KOCHA mkuu
wa Young Africans, Mholanzi, Hans Van der Pluijm amepata kazi mpya
nchini Saudi Arabia na tayari ameshaaga rasmi mchana huu kwa wachezaji
wake, viongozi, wapenzi na wanachama wa klabu hiyo.
Pluijm
aliyejiunga na Yanga mapema januari mwaka huu umepata shavu hilo katika
klabu ya Al Shoalah FC inayoshiriki ligi kuu soka nchini Saudi Arabia.
Yanga
chini ya Pluijm ilimaliza katika nafasi ya pili, huku Azam fc chini ya
kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog wakibeba taji lao la kwanza tangu
wapande ligi kuu msimu wa 2008/2009.
Pluijm
alirithi mikoba ya mholanzi mwenzake, Ernie Brandts aliyetimuliwa mwezi
desemba mwaka jana baada ya kufungwa mabao 3-1 na Simba katika mechi ya
Nani Mtani Jembe.