Baada ya Mvutano wa hapa na
pale nani aachwe kati ya Emerson kiiza na Coutinho Yanga sasa imeamua kuwaacha kuwatupia virago Mbrazil, Emerson de Oliviera Roque na Mganda Hamis Kiiza na kumsajili mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Mrundi Amisi
Tambwe.
Tambwe amesaini Mkataba wa
mwaka mmoja baada ya kuachwa na klabu yake, Simba SC aliyoichezea msimu mmoja
uliopita akitokea Vital’O ya Burundi.
Yanga SC imeamua kumuacha
Mbrazil Emerson baada ya kushindwa kupata Hati yake ya Uhamisho wa Kimataifa
(ITC).
Tambwe anaungana na
Mliberia, Kpah Sherman, Wanyarwanda Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Mbrazil
Andrey Coutinho kukamilisha idadi ya wachezaji watano wa kigeni Yanga SC.
Yanga SC imesajili jumla ya wachezaji watatu
wapya baada ya kumuacha Emerson, mwingine ni Danny Mrwanda.
Katika kipindi cha msimu
mmoja, Tambwe ameichezea Simba SC jumla ya mechi 43 na kuifungia mabao 26.
Maisha yake yalianza kuwa
magumu Simba SC baada ya ujio wa kocha Mzambia, Patrick Phiri kuchukua mikoba
ya Mcroatia, Zdravko Logarusic.

