CLUB ya Real Madrid ya
Hispania imetajwa kuwa klabu yenye thamani zaidi katika orodha ya timu
za michezo 50 zenye thamani zaidi duniani iliyotolewa na jarida Forbes
la nchini Marekani. Katika orodha hizo timu za Ligi Kuu ya Mpira wa Kimarekani-NFL ndizo zilizoonekana kutawala kwa kiasi kikubwa. Kwa
mujibu wa taarifa zilizochapishwa na jarida hilo Madrid ambao ni
mabingwa mara tisa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya wana utajiri unaofikia dola
bilioni 3.3, utajiri huo ukiwa umeongezeka kwa dola bilioni 1.88
kulinganisha na mwaka uliopita baada ya kuongeza mapato yao kwa kuingia
mikataba na kampuni za Adidas na Shirika la Ndege la Emirates. Manchester
United wamepigwa kikumbo na Madrid na kushuka mpaka nafasi ya pili
wakiwa na utajiri wa dola bilioni 3.17 wakati mabingwa wa Hispania
Barcelona wao wamekwea kutoka nafasi ya tano mpaka ya tatu wakiwa na
utajiri unaofikia dola bilioni 2.6. Nafasi
ya nne inashikiliwa na timu ya Baseball ya Marekani ya New York Yankees
ambao wana dola bilioni 2.3, wakifuatiwa na Dallas Cowboys ya NFL dola
bilioni 2.1 na New England Patriots dola bilioni 1.6. Nyingine
ni Los Angeles Dodgers ya baseball dola bilioni 1.6, timu za NFL
Washington Redskins na New York Giant pamoja na klabu ya soka ya Arsenal
ya Uingereza ambazo zote hizo zina utajiri wa dola bilioni 1.3.
Tuesday, July 16, 2013
KAMPUNI YA VIFAA VYA MICHEZO ADIDAS YA SIMAMISHA MKATABA WA TYSON GAY
Kampuni ya vifaa vya
michezo ya Adidas imesimamisha mkataba wake wa udhamini na mwanariadha
nyota wa mbio fupi Tyson Gay wa Marekani baada ya kukutwa na
chembechembe za dawa za kuongeza nguvu. Msemaji
wa kampuni alidai kuwa awameshtushwa na tuhuma hizo kwa Gay na hata
kama bado hajakutwa na hatia ya kosa hilo moja kwa moja kampuni
itasimamisha udhamini wake mpaka hapo hukumu itakapotolewa. Gay
mwenye umri wa miaka 30, ndio mwanariadha wa pili mwenye kasi zaidi
duniani katika mbio za mita 100 akiwa sambamba na Yohan Blake wa Jamaica
na pia ndiye mwanariadha aliyeweka rekodi ya kasi zaidi kwa mwaka huu. Nyota
huyo ambaye aliwahi kuwa bingwa wa dunia katika mbio za mita 100, 200
na mita 400 kupokezana vijiti mwaka 2007 alishindwa kukata tuhuma hizo
na kudai kuwa alimwamini mtu ambaye alimwangusha na hivyo atapokea
adhabu yoyote atakayopewa.
Sunday, July 14, 2013
Coastal Union yanasa saini ya Udula wa Bandari ya Kenya
Na Paul Mkai,Tanga.
UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga umesema tayari umeshamalizana na aliyekuwa mshambulizi wa timu ya Bandari ya Kenya,Christian Udula kwa mkataba wa miaka miwili kwa ajili ya kuichezea timu kwenye msimu mpya ambao utaanza Agosti mwaka huu.
Akizungumza na Blogg hii,Katibu Mkuu wa timu ya Coastal Union ya Tanga,Kassim El Siagi alisema baada ya kumalizina na mchezaji huyo anatarajiwa kutua mkoani Tanga wiki ya leo akiwa na mchezaji mwengine wa timu hiyo Jerry Santos.
Siagi alisema msimu huu wamedhamiri kufanya usajili wa nguvu ambao utaifanya timu hiyo kuwa tishio kwenye mechi zao za Ligi kuu ya Tanzania bara kwani malengo yao ni kuchukua ubingwa wa mashindano hayo makubwa hapa nchini.
Aidha alisema timu hiyo itacheza mechi mbalimbali za majaribio nchini Kenya na timu za Sofapaka,Bandari na Goromahia lengo likiwa ni kukipa makali kikosi hicho ambacho kinatarajiwa kuwa tishio.
Katibu huyo aliwataka wapenzi na mashabiki wa timu hiyo kuendelea kujitokeza kuisapoti timu hiyo ili iweze kutimiza azma yao waliyojiwekea kwenye michuano hiyo.
Mwisho.
UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga umesema tayari umeshamalizana na aliyekuwa mshambulizi wa timu ya Bandari ya Kenya,Christian Udula kwa mkataba wa miaka miwili kwa ajili ya kuichezea timu kwenye msimu mpya ambao utaanza Agosti mwaka huu.
Akizungumza na Blogg hii,Katibu Mkuu wa timu ya Coastal Union ya Tanga,Kassim El Siagi alisema baada ya kumalizina na mchezaji huyo anatarajiwa kutua mkoani Tanga wiki ya leo akiwa na mchezaji mwengine wa timu hiyo Jerry Santos.
Siagi alisema msimu huu wamedhamiri kufanya usajili wa nguvu ambao utaifanya timu hiyo kuwa tishio kwenye mechi zao za Ligi kuu ya Tanzania bara kwani malengo yao ni kuchukua ubingwa wa mashindano hayo makubwa hapa nchini.
Aidha alisema timu hiyo itacheza mechi mbalimbali za majaribio nchini Kenya na timu za Sofapaka,Bandari na Goromahia lengo likiwa ni kukipa makali kikosi hicho ambacho kinatarajiwa kuwa tishio.
Katibu huyo aliwataka wapenzi na mashabiki wa timu hiyo kuendelea kujitokeza kuisapoti timu hiyo ili iweze kutimiza azma yao waliyojiwekea kwenye michuano hiyo.
Mwisho.
Friday, July 12, 2013
KAMPUNI YA MADUKA NCHINI BRAZIL WATISHIA KWENDA MAHAKANI KUHUSU USAJILI NEYMAR
Kampuni ya DIS
inayomiliki maduka makubwa nchini Brazil na ambao wanamiliki asilimia 40
ya haki za usajili wa Neymar wametishia kwenda mahakamani kuhusiana na
mgao wao kwa nyota huyaa o katika usajili wake kwenda Barcelona. Kampuni
hiyo inayoendeshwa na Idi Sonda imedai kuwa na haki ya kupata fedha
zaidi juu ya makubaliano ya ziada kati ya klabu ya Santos na Barcelona
ambayo yako nje ya ada ya uhamisho wake ambayo ilifikia kiasi cha euro
milioni 57. Mkurugenzi
Mtendaji wa DIS, Roberto Moreno ameomba kupewa taarifa kamili ya hati
ya uhamisho wa Neymar kwenda Barcelona ili kupata ufafanuzi kuhusu
malipo ya baadae watakayopewa Santos. Moreno
amesema mpaka kipindi hicho hawajaonyeshwa hati yoyote, hivyo atafunga
safari kwenda makao makuu ya Santos kufuatilia hati hiyo na baada ya
hapo wataamua kama watahitaji kwenda mahamani. Hatua
ya kampuni hiyo imekuja kufuatia taarifa zilitolewa na vyombo vya
habari nchini humo kwamba Santos watapata nyongeza ya euro milioni mbili
kama mchezaji huyo atakuwemo katika orodha ya wachezaji watatu kwenye
tuzo ya Ballon d’Or kwenye kipindi cha miaka mitano ijayo.FIFA YA FUATILIA KWA KARIBU KASHFA YA UPANGAJI MATOKEO
SHIRIKISHO la Soka
Duniani-FIFA linafuatilia kwa karibu kashfa ya upangaji matokeo
inayozikabili vilabu viwili vya soka vya ridhaa nchini Nigeria
iliyotokea wiki iliyopita. Katika
matokeo ambayo yanaonekana kama ya mchezo wa kriketi, klabu ya Plateau
United Feeders iliibugiza Akurba FC kwa mabao 79-0 wakati Police Machine
wao waliitandika Bubayaro FC kwa mabao 67-0 mwishoni mwa wiki
iliyopita. Hatua uchunguzi kwa vilabu hivyo imekuja kutokana na timu hizo kuhitaji matokeo ya aina hiyo ili waweze kupanda daraja. Ambapo
katika taarifa yake FIFA imedai kuwa inafuatilia tukio hilo la tmu hizo
za Nigeria kwa karibu ili kuona jinsi gani Shirikisho la Soka la nchi
hiyo, NFF litatatua tatizo hilo. FIFA
inafanya hivyo kwa kutambua kuwa suala hilo ni la ndani hivyo NFF ina
wajibu wa kufanya uchunguzi na kuchukua hatua zinazostahiki kama
ikigundulika aina yoyote ya udanganyifu katika mechi hizo.
TAIFA STARS SASA MMEIVA KUPAMBANA- TENGA
Rais
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amesema
kikosi cha Taifa Stars sasa kina uwezo wa kushindana katika mashindano
yoyote, kwani tayari kimeiva.
Akizungumza
na wachezaji wa timu hiyo kambini kwao hoteli ya Tansoma, Dar es
Salaam, Rais Tenga aliwaambia kuwa kiwango walichoonesha kwenye mechi
zilizopita za mchujo za Kombe la Dunia dhidi ya Morocco na Ivory Coast
kimethibitisha hilo.
“Kiwango
mlichoonyesha katika mechi hizo kila Mtanzania anayewafuatilia
amekiona, hivyo hatuna shaka kuwa mtatuwakilisha vizuri kwenye mechi ya
kesho dhidi ya Uganda,” amesema Rais Tenga na kuwataka kupigana kwa
ajili ya Tanzania.
Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kesho (Julai 13 mwaka
huu) saa 9 kamili alasiri Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itacheza na
Uganda (The Cranes) katika mechi ya kwanza ya raundi ya mwisho kuwania
tiketi ya kucheza Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika
Kusini.
Rais
Tenga amesema TFF, mdhamini Kilimanjaro Premium Lager, Kamati ya
Ushindi na Watanzania kwa ujumla wanawaunga mkono kwani wamekuwa
wakiboresha kiwango chao kila wanavyozidi kucheza mechi tangu wake chini
ya Kocha Kim Poulsen, Mei mwaka jana.
Wakati
huo huo, Rais Tenga ameahidi kumpatia tiketi ya kwenda Uganda kwenye
mechi ya marudiano mshabiki Wiseman Mwakyusa Luvanda anayetembea kwa
miguu kutoka Mbeya kuja Dar es Salaam kushuhudia mechi ya kesho.
“Kama
ni kweli anakuja kwa kutembea, huyu ameonyesha kiwango kikubwa cha
uzalendo kwa timu ya Taifa, nitampatia tiketi ya kwenda Kampala
kuishangilia Taifa Stars kwenye mechi ya marudiano,” amesema Rais Tenga.
POULSEN, MICHO WATABIRI MECHI KALI
Makocha
wa timu hizo Kim Poulsen wa Taifa Stars na Sredojvic Micho wa The
Cranes wamesema mechi ya kesho itakuwa ngumu kwa vile kila mmoja
amejiandaa kuhakikisha anafanya vizuri.
Wakizungumza
na Waandishi wa Habari leo, makocha wote waliezea ubora wa wapinzani
wao, lakini wakasisitiza kuwa wanaingia uwanjani kuhakikisha wanashinda
ili kujiweka katika mazingira mazuri kwa ajili ya mechi ya marudiano
itakayochezwa Kampala wiki mbili zijazo.
Kim
alisema Uganda ndiyo inayoongoza kwa ubora wa viwango vya FIFA katika
ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati, hivyo ni changamoto kwao ingawa
wachezaji wake tayari wamejipanga vizuri kwa ajili ya mechi hiyo.
Naye
Micho aliyefuatana na nahodha wake Hassan Wasswa alisema Taifa Stars
imekuwa ikifanya vizuri tangu iwe chini ya Kim, na itakuwa na wachezaji
tisa wa kikosi cha kwanza kinachocheza mechi za mchujo za Kombe la Dunia
wakati kwa upande wake atakuwa na wachezaji wawili tu.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Thursday, July 11, 2013
DROGBA ATANGAZA KUJENGA HOSPITAL 5 ZA KINA MAMA NA WATOTO"NCHINI IVORY" COAST
Uamuzi huu umetangazwa huko Mjini
Abidjan na Katibu wa Didier Drogba Foundation, Guy Roland Tanoh, ambae
amesema itajengwa Hospitali moja katika Miji mitano ya Ivory Coast
ambayo ni Abidjan, Yamoussoukro, Man, Korhogo na San Pedro.
Kwenye Tafrija huko
London tulichangisha na kukusanya Dola Milioni 4 na zilizobaki si tatizo
ili kukamilisha Mradi huu ambao uko moyoni kabisa mwa Drogba.”
Taasisi ya Didier Drogba ilianzishwa
Mwaka 2007 na ilipanga kujenga Hospitali yenye gharama ya Pauni Milioni 3
lakini hadi leo ilikuwa haijajengwa na Tanoh hakufafanua kama Hospitali
hiyo ni moja ya hizo tano zitakazojengwa.
Wakati huo, Drogba, mwenye Miaka 35 hivi
sasa na ambae anachezea Klabu ya Turkey Galatasaray, alisema ujenzi wa
Hospitali hiyo utatokana na malipo ya Picha na Matangazo yake na Kampuni
ya Pepsi.
Subscribe to:
Posts (Atom)



