MSHAMBULIAJI nyota wa
kimataifa wa Argentina Lionel Messi ametua nchini Senegal jana kwa ndege
binafsi na kulakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Dakar na mashabiki wa
soka na vijana wadogo waliotoka pembe mbalimbali za nchi hiyo. Nyota
huyo anayecheza katika klabu ya Barcelona alialikwa na shule ya soka ya
Qatar Aspire ambao wana tawi lao nchini humo kwa ajili ya kwenda kwenye
kampeni ya kupiga vita ugonjwa wa malaria. Kwa
mujibu wa waratibu ya ziara hiyo maelfu ya neti ambazo zitakuwa na
picha ya Messi zitasambazwa kwa watoto na familia katika vijiji
mbalimbali nchini humo. Messi
atasafiri kwa helikopta kwenda Saly eneo la karibu na mji wa Dakar
ambapo atatembelea nyumba za yatima na kuongea na wenyeji wa hapo jinsi
watakavyoweza kujikinga na malaria.
Friday, June 28, 2013
HISPAIN YATINGA FAINALI SASA KUUMANA NA WENYEJI BRAZIL
Wataliano walifungwa na Waspanyola
katika Fainali ya Euro mwaka jana wameshindwa kulipa kisasi na sasa
Fainali ya michuano hiyo mwaka huu Jumapili Uwanja wa Maracana,
itawakutanisha wenyeji La Roja na Brazil wenyeji.
Leonardo Bonucci wa Italia alikosa moja
ya penalti 14 na Jesus Navas akaweka nyavuni mkwaju wa mwisho na
kuipeleka Hispania Fainali.
TUTAFAKARI KUELEKEA FAINALI JE NANI KUIBUKA NA UBINGWA"
USO KWA USO
JUMLA: Mechi 8
USHINDI: Brazil 4 Spain 2
SARE: 2
MAGOLI JUMLA: Brazil 11 Spain 8
Mechi zenyewe:
FIFA KOMBE LA DUNIA:
Jumla: Mechi 5
USHINDI: Brazil 3 Spain 1
SARE: 1
MAGOLI JUMLA: Brazil 10 Spain 5
1986 Spain 0 Brazil 1 {Guadalajara, Mexico}
1978 Brazil 0 Spain 0 {Mar Del Plata, Argentina}
1962 Brazil 2 Spain 1 {Vina Del Mar, Chile}
1950 Brazil 6 Spain 1 {Rio De Janeiro, Brazil}
1934 Spain 3 Brazil 1 {Genoa, Italy}
KIRAFIKI:
Jumla: Mechi 3
USHINDI: Brazil 1 Spain 1
SARE: 1
MAGOLI: Spain 3 Brazil 1
1999 Spain 0 Brazil 0 {Vigo, Spain}
1990 Spain 3 Brazil 0 {Gijon, Spain}
1981 Brazil 1 Spain 0 {Salvador, Brazil}
WAWILI WACHAGULIWA KITUO CHA VIPAJI ASPIRE
Wachezaji
wawili kutoka Tanzania wamechaguliwa miongoni mwa 50 waliofanyiwa
majaribio nchini Uganda kwa ajili ya kuingia katika kituo cha kuendeleza
vipaji (centre of excellence) kilichoko Doha nchini Qatar kupitia
mpango wa kukuza vipaji wa Aspire Football Dream.
Abdulrasul
Tahir Bitebo (15) ambaye ni mshambuliaji kutoka Kituo cha Uwanja wa
Karume, na Martin Omela Tangazi (14) ambaye ni beki kutoka Kituo cha
Ukonga ndiyo waliochaguliwa kutoka Tanzania kuingia katika kituo ambapo
watakaa kwa mwezi mmoja kabla ya kusaini mkataba rasmi wa kuendelezwa.
Wachezaji
wengine walikuwa wakitoka katika nchi za Uganda na Kenya. Mchezaji
mwingine aliyefuzu katika nafasi tatu zilizokuwepo ni kutoka nchini
Kenya.
Mpango
wa Aspire Football Dream unafadhiliwa na Mtoto wa Mfalme wa Qatar
katika nchi 16 duniani, na kwa hapa nchini uko chini ya Idara ya Ufundi
ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
TFF
ina jumla ya vituo 14 vya kuendeleza vipaji kupitia mpango huo wa
Aspire Football Dream. Vituo hivyo ni Karume, Kigamboni, Tandika, Kawe,
Ukonga, Kitunda, Mbagala, Magomeni, Makongo, na Tabata vilivyo katika
Mkoa wa Dar es Salaam. Vingine ni Bagamoyo kilichopo mkoani Pwani,
Morogoro, Arusha na Moshi mkoani Kilimanjaro.
Kituo kingine cha kuendeleza vipaji (centre of excellence) cha Aspire kipo Dakar nchini Senegal.
TFF KUENDESHA KOZI SITA KATI YA JULAI- SEPTEMBA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaendesha kozi sita tofauti za mpira wa miguu kati ya Julai na Septemba mwaka huu.
Kozi
hizo ni FIFA 11 For Health itakayofanyika Hombolo mkoani Dodoma kuanzia
Julai 8 hadi 19 mwaka huu. Julai 6 hadi 15 mwaka huu kutakuwa na kozi
ya mpira wa miguu wa ufukweni (Beach Soccer) itakayofanyika jijini Dar
es Salaam.
Waamuzi
wa FIFA nao watakuwa na kozi itakayofanyika kati ya Agosti 22 hadi 26
mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati kozi ya ukocha kwa ajili ya Copa
Coca-Cola itafanyika jijini Dar es Salaam kati ya Agosti 12 na 17 mwaka
huu.
Vilevile kutakuwa na kozi ya mpango
wa grassroots unaolenga wachezaji mpira wa miguu (wasichana na
wavulana) wenye umri kuanzia miaka 6-12 itafanyika kuanzia Septemba 9
hadi 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati tamasha (festival) la
grassroots litafanyika Uwanja wa Karume, Septemba 14 mwaka huu.
RCL KUKAMILISHA HATUA YA NNE JUMAPILI
Mechi
za marudiano za hatua ya nne ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL)
zitachezwa Jumapili (Juni 30 mwaka huu) kwenye viwanja vya Sokoine
jijini Mbeya, na Kambarage mjini Shinyanga.
Friends
Rangers ya Dar es Salaam ambayo katika mechi ya kwanza ilifungwa
nyumbani mabao 3-0 itakuwa mgeni wa Stand United FC mjini Shinyanga
wakati Kimondo SC itaikaribisha Polisi Jamii ya Mara jijini Mbeya.
Katika mechi ya kwanza timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.
Hatua
ya mwisho ya RCL itachezwa Julai 3 mwaka huu kwa mechi za kwanza wakati
zile za marudiano zitafanyika Julai 7 mwaka huu. Timu tatu za kwanza
zitapanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
TENGA ASEMA MKUTANO UPO PALEPALE"-MKUU WA TFF
Wadau wengi wamekuwa wakihoji kufanyika kwa Mkutano huo wakati Nchi inakabiliwa na Mechi muhimu Siku hiyo hiyo huku wengine wakidiriki kudai kuna walakini ndani yake.
Lakini Rais wa TFF, Leodegar Tenga, amefafanua kuwa vitu hivyo viwili haviwezi kuleta mgongano kwani Mechi itachezwa kwa Dakika 90 na Mkutano Mkuu umepangwa kuwa wa Siku mbili.
Tenga alisema: “Hamna njama zozote. Vitu hivyo viwili vitaendelea kama ilivyopangwa.”
Akifafanua, Tenga alisema Wajumbe wa Mkutano Mkuu wamezoea kujadili Ajenda hadi 12 katika Siku moja lakini safari hii Ajenda ni moja tu na imepangiwa Siku mbili.
Ajenda ya Mkutano Mkuu huo ni kujadili na kupitisha Mabadiliko ya Katiba ili kuruhusu Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho hilo ufanyike kama ilivyoagizwa na FIFA.
Awali Uchaguzi ulikuwa ufanyike hapo Februari 24 lakini ukatokea mgongano mkubwa baada ya baadhi ya Wagombea kufutwa na pia madai kuwa Katiba ilibadilishwa bila kufuata taratibu.
Akifafanua zaidi, Tenga alisema upo uwezekano mkubwa kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu kumaliza Kikao chao kabla hata Mechi kuchezwa.
Thursday, June 27, 2013
FEDERER ASEMA BADO ATAENDELEA KUCHEZA MCHEZO HUO".
Mchezaji tenesi mahiri wa
Switzerland, Roger Federer amesisitiza kuwa bado ataendelea kucheza
mchezo huo kwa miaka mingi ijayo pamoja na kutolewa mapema katika
michuano ya Wimbledon jana. Nyota
huyo ambaye anashika namba tatu katika orodha za ubora duniani amesema
hana hofu yoyote pamoja na kutolewa na Sergiy Stakhovisky wa Ukraine
katika mzunguko wa pili wa michuano hiyo. Katika
mchezo huo Federer aliburuzwa kwa kufungwa 6-7 7-6 7-5 7-6 na
Stakhovsky anayeshika namba 116 katika orodha za ubora duniani. Baadhi
ya wadau wa mchezo huo wamekuwa wakihoji kiwango cha Federer mwenye
umri wa miaka 31 na kudai kuwa amekwisha lakini mwenye amesisitiza kuwa
bado yuko fiti na ataendelea kucheza kwa miaka kadhaa ijayo. Kwa
upande wa wanawake mwanadada nyota anayeshika namba mbili kwa ubora kwa
upande wanawake Maria Sharapova wa Urusi naye aliyaaga mashindano hayo
baada ya kukubali kipigo cha 6-3 6-4 kutoka kwa Michelle Larcher de
Brito wa Ureno anayeshika namba 131 katika orodha hizo.
SCOLARI AMEKIRI KUWA TIMUYA BRAZIL BADO HAIKO FITI-DUNIA
KOCHA wa timu ya taifa ya
Brazil, Luis Felipe Scolari amekiri kuwa kikosi chake bado hakiwezi
kuanza kuweka matumaini ya kutwaa kombe lao la sita la Kombe la Dunia mwaka ujao
lakini wamebakisha mechi moja kunyakuwa taji lao la tatu la Kombe la
Shirikisho baada ya kuiengua Uruguay katika hatua ya nusu fainali. Scolari
amesema anafikiri kikosi hicho kimefikia mahali pazuri lakini bado kuna
vitu vingi vya kufanyia marekebisho mpaka kikamilike kwa ajili ya
michuano ya Kombe la Dunia mwakani. Kocha
huyo aliendelea kudai kuwa kwasasa wanahamishia nguvu zao katika mchezo
wa fainali na baada ya hapo wataangalia mapungufu yalijitokeza ili
kuhakikisha wanakuwa na kikosi imara kitakachoweza kulibakisha Kombe la
Dunia nyumbani. Brazil
kwasasa wanasubiri mshindi wa nusu fainali nyingine ya michuano hiyo
itakayopigwa baadae leo kati ya mabingwa wa Ulaya na Dunia Hispania
watakaochuana na Italia.
ABEL NA KISPANG WAJITOA TIMU YA WANARIADHA WA KENYA
BINGWA mara mbili wa
dunia mashindano ya mbio ndefu Abel Kirui na mshindi wa medali ya shaba
katika michuano ya olimpiki Wilson Kipsang wamejitoa katika timu ya
wanariadha ya Kenya itakayoshiriki michuano ya riadha ya dunia
itakayofanyika jijini Moscow. Makamu
wa rais wa Chama cha Riadha cha nchi hiyo Paul Mutwii amedai kuwa Kurui
aliwafahamisha kwamba amejitoa kwasababu ya kusumbuliwa na majeraha
wakati Kipsang yeye amewaambia kuwa ana majukumu mengine. Kirui
ambaye alishinda taji la dunia la mbio ndefu mwaka 2009 na 2011 amekuwa
akisumbuliwa jeraha la kifundo cha mguu wake wa kulia na anatarajiwa
kukaa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki sita. Kuziba
nafasi hizo Mutwii amesema wamewaita Mike Kipyego ambaye alishinda mbio
za marathon jijini Tokyo mwaka jana, Bernard Kipyego mshindi wa medali
ya fedha mbio za nusu marathon 2009 na bingwa wa mbio za marathoni za
Paris Peter Some. Kikosi cha mwisho kitakachokwenda Moscow kitatajwa mwezi ujao baada ya kufanyika mbioza mchujo.
Subscribe to:
Posts (Atom)




