Saturday, February 15, 2014

JK: MTANDAO WA UJANGILI WAJULIKANA


Rais Jakaya Kikwete, amesema mtandao wa majangili unajulikana na jitihada za serikali zimefanikiwa kukamata vigogo 40 walio kwenye mtandao mkubwa wa biashara ya nyara hizo za serikali.
 
Akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya BBC , jana asubuhi alisema watuhumiwa hao wamebainika kuwa wanajihusisha na mtandao kwenye ukanda wa Kaskazini na kwamba tajiri mkuu wa biashara hiyo naye amefahamika na kwamba anapatikana mkoani Arusha .
Akizungumza katika kipindi cha Amka na BBC , alikozungumzia ujangili, alieleza kuwa mtandao umefahamika na kwamba unahusisha matajiri na miongoni mwa watu hao 40 yupo tajiri huyo wa Arusha ambaye hakutaka kumtaja jina redioni.

“Tumeutambua mtandao huo hadi wakubwa zao ni matajari pale Arusha kuna mmoja mkubwa ambaye sitaki kumtaja jina alikuwa akiendesha biashara hiyo naye yupo kwenye kundi hili la watu 40 kazi iliyokuwa ikifanyika ni kuutambua huo mtandao kwa upana,” alisema.

Awali alisema Tanzania ilikuwa na tembo wengi barani Afrika na hata duniani wakati huo baada ya Uhuru walikuwa 350,000 na ilipofikia mwaka 1987 walipungua hadi 55,000.
Alisema hapo ndipo serikali ilipofanya maamuzi ya kuingiza jeshi katika mapambano ya kupambana na ujangili jambo lililosaidia kwa kiasi kupunguza tatizo.

Hata hivyo, alisema ilipofikia mwaka 1989 shirika linaloshughulikia haki za wanyama walioko hatarini kutoweka (CITES) ilifanya maamuzi ya ku
piga marufuku biashara ya pembe za ndovu duniani.
Rais Kikwete alisema kwa mambo hayo mawili ikiwamo nguvu ya jeshi kuingilia kupambana na ujangili pamoja na biashara hiyo kupigwa marufuku duniani ilisaidia kupungua ujangili na tembo kuanza kuonekana.

Alisema ilipofika mwaka 2009 hesabu ilikuwa kubwa ambapo idadi ya tembo iliongezeka na kufikia 110,000.

Alipohojiwa juu ya gazeti moja la Uingereza la Daily Maili kumuandika kuwa hajafanya jitihada za kutosha kupambana na ujangili, alisema gazeti hilo limeandika uongo na kwamba serikali imejitahidi kufanya mikakati mbalimbali kuokoa maisha ya tembo na kupunguza ujangili.

Pembe hizo za ndovu wanaouliwa Afrika soko lake lipo katika nchi za Asia ikiwamo China.

Kikwete alisema jitihada mbalimbali zimefanywa ndiyo maana mtandao huo ambao unajihusisha na biashara ya meno ya tembo umegundulika.

Wakati Rais akiwa kwenye mkutano nchini Uingereza uliokuwa ukijadili ujangili na biashara haramu ya meno ya tembo na pembe za faru, polisi mkoani Singida wamemkamata George James na vipande 21 vya meno hayo.

Polisi ilisema meno hayo yenye thamani ya Sh. milio
ni 43 yana uzito wa kilo 49.

MAHOJIANO NA CNN
Wakati huo huo, ujangili umemfikisha Rais Kikwete, kwenye televisheni y
a CNN ya Marekani, alikohojiwa akitakiwa kueleza vita dhidi ya majangili inayofanyika nchini.
Akihojiwa na CNN jijini London juzi, alisema Tanzania imefanya operesheni nyingi dhidi ya majangili na kuhimiza haja ya mataifa makubwa kusaidia juhudi za kupambana na ujangili huo.
Akijibu maswali ya Christiane Amanpour wa CNN, Rais alitaka dunia kuungana kusimamisha biashara ya pembe za ndovu.

Alieleza kuwa hatua hiyo itaondoa kichocheo cha mtu kuwaua wanyama hao
Alieleza kuwa wakati wa uhuru walikuwepo tembo 350,000 kabla ya kuibuka wimbi la ujangili mkubwa ulioiachia nchi tembo 13,000 pekee.

AHADI YA MSAADA 
Akijibu swali kama kuna ahadi yoyote aliipata katika mkutano juu ya ulinzi wa wanyama pori uliofanyika London juzi, Rais Kikwete aliitaja Canada kuwa imeahidi kutoa Dola milioni mbili, wakati serikali ya Uingereza imeahidi kutoa msaada.

ALICHOTARAJIA
Alieleza kuwa kitu muhimu kwake na viongozi wa Afrika ni kufahamisha kuwa ili kuupiga vita ujangili kunahitajika rasilimali watu, kuwajengea uwezo askari wa wanyama pori wa kulinda wanyama.
Rais alisema alikuwa anategemea nchi zilizoendelea hasa Uingereza na Marekani kusaidia upande wa mafunzo ya askari wa wanyama pori na pia kuwapatia vifaa.

Alitaja silaha, magari na vyombo vyenye uwezo wa kufanya uchunguzi na kwamba ndicho alichotegemea kutoka kwenye mkutano huo na kwamba amepata ahadi za msaada.
AKIBA YA MENO
Rais Kikwete alisema Tanzania ina karibu tani 112 za pembe za ndovu ambazo haijajua itazifanya nini kwa sababu nchi ilizoea kuomba idhini ya kuziuza hatua ambayo inahitaji kuangaliwa upya.

UMASKINI
Akijibu swali kuhusu kukua kwa uchumi kwa kiasi kikubwa kulinganisha na nchi nyingine katika kipindi cha miaka michache iliyopita lakini nchi ikiwa na maskini wanaoishi kwenye ufukara, alisema “uchumi unakua kwa asilimia 70 lakini umasikini unapungua kwa asilimia 2.0” akiongeza kuwa mchango huo wa ukuaji wa asilimia 7.0 umetokana na sekta ya mawasiliano na usafiri.  
Chanzo: Nipashe

YANGA KUTUPA KARATA LEO VS KOMOROZINE.


YANGA SC Mabingwa wa Tanzania Bara, jioni ya leo wanashuka dimbani kucheza mechi yao ya mwisho ya Raundi ya Awali Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji Komorozine mjini Moroni.
Katika me

chi ya kwanza Yanga SC walishinda mabao 7-0 katika mchezo wa kwanza dhidi ya Wacomoro Dar es Salaam Jumapili na leo wanatakiwa kumalizia vyema kazi yao dhidi ya timu hiyo dhaifu.
Endapo Yanga SC itafanikiwa kukamilisha vyema matokeo ya Randi ya Awali, basi itakutana na mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misiri katika Raundi ya Kwanza. 

BALOTELI AIPA MILAN BAO LA DAKIKA ZA LALA SALAMA

Kunako dakika za  lala salama Mario Balotelli amefanikiwa kuipatia AC Milan ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Bologna katika mchezo wa Serie A usiku wa jana.
Balotelli alifunga bao lake  la 10 msimu huu kwa shuti la umbali wa mita 30 dakika nne kabla ya filimbi ya mwisho na kuipandisha Milan hadi nafasi ya 10 ikifikisha pointi 32 sawa na Lazio iliyo nafasi ya tisa.
SERIE A
RATIBA/MATOKEO:
Ijumaa Februari 14
AC Milan 1 Bologna 0
[Saa za Bongo]
Jumamosi Februari 15
2245 ACF Fiorentina v Inter Milan
Jumapili Februari 16
1430 Calcio Catania v SS Lazio
1700 Atalanta BC v Parma FC
1700 Juventus FC v AC Chievo Verona
1700 Cagliari Calcio v AS Livorno Calcio

1700 Genoa CFC v  Udinese Calcio
1700 US Sassuolo Calcio v SSC Napoli
2245 AS Roma v UC Sampdoria
Jumatatu Februari 17
2245 Hellas Verona FC v Torino FC
MSIMAMO-Timu za Juu:
NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 Juventus FC 23 19 3 1 56 18 38 60
2 AS Roma 22 15 6 1 45 11 34 51
3 SSC Napoli 23 14 5 4 47 27 20 47
4 ACF Fiorentina 23 13 5 5 42 24 18 44
5 Inter Milan 23 9 9 5 40 27 13 36
6 Hellas Verona 23 11 3 9 39 37 2 36
7 Torino FC 23 8 9 6 36 30 6 33
8 Parma FC 22 8 9 5 32 27 5 33
9 AC Milan 24 8 8 8 37 35 2 32

TWIGA STARS YA TANZANIA YALALA 2-1 ZAMBIA

Twiga Stars imepoteza mechi ya kwanza ya raundi ya kwanza kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) baada ya leo kufungwa mabao 2-1 na Zambia (Shepolopolo) kwenye Uwanja wa Nkoloma jijini Lusaka.

Hadi dakika 45 za kwanza zinamalizika katika mechi hiyo iliyochezeshwa na mwamuzi Salma Mukansanga timu hizo zilikuwa suluhu.

Wenyeji ndiyo walianza kupata bao lililofungwa na Hellen Mubanga dakika ya 75. Mfungaji huyo aliyeingia kipindi cha pili nchini alimalizia wavuni mpira uliotemwa na kipa Fatuma Omari.

Dakika nne baadaye Zambia ambao walikuwa wakishangiliwa kwa nguvu na washabiki wao baada ya kufunga la kwanza, walipata bao la pili ambalo nahodha wa Twiga Stars, Sophia Mwasikili alijifunga mwenyewe.

Mwasikili alikuwa akijaribu kutoa nje mpira uliopigwa na nahodha wa Shepolopolo, Mupopo Kabange ambapo ulipishana na kipa Fatuma Omari kabla ya kujaa wavuni.

Bao la Twiga Stars lilifungwa na Donisia Daniel dakika ya 90. Beki huyo wa kushoto ambaye pia ni mchezaji wa Tanzanite alipanda mbele kuongeza mashambulizi ambapo akiwa nje ya eneo la hatari alipiga shuti lililomshinda kipa Hazel Nali.

Akizungumza baada ya mechi, Kocha wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage alisema amebaini upungufu katika kikosi chake ambao ataufanyia kazi kabla ya mechi ya marudiano ili timu yake iweze kusonga mbele.

“Kwa matokeo haya bado tuna nafasi ya kufanya vizuri kwenye mechi ya marudiano nyumbani na kusonga mbele,” alisema Kaijage.

Twiga Stars iliwakilishwa na Fatuma Omari, Fatuma Bashiru, Donisia Daniel, Fatuma Issa, Evelyn Sekikubo, Sophia Mwasikili, Vumilia Maarifa, Mwapewa Mtumwa/Amina Ali, Asha Rashid, Etoe Mlenzi/Zena Khamis na Shelida Boniface.

Timu hiyo inarejea nyumbani kesho kwa ndege ya Fastjet ambapo itatua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 7 kamili mchana.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
+260 976375482
Lusaka, Zambia

Friday, February 14, 2014

VPL: KAZI IPO MBEYA CITY YAJIPANGA KUMUUWA MNYAMA SIMBA DIMBANI SOKOINE KESHO J"MOSI


RATIBA:
Jumamosi Februari 15

Rhino Rangers v Mgambo JKT

Ashanti United v Kagera Sugar

Mtibwa Sugar v Tanzania Prisons

JKT Oljoro v JKT Ruvu

Mbeya City v Simba

Ruvu Shooting v Coastal Union

­­
MSIMAMO:

NA TIMU P W D L GD PTS
1 Azam FC 16 10 6 0 19 36
2 Yanga SC 16 10 5 1 22 35
3 Mbeya City 17 9 7 1 10 34
4 Simba SC 17 8 7 2 17 31
5 Coastal Union 17 4 10 3 4 22
6 Ruvu Shooting 16 5 7 4 2 22
7 Mtibwa Sugar 17 5 7 5 0 22
8 Kagera Sugar 17 5 7 5 0 22
9 JKT Ruvu 16 6 0 10 -8 18
10 Ashanti UTD 16 3 4 9 -14 13
11 JKT Oljoro 17 2 7 8 -14 13
12 Mgambo 17 3 4 10 -18 13
13 Rhino Rangers 17 2 6 9 -10 12
14 Prisons FC 14 1 7 6 -10 10

RATIBA MECHI ZIJAZO:

Jumatano Februari 19

Tanzania Prisons v JKT Ruvu

Jumamosi Februari 22

Ruvu Shooting v Yanga

Kagera Sugar v Rhino Rangers

Mtibwa Sugar v Ashanti United

Coastal Union v Mbeya City

JKT Oljoro v Mgambo JKT

Azam FC v Tanzania Prisons

Jumapili Februari 23

Simba v JKT Ruvu

CHAMAZI NDIO HABARI YA MJINI-YANGA YAKUBALI KUWEKA KAMBI"

Dimba la Uwanja wa Azam Complex Chamazi
Yanga SC Kupitia Uongozi wake umetanabisha kuwa upo tayari kuweka kambi Chamazi kufuatia ofa waliyoitoa Azam ya kuwataka wakaweke kambi maeneo hayo kwa ajili ya kujiweka sawa na mchezo wa raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly ya Misri.
KAama unakumbuka wiki iliyopita uongozi wa Azam FC ulikataa ombi la Al Ahly kuweka kambi kwenye eneo lao hilo wakati watakapokuja nchini kucheza dhidi ya Yanga katika hatua hiyo baada ya kufanikiwa kuitoa Komorozine ya morroco.
Wachezaji Wa Yanga Wakiwa Katika Swimming Pool
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Abdallah Bin Kleb amesema hawawezi kuiachia ofa kama hiyo kwa kuwa mtazamo wao ni kuona wanafanikiwa kufanya vizuri katika mechi hiyo.
"Katika hali ya kawaida hakuna mtu anaeweza kukataa ofa kama hiyo, iwapo Azam wameamua kutusaidia sisi tupo tayari ila tunamsikiliza upande wa benchi la ufundi kupitia Kocha Mkuu mwalimu Hans Van Pluijm anahitaji kambi ya aina gani ili kuweza kujiandaa.
"Hata hivyo Bin Kleb amesema Kocha ndiye anayejua aina ya timu anayotarajia kukutana nayo, hivyo uongozi unamwachia kila kitu na yeye ndiye atakayetoa maamuzi.

TFF YAWATAKA WANACHAMA WAKE KUFAVYA MAREKEBISHO YA KATIBA KABLA YA MACHI 20

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeamuru wanachama wake wote kufanya marekebisho ya katiba zao kabla ya Machi 20, mwaka huu, hivyo kutengua tarehe ya mkutano mkuu wa Simba.

Simba iliyo chini ya mwenyekiti wake, Ismail Aden Rage, ilipanga kufanya mkutano wake huo Machi 23, mwaka huu kwa ajenda moja ya marekebisho ya katiba yao ambapo sasa imeamua kufanya mkutano huo mapema, Machi 16 ili kwenda sawa na maagizo ya TFF.
Ofisa Habari wa Simba, Asha Muhaji alisema kuwa walitumiwa barua ya maagizo hayo na TFF wiki hii na hivyo wameamua kuurudisha nyuma ili marekebisho hayo yafanyike kabla ya Machi 20.
“Mkutano wa marekebisho hautafanyika tena Machi 23 kama wanachama na wadau wote wa Simba walivyokuwa wakifahamu, tumepata barua kutoka TFF inayotuelekeza kufanya mkutano huo kabla ya Machi 20, hivyo sasa mkutano utakuwa Machi 16.