MENEJA wa klabu ya AC
Milan, Clerence Seedorf amedai kuwa klabu hiyo inaendelea kuimarika
pamoja na kupata sare ya kufungana mabao 1-1 na Torino katika mchezo wa
Serie A uliofanyika jana. Katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa
San Siro wageni Torino ndio walioanza kupata bao kipindi cha kwanza
kupitia kwa Ciro Immobile lakini wenyeji walirudisha bao hilo katika
kipindi cha pili kupitia kwa Adil Rami. Sare hiyo inaonekana
kumfurahisha Seedorf ambaye anadai kuwa wachezaji wake wameanza kuzoea
mfumo anaofundisha. Seedorf amesema ni jambo jema kuona kikosi chake
kikianza kuelewana taratibu na kudai kuwa ni dalili nzuri za kufanya
vyema huko mbele. Sare hiyo imeiacha Milan katika nafasi ya tisa ya
Serie A, wakiwa wanajikongoja toka alipotimuliwa kocha Massimiliano
Allegri Januari mwaka huu.
Sunday, February 2, 2014
LIBYA WATWAA UBINGWA WA CHAN KWA MARA YA KWANZA VS GHANA
TIMU ya taifa ya Libya
wametawadhwa mabingwa wapya wa michuano ya Mataifa ya Afrika kwa
wachezaji wa ndani, CHAN baada ya kuifunga Ghana kwa changamoto ya
mikwaju ya penati katika mchezo wa fainali uliochezwa katika Uwanja wa
Cape Town nchini Afrika Kusini. Libya walinyakuwa taji lao hilo la
kwanza la kihistoria kwa kuigaragaza Ghana kwa penati 4-3 baada ya
mchezo huo kumalizika bila ya kufungana mpaka katika muda wa nyongeza.
Hiyo inakuwa mechi ya tatu kwa Libya kushinda kwa changamoto ya mikwaju
ya penati baada ya kuziengua Gabon na Zimbabwe katika hatua ya robo
fainali na nusu fainali. Kwa wa mechi ya kutafuta mshindi wa tatu
Nigeria walifanikiwa kuibuka kidedea baada ya kuifunga Zimbabwe kwa bao
1-0.
TPLB YATAKIWA KUKETI MEZANI KUTATHIMINI MECHI YA STEND UNITED VS KANEMBWA JKT
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la
Mpira wa Tanzania (TFF) imeiagiza Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) ifanyie
marejeo (review) uamuzi wake wa kuagiza mechi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL)
irudiwe mkoani Tabora.
Maagizo hayo yametolewa na Kamati ya
Utendaji iliyokutana jana (Februari 1 mwaka huu) baada ya kupokea vielelezo
vipya kuhusiana na mechi hiyo iliyochezwa Novemba 22 mwaka jana mjini
Shinyanga.
Mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa
Kambarage ilivunjwa na mwamuzi dakika ya 87 baada ya kupigwa na wachezaji wa
Kanembwa JKT.
Pia Kamati ya Nidhamu ya TFF
inatarajiwa kukutana wiki ijayo kujadili tukio hilo la Shinyanga wakiwemo
wachezaji wanane wa Kanembwa JKT waliripotiwa kumpiga mwamuzi wa mechi hiyo.
TFF,CRDB KUKETI KUTATHIMINI TIKETI ZA ELEKTRONIC
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF) imeagiza kifanyike kikao cha dharura kati ya
Sekretarieti ya TFF, Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) na benki ya CRDB ili
kutathimini maendeleo ya matumizi ya tiketi za elektroniki.
Lengo la kikao hicho ni kutathimini
maendeleo ya utekelezaji wa mfumo huo wa tiketi za elektroniki ni kutafuta
ufumbuzi pamoja changamoto zake.
Viwanja vinane nchini vimefungwa
mfumo huo wa tiketi za elektroniki. Viwanja hivyo ni Uwanja wa Azam uliopo
Chamazi, Uwanja wa Kaitaba, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Uwanja wa Jamhuri,
Morogoro, Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid,
Uwanja wa Mkwakwani, na CCM Kirumba.
TARIMBA MWENYEKITI WA ZAMANI WA YANGA APEWA KAMATI YA NIDHAMU TFF
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imefanya uteuzi wa wajumbe kuunda kamati mbili za
awali za haki, na kamati mbili za rufani za vyombo hivyo.
Rais wa zamani wa Yanga, Tarimba
Abbas ambaye pia kitaaluma ni mwanasheria ataongoza Kamati ya Nidhamu. Wajumbe
wanaounda kamati hiyo ni Wakili Jerome Msemwa (Makamu Mwenyekiti), Kassim Dau,
Nassoro Duduma na Kitwana Manara.
Kamati ya Rufani ya Nidhamu
inaendelea kuongozwa na Profesa Mgongo Fimbo wakati makamu wake ni Wakili
Hamidu Mbwezeleni. Wajumbe wengine wa kamati hiyo ni Titus Bandawe, Twaha
Mtengera na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) mstaafu Boniface Mpaze.
Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio
ambaye pia kitaaluma ni mwanasheria anaongoza Kamati ya Maadili. Wajumbe ni
Wakili Ezekiel Maganja, Wakili Victoria Mandari, Kanali mstaafu Enos Mfuru na
Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi, Said Mtanda.
Kamati ya Rufani ya Maadili inaundwa
na Jaji mstaafu Stephen Ihema (Mwenyekiti), Wakili Alesia Mbuya (Makamu
Mwenyekiti), Lilian Kitomari, Jabir Shekimweri na Chabanga Hassan Dyamwale.
Tuesday, January 28, 2014
TFF YAANZA KUUZA TIKETI ZA ELECTRONIC COAST VS YANGA
Mauzo
ya tiketi za elektroniki kwa mechi tatu kati ya nne za Ligi Kuu ya Vodacom
(VPL) zitakazochezwa keshokutwa (Januari 27 mwaka huu) tayari yameanza, hivyo
wanatakiwa kununua mapema.
Mechi
hizo ni kati ya Coastal Union na Yanga itakayofanyika Uwanja wa Mkwakwani
jijini Tanga, Kagera Sugar na Mtibwa Sugar itakayochezwa Uwanja wa Kaitaba
mjini Bukoba na ile ya Azam dhidi ya Rhino Rangers kwenye Uwanja wa Azam
Complex.
Kwa
washabiki wa Dar es Salaam watakaokwenda Tanga kushuhudia mechi kati ya Coastal
Union na Yanga wanashauriwa kuanza safari wakiwa na tiketi zao mikononi, hasa
kwa wale watakaonunua kupitia maduka ya Fahari Huduma.
Tiketi
pia zinaweza kununuliwa kupitia mtandao wa M-Pesa kwa kupiga namba *150*03*02#.
Kwa wanaotumia CRDB simbanking wanaingia kawaida kwa *150*03.
Vilevile
tunawakumbusha washabiki kuwa kwa viwanja ambavyo tayari vina mfumo wa tiketi
za elektroniki hakuna tiketi zitakazouzwa uwanjani, hivyo wanaokwenda kwenye
mechi wanatakiwa kuwa na tiketi zao mikononi.
YANGA YAANZA LIGI KWA KITITA CHA PESA MIL.86
Mechi
za Ligi Kuu ya Vodacom zilizohusisha timu za Simba na Yanga na kuchezwa Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam wikiendi zimeingiza jumla ya sh. 139,850,000.
Yanga
iliyoibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ashanti United pambano lake
liliingiza sh. 86,035,000 kutokana na watazamaji 14,261. Mechi ya Simba ambayo
ilishinda bao 1-0 dhidi ya Rhino Rangers kutoka Tabora iliingiza sh. 53,815,00
kwa watazamaji 9,629.
Mgawanyo
kwa mechi ya Yanga ulikuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 13,123,983.05,
gharama za kuchapa tiketi sh. 2,910,300 wakati kila klabu ilipata sh.
20,650,211.50.
Uwanja
sh. 10,500,107.54, gharama za mechi sh. 6,300,064.53, Bodi ya Ligi sh. 6,300,064.53,
Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 3,150,032.26 na Chama cha Mpira
wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 2,450,025.09.
Mechi
ya Simba mgawo ulikuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 8,209,067.80,
gharama za kuchapa tiketi sh. 2,910,300 wakati kila klabu ilipata sh.
12,595,211.50.
Uwanja
sh. 6,404,344.83, gharama za mechi sh. 3,842,606.90, Bodi ya Ligi sh.
3,842,606.90, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,921,303.45 na
Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,494,347.13.
Vilevile
tiketi zinapatikana kupitia maduka ya CRDB Fahari Huduma ambayo yapo katika
maeneo mbalimbali nchini. Watakaonunua kupitia maduka hayo watapata tiketi na
kwenda moja kwa moja uwanjani.
Subscribe to:
Posts (Atom)


