Friday, May 3, 2013

BENITEZ AWATAKA MASHABIKI WA CHELSEA KUMUHESHIMU


Rafael Benitez kocha wa muda wa chelsea amesema anastahili kuheshima kwa kuipeleka Chelsea kutinga Fainali ya EUROPA LIGI ambapo watakutana na Benfica huko Amsterdam ArenA hapo Mei 15.








Wakiwa katika dimba la uwanja wa Stamford Bridge katika Mechi ya Marudiano ya
Nusu Fainali ya EUROPA LIGI na FC Basel huku wakiwa wameshinda Bao 2-1
toka Mechi ya kwanza, Chelsea walitanguliwa Bao 1-0 hadi Mapumziko
 lakini Kipindi cha Pili waliisambaratisha Basel kwa kuitandika Bao 3 ndani ya
Dakika 9 kwa Bao za Torres, Moses na Luiz.
MAGOLI:
Chelsea 3
*Torres Dakika ya 50
*Moses 52
*Luiz 59
FC Basel 1
*Salah Dakika ya 45
Hii ni Fainali ya 10 kwenye himaya ya Mmiliki Roman Abramovic huku
 Chelsea wakitwaa  Mataji 11 na watakuwa wakiwania Rekodi ya kuwa
 Klabu ya 4 Barani Ulaya kuweza kutwaa Mataji yote makubwa ya Ulaya
yakiwemo UEFA CUP WINNERS CUP [Kombe la Washindi] na
UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Chelsea, ambao walitwaa Kombe ambalo sasa halipo, Kombe la Washindi,
mara mbili Miaka ya 1970/71 na 1997/98, pamoja na la Klabu Bingwa Ulaya Mwaka jana
, hawajawahi kutwaa UEFA CUP, ambalo sasa ndio EUROPA LIGI.
Klabu nyingine 3 ambazo zimefuzu kutwaa Mataji yote hayo makubwa ni Juventus, Ajax
 na Bayern Munich.
MAKOMBE ENZI ZA ABRAMOVICH:
*BPL 3
*FA CUP 3
*KOMBE LA LIGI 2
*UEFA CHAMPIONZ LIGI 1
*NGAO YA HISANI 2