, SIMBA SASA KUCHEZA MEI 5
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Ruvu Shooting na Simba iliyokuwa ichezwe leo (Aprili 25 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam sasa itafanyika Mei 5 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.

Mabadiliko hayo yametokana na Serikali kuutumia uwanja kwa ajili ya maandalizi ya sherehe za Muungano ambazo kitaifa zitafanyika kesho (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawaomba radhi washabiki kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na mabadiliko hayo na ghafla. Ratiba ya mechi nyingine za VPL zinabaki kama zilivyo.

Ligi hiyo inaendelea kesho (Aprili 26 mwaka huu) kwa mechi kati ya Coastal Union na Azam itakayochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wakati Jumapili (Aprili 28 mwaka huu) itakuwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni Simba dhidi ya Polisi Morogoro.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

OLIVER USO KWA USO NA FA
MSHAMBULIAJI wa Arsenal, Oliver Giroud amekishambulia Chama cha Soka nchini Uingereza-FA baada ya uamuzi wake wa kutupilia rufani yake ya kupinga kadi nyekundu aliyopewa. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alitolewa nje na mwamuzi Andre Marriner kwa kumchezea vibaya Stanislav Manolev wakati wa mchezo baina ya Arsenal na Fulham Jumamosi iliyopita hivyo kupelekea kufungiwa mechi tatu kwasababu ya kupewa kadi nyekundu ya moja kwa moja. Giroud mwenye umri wa miaka 26 amekuwa akijitetea kwamba aliteleza bahati mbaya kwenye tukio hilo na baada ya rufani yake kutupiliwa mbali amewakosoa FA kwa hatua waliyochukua. Giroud amesema ameshangazwa na hatua iliyochukuliwa na FA dhidi yake, sio kwamba imemuumiza ila anadhabu sheria za Uingereza zimekuwa kali sana ukilingasha na makosa yanayofanywa.

Thursday, April 25, 2013

TIMU ZA HISPAIN HOI BUNDASLIGA NOMA KWELI KWELI"TAZAMA MAMBO YALIVYOKUWA"

Katika mechi ya usiku  huu mchezaji aliye katika kiwango bora kabisa Robert Lewandowski  yameipa Borussia Dortmund ushindi wa 4-1 dhidi ya Real Madrid katika Nusu Fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya nchini Ujerumani.
Mabao ya mshambuliaji huyo wa Poland yameipa  Dortmund kujiweka katika nafasi nzuri ya kutingaa fainali ya klabu za bundasliga pekee  itakayopigwa Uwanja wa Wembley mwezi ujao, kufuatia jana Bayern Munich kuichapa 4-0 Barcelona nchini Ujerumani pia.
Lewandowski alifunga bao la kwanza dakika ya nane, kabla ya Cristiano Ronaldo kuisawazishia Real dakika ya 43.
Lakini lewandowski akaonyesha makali yake katika kipindi cha pili na kufunga mabao matatu zaidi dakika za 50, 55 na 67 kwa penalti.
Kocha wa Real, Mreno Jose Mourinho ambaye hakutegemea kipigo hicho kitakatifu, sasa real madrid inatakiwa  kutengeneza mipango ya kushinda 3-0 katika mchezo wa marudiano wiki ijayo, ili kuwapiku Dortmund.




UCL-NUSU FAINALI
RATIBA:
MARUDIANO
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
Jumanne Aprili 30
Real Madrid v Borussia Dortmund [1-4]
Jumatano Mei 1
Barcelona v Bayern Munich [0-4]
FAINALI
25 Mei 2013

UWANJA wa WEMBLEY, London.

Wednesday, April 24, 2013

TAFAKARI YA LEO 
TOMATH MULLER 
Taarifa kamili
Jina kamili”
Thomas Müller
Kuzaliwa”
13 September 1989 (age 23)
Mahali”
Weilheim, West Germany
Urefu”
1.86 m (6 ft 1 in)
Nafasi anayocheza”
Timu ya sasa
Current club
Number
25
Timu za vijana*
1993–2000
TSV Pähl
2000–2008
Timu ya Ukubwa*
Years
Team
Mechi
(Goli)
2008–2009
35
(16)
2008–sasa
131
(44)
Timu ya Taifa
2004–2005
6
(4)
2007
1
(0)
2008
1
(1)
2009–2010
6
(1)
2010–
41
(13)
AJIWEKA PEMBENI KAMATI YA FIFA
MJUMBE wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Nicolas Leoz kutoka Paraguay amejiuzulu wadhifa wake huo kutokana na kile alichodai kuwa na matatizo ya kiafya ikiwa ni siku chache kabla ya shirikisho hilo halijatangaza uchunguzi wa bakshishi katika michuano ya Kombe la Dunia. FIFA ilithibitisha kupokea barua ya Leoz mwenye umri wa miaka 84 ambaye pia ataachia ngazi wadhifa wake wa urais wa Shirikisho la Soka la Amerika Kusini-CONMEBOL. Leoz ambaye amefanyiwa upasuaji wa moyo mara kadhaa amekuwa mjumbe katika bodi ya FIFA kuanzia mwaka 1998 na amekuwa rais wa CONMEBOL kuanzia mwaka 1986. Katika barua yake Leoz amesisitiza kuwa uamuzi aliochukua ni binafsi kutokana na matatizo ya kiafya aliyonayo kwani hawezi kusafiri mara tano kwa mwaka kama ilivyokuwa zamani.


Ijapo kuwa matajiri wa london Man city wameonekana kuvutiwa na kiwango chake KLABU ya Paris Saint-Germain-PSG ya Ufaransa imemtengea mkataba mnono wa euro milioni 8.5 kwa msimu mshambuliaji nyota wa Napoli ya Italia Edinson Cavani. Imeripotiwa na vyombo vua habari nchini humo kuwa mkurugenzi wa michezo wa klabu ya PSG, Leonardo ameshafanya vikao kadhaa na wakala wa nyota huyo kuzungumzia uhamisho wake kutoka Napoli ambao unakaribia kufikia kiasi cha euro milioni 63. Mbali na PSG vilabu vingine vikubwa barani Ulaya ambavyo vimeonyesha nia ya kuhitaji sahihi ya nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay ni pamoja na Real Madrid, Manchester City na Chelsea. Cavani mwenye umri wa miaka 26 ana mkataba na Napoli mpaka 2015 ambao unamuwezesha kulipwa kiasi cha euro milioni 1.4 kwa msimu.
MKALI RONALDINHO APEWA UNAHODHA VS CHILE:;
RONALDINHO anatarajiwa kupewa unahodha wa timu ya taifa ya Brazil katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Chile hatua ambayo itamuweka katika nafasi nzuri ya kujumuishwa katika kikosi kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Shirikisho.
Kocha wa Brazil Luis Felipe Scolari ameonyesha matumaini yake kwa Ronaldinho ambaye amaewahi kunyakuwa tuzo ya mchzaji bora wa dunia mara mbili kwa kumpa unahodha kwenye mechi ya mwisho kabla hajatangaza kikosi cha michuano ya Kombe la Shirikisho.
Scolari tayari amebainisha kuwa kuna uwezekano akamchukua kati ya Ronaldinho au Kaka kwa ajili ya michuano hiyo itakayofanyika June mwaka huu. Kaka atakosa mchezo dhidi ya Chile kwasababu ni wachezaji wanaocheza katika vilabu vya Brazil peke ndio waliochaguliwa kwa ajili ya mchezo huo kirafiki kitendo ambacho kinampa nafasi kubwa kama akionyesha kiwango kizuri.