KAMATI ya Rufani ya Uchaguzi ya
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) inakaa Jumatatu (Juni 9 mwaka huu) kusikiliza
rufani moja inayopinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi
ya Simba.
Michael Wambura amewasilisha rufani yake TFF akipinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya Simba iliyomwengua katika kinyang’anyiro cha kuwania urais katika uchaguzi wa klabu hiyo unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.
Kamati
hiyo inayoongozwa na Wakili Julius Lugaziya itakutana saa 5 asubuhi kwenye
hoteli ya Courtyard iliyopo Upanga, jijini Dar es Salaam.