Meneja wa Chelsea, Jose Mourinho amesema lengo kuu anataka kurudisha upya familia ya
wadau wa Chelsea ambayo ilivunjika baada ya kocha aliyeondoka Rafa Benitez
kumrithi kocha kipenzi cha mashabiki Roberto Di Matteo na kusababisha
tofauti kwa mashabiki wa klabu hiyo.
Chelsea
waliingia katika vita ya wenyewe kwa wenyewe baada ya kumfukuza kocha
aliyewapa ubingwa wa ligi ya mabingwa barani Ulaya, na hata baada ya
Benitez kushinda kombe la Uropa haikumnusuru kufungashiwa virago.
Ambapo mmiliki Roman Abramovich alimgeukia tena kwa mara ya pili Mourinho majira haya ya kiangazi na amefanikiwa kumrejesha.
Kocha
huyo mwenye Umri wa miaka 50, raia wa Ureno aliliambia gazeti la The
Sun: “Nawataka kuwa nasi kama familia ya Chelsea-familia ambayo kwa muda
fulani mwaka jana ilionekana kuvunjika”.

