Maafande wa Ruvu shootingi wa kibaha Mkoani Pwani imefanikiwa kumnasa aliyekuwa Mshambuliaji wa zamani wa
Simba, Betram Mwombeki na kumpatia kitanzi cha mkataba wa mwaka mmoja.
Straika huyo msimu uliopita alikuwa akiitumikia Simba
akitokea Pamba na aliweza kufanya vyema katika mzunguko wa kwanza lakini wa
pili hakuweza kupata nafasi ya uhakika, hivyo akaumaliza msimu akiwa na mabao
manne tu.
Akizumgumza na mkali wa dimba Msemaji wa Ruvu Shooting,
Masau Bwire amethibitisha hilo huku akidai kuwa wakati ukifika ataweka hadharani huku akihitaji siku muda ili kulitanabaisha hadharani.
Baada ya kuondoka Simba, Mwombeki
alikwenda Oman na kufanya majaribio katika kikosi cha Oman Club FC
linachoshiriki daraja la kwanza. Lakini mambo yalikwenda kombo.