KOCHA RHINO APIGWA FAINI, AFUNGIWA MECHI SITA
KAMATI
ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imempiga faini
ya sh. 400,000 na kumfungia mechi sita Kocha wa Rhino Rangers, Renatus
Shija kwa kushiriki vitendo vinavyoashiria imani za ushirikina na
kumdhihaki mwamuzi kwenye mechi za Ligi Daraja la Kwanza (FDL).
Adhabu
hizo zimetolewa kwa mujibu wa kifungu cha 31(1)(a) na (b) cha Kanuni za
FDL ambapo Kocha huyo aliyeipandisha daraja Rhino Rangers kucheza Ligi
Kuu ya Vodacom (VPL) alifanya vitendo hivyo kwenye mechi mbili tofauti.
Mechi
hizo ni kati ya Kanembwa JKT na Rhino Rangers iliyochezwa Februari 23
mwaka huu Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma, na ile kati ya Rhino
Rangers na Morani iliyochezwa Machi 17 mwaka huu Uwanja wa Ali Hassan
Mwinyi mjini Tabora.
Pia
klabu ya Rhino Rangers imepigwa faini ya sh. 200,000 kutokana na Polisi
Wanajeshi- MP kuwapiga walinzi milangoni kwenye mechi hiyo dhidi ya
Kanembwa JKT ili kupisha washabiki wa timu hiyo waingie bure uwanjani.
Mchezaji
wa timu ya Pamba ya Mwanza, Leonard Nahole amepigwa faini ya sh.
200,000 na kufungiwa mechi nne baada ya kumrushia chupa ya maji mwamuzi
kwa madai amependelea kwenye mechi dhidi ya Polisi Tabora iliyochezwa
Machi 16 mwaka huu.
Nao
wachezaji Joseph Mapalala, Yohana Mirobo, Noel Makunja, Mkome Pastory
na Rudenzi Kilinga wa Polisi Mara wamepigwa faini ya sh. 200,000 kila
mmoja na kufungiwa mechi tatu kwa kufanya vitendo vinavyoshiria
ushirikina na kumkimbiza mwamuzi kwenye mechi dhidi ya Morani
iliyochezwa Machi 9 mwaka huu. Adhabu za wachezaji hao ni kwa mujibu wa
kifungu cha 27(1)(g) cha Kanuni za FDL.
Klabu
ya Villa Squad imepigwa faini ya sh. 150,000 kwa kuchelewa uwanjani
kwenye mechi yake dhidi ya Ashanti United wakati Majimaji imepigwa faini
ya sh. 200,000 kutokana na washabiki wake kufanya vurugu kwenye mechi
dhidi ya Mbeya City iliyochezwa Uwanja wa Majimaji.
Vilevile
Msimamizi wa Uwanja wa Majimaji aliyetambulika kwa jina moja la Mapunda
aliwatukana waamuzi kwenye mechi hiyo, na suala lake litafikishwa
kwenye Kamati ya Nidhamu ya TFF kwa ajili ya hatua za kinidhamu.
Pia
uongozi wa Uwanja wa Mafinga unaotumiwa na timu ya daraja la kwanza ya
Kurugenzi umetakiwa kuufanyia marekebisho, vinginevyo hautatumika kwa
mechi za FDL msimu ujao.
MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kesho (Aprili 11 mwaka huu) litakuwa
na Mkutano na Waandishi wa Habari. Mkutano huo utafanyika saa 5 asubuhi
kwenye ofisi za TFF.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
UEFA KUANZISHA ADHABU MPYA
Ofisa Habari
UEFA KUANZISHA ADHABU MPYA
SHIRIKISHO la Soka barani Ulaya-UEFA limepanga kuanzisha adhabu mpya kali ya kupambana na ubaguzi wa rangi ambap wachezaji watakaokutwa na hatia ya kufanya vitendo hivyo watafungiwa si chini mechi 10. Katika Mkuu wa UEFA Gianni Infantino amesema pia watafunga viwanja kwa muda viwanja ambavyo mashabiki wake watafanya tukio kama hilo kwa mara ya kwanza na kuufunga kabisa kama mashabiki wa timu husika watarudia tukio hilo kwa mara ya pili pamoja na faini ya fedha nyingi. Adhabu hizo mpya ambazo zilizungumziwa katika kikao cha kamati ya utendaji ya UEFA kilichokutana jana kitahusisha mechi zote za mashindano barani Ulaya. Infantino alifafanua kuwa kama mashabiki wa klabu fulani watakutwa na hatia ya kufanya vitendo hivyo basi upande wa uwanja uliohusika na tukio hilo utafungwa lakini kama tatizo ilikijirudia basi mashabiki wote watazuiwa kuingia uwanjani na kutozwa faini itakayofikia dola 65,300.
MCHEZA gofu namba moja duniani, Tiger Woods amesema yuko katika kiwango kizuri tayari kukata ukame wa miaka mitano kupita bila kushinda taji kubwa la Masters wiki hii. Woods ndio anapewa nafasi kubwa ya kunyakuwa zawadi ya Koti ya Bluu toka alipofanya hivyo mwaka 2005 na taji la kwanza kubwa toka mwaka 2008 baada ya kurejea kileleni mwa orodha ya wachezaji bora wa mchezo huo kwa kushinda mataji matatu mwaka huu. Nyota huyo alianguka mpaka katika nafasi ya 58 mwaka 2011 kufuatia kukumbwa na kashfa katika maisha yake binafsi na pia kusumbuliwa na majeruhi. Akihojiwa Woods mwenye umri wa miaka 37 amesema kwasasa anajisikia kurejesha makali yake ya zamani hivyo anategemea kufanya vizuri zaidi mwaka huu.