Saturday, November 8, 2014

YANGA YAKWEA MPAKA NAFASI YA PILI MBEYA CITY BADO HALI TETE YAPIGWA 1 NA STEND UNITED.


MATOKEO MECHI ZA VPL
Stand United 1 Mbeya City 0       
Yanga 2 Mgambo JKT 0             
Mtibwa Sugar v Kagera Sugar (Mvua yavunja yaleta balaa Mtibwa 1 Kagera 0)             
Azam FC 2 Coastal Union 1                 
Polisi Moro 1 Prisons 0
Katika Mtanange wa Vinara wa Ligi Kuu Vodacom, Mtibwa Sugar, na Kagera Sugar huko Morogoro umevunjika kutokana na mvua kunyesha ambapo Mtibwa wakiwa mbele kwa Bao 1-0 na katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam baada ya kupoteza dhidi ya kagera sugar Yanga leo imefanikiwa kuibuka na ushindi wa 2-0 zikiwekwa kimiani na Saimon Msuva kunako Dakika za 74 na 90 na kuipandisha Yanga hadi Nafasi ya Pili. .
na huko katika Viunga vya Azam Complex, Chamazi Mabingwa Azam FC walifunga mabao yao katika dakika za mwishoni na kushinda 2-1 wakiumana na Coastal Union.
Mabao Azam FC wamefunga Kipre Tchetche Dakika ya 88 kwa Azam FC na Rama kuisawazishia Coastal lakini Shomari Kapombe akaipa ushindi Azam FC kwa Bao la Dakika ya 90.
LIGI KUU VODACOM
RATIBA
Jumapili Novemba 9
Simba v Ruvu Shootings             
JKT Ruvu v Ndanda FC
Ijumaa Desemba 26
Simba v Kagera Sugar
Jumamosi Desemba 27
Mtibwa Sugar v Stand United               
Prisons v Coastal Union             
JKT Ruvu v Ruvu Shootings
Jumapili Desemba 28
Mbeya City v Ndanda FC            
Polisi Moro v Mgambo JKT          
Yanga v Azam FC             
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Mtibwa Sugar
6
4
2
0
9
2
7
14
4
Yanga
7
4
1
2
9
5
4
13
3
Azam FC
7
4
1
2
8
4
4
13
2
Coastal Union
7
3
2
2
8
6
2
11
5
Kagera Sugar
6
2
3
1
4
2
1
9
12
Polisi Moro
7
3
2
2
6
7
-1
9
6
Mgambo JKT
7
3
0
4
4
7
-3
9
13
Stand United
7
2
3
2
5
9
-4
9
7
JKT Ruvu
6
2
1
3
5
7
-2
7
8
Ruvu Shooting
6
2
1
3
4
6
-2
7
9
Simba
6
0
6
0
6
6
0
6
10
Tanzania Prisons
7
1
3
3
5
6
-1
6
11
Ndanda FC
6
2
0
4
8
10
-2
6
14
Mbeya City
7
1
2
4
3
5
-2
5

Friday, November 7, 2014

UUZAJI MCHANGANYIKO WA TIKETI MWISHO WIKIENDI HII

Uuzaji mchanganyiko wa tiketi za elektroniki kwenye Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) utakoma baada ya mechi mbili za wikiendi hii kati ya Yanga na Mgambo Shooting na Simba na Ruvu Shooting zitakazochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ligi itasimama kupisha mechi ya Kalenda ya FIFA, mashindano ya Chalenji na dirisha dogo la usajili. Baada ya hapo tiketi zote zitauzwa kwa njia ya mtandao, hivyo hakutakuwepo na vibanda vya kuuza tiketi viwanjani.

MSHAMBULIAJI WA YANGA MRISHO NGASSA RASMI AINGIA KATIKA REKODI AFRIKA.

Mshambuliaji wa Klabu ya Yanga, Mrisho Ngassa, ameingia kwenye Rekodi rasmi za Afrika baada ya kuibuka kuwa Mfungaji Bora wa CAF Championz ligi Msimu wa 2014 akiwa na Bao 6 akifungana na Wachezaji wengine Watatu.
Wengine waliofunga Bao 6 kwenye Mashindano hayo ambayo ES Setif ya Algeria iliibuka kuwa Mabingwa ni El Hedi Belameiri wa Setif, Firmin Ndombe Mubele wa AS Vita ya Congo DR na Haythem Jouini wa Esperance ya Tunisia.
Hii ni mara ya kwanza kwa Mtanzania kuingia kwenye Chati aina hii kwenye Mashindano ya Barani Afrika.
CAF CHAMPIONZ LIGI 2014  
WAFUNGAJI BORA:
Wote Bao 6
@Mrisho Ngasa (Yanga, Tanzania)
@Haythem Jouini (Espérance Tunis)                  
@Firmin Ndombe Mubele (AS Vita, Congo DR)                      
@El Hedi Belameiri (ES Setif, Algeria)                        
Ngassa alifunga Bao zake zote 6 dhidi ya Komorozine ya Visiwa vya Comoro waliyokutana nayo Raundi ya Awali ya CAF CHAMPIONZ LIGI mapema Mwaka huu.
Kwenye Mechi ya kwanza Jijini Dar es Salaam Ngassa alipiga Bao 3 Yanga waliposhinda 7-0 na marudiano huko Comoro, Ngassa tena alipiga Hetitriki Yanga ikishinda 5-1.
Raundi iliyofuata Yanga walikutana na waliokuwa Mabingwa wa Afrika, Al Ahly ya Misri na kubwagwa nje. 
Ngassa, mwenye Miaka 25, Mwaka 2009 aliwahi kwenda kufanya majaribio huko England na Klabu ya West Ham na vile vile huko Marekani na Klabu ya Seattle Sounders Mwaka 2011 na kucheza Mechi dhidi ya Manchester United waliyofungwa 7-0.

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU MAHAKAMA ZA MWANZO KUAMUA MASHAURI YA KESI ZA ARDHI.

SERIKALI, imezipiga marufuku Mahakama za Mwanzo kuamua mashauri ya kesi za Ardhi kwani jukumu hilo ni la Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya.
Onyo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angellah Kairuki, wakati alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Nkenge, Assumpter Mshama (CCM), lililoulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa Mwibara, Alphaxard Lugola (CCM).
Mbunge huyo ametaka kujua kwanini serikali isitoe kauli na tamko la kuwataka Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo kutopokea kesi hizo na badala yake izipeleke kwenye mabaraza ya ardhi.
Amesema, kukomesha tabia ya mahakama za Mwanzo kuhukumu kesi la Ardhi serikali itawasiliana na Makama za mwanzo ili ziweze kuchukua hatua stahiki katika jambo hilo.
Kuhusu, ucheleweshwaji wa kesi taratibu  zinafahamika kwa wale ambao watakuwa na sababu za msingi lakini mahakama zimekuwa haziahirishi kesi bila sababu yoyote endapo itakuwa kusababu zimeeleweka kamati za mahakimu na za majaji wataweza kufuatilia na kuchukua hatua.