Uongozi wa Klabu ya Mtibwa Sugar umeweka wazi kwamba upo
katika hatua za mwisho za kumalizana na Simba kwa ajili wa beki wao namba mbili Hassani Ramadhani Kessy licha ya kuripotiwa kuwepo na ugumu wa mchakato huo wa usajili.
Hata hivyo kumekuwa na taarifa kwamba
mazungumzo yako katika hatua nzuri sana na pande zote mbili, yaani Simba
na Mtibwa Sugar zimekubali kwamba zimefanya mazungumzo.
Afisa Habari wa Mtibwa Sugar Tobias Kifaru ameweka wazi kuwa Simba wameonyesha nia ya kumtaka mchezajihuyo ambapo mazungumzo
yanaendelea vizuri na kila kitu kinakwenda vizuri katika uwezekano wa
kumsajili kukamilika ndani ya siku chache zijazo.