CLUB ya Real Madrid, ikiwa katika dimba la Uwanjan wa nyumbani wa
Santiago Bernabeu Jijini Madrid Nchini Spain, jana usiku wamefanikiwa kuifumua
Borussia Dortmund Bao 3-0 katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA
CHAMPIONZ LIGI.
Mchezaji Gareth Bale ndie aliefunga Bao la Kwanza
katika Dakika ya 3 tu baada kuunganisha pasi safi ya Daniel Carvajal na
kumzidi akili Kipa Roman Weidenfeller
Hilo ni Bao la 14 kwa Ronaldo kwenye
UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu huu na ameifikia Rekodi ya Ronaldo ya Lionel
Messi aliefunga Bao 14 katika Mechi 11 za UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu wa
2011/12 wakati Ronaldo amechukua Mechi 8 tu.
Mchezaji Ezequiel Lavezzi alitangulia kuwapa PSG
Bao la kuongoza katika Dakika ya 4 baada kuweka gambani Mpira
uliookolewa kwa Kichwa na John Terry na kufumua Shuti moja kwa moja na
kumpita Kipa Petr Cech.
Bao la Pili la Real lilifungwa katika Dakika ya 27 kupitia Isco kwa Shuti la chini toka Mita 20.
Hadi Mapumziko Bao zilikuwa Real 2 Dortmund 0.
Kunako Dakika ya 57, Mchezaji Bora
Duniani, Cristiano Ronaldo, alipiga Bao la 3 baada kumtoka Kipa Roman
Weidenfeller kufuatia kupokea pasi safi ya Luka Modric.
Ronaldo hakumaliza Mechi hii baada ya kuumia na kutolewa nje katika Dakika ya 80.
Timu hizi zitarudiana huko Signal Iduna Park, Jijini Dortmund, Germany Jumanne Aprili 8.
VIKOSI:
REAL MADRID: Casillas, Carvajal, Pepe, Sergio Ramos, Fabio Coentrao, Modric, Alonso, Isco, Bale, Benzema, Ronaldo
Akiba: Diego Lopez, Varane, Casemiro, Nacho, Morata, Illarramendi, Jose Rodriguez.
BORUSSIA DORTMUND: Weidenfeller, Piszczek, Hummels, Papastathopoulos, Durm, Kehl, Sahin, Grosskreutz, Mkhitaryan, Reus, Aubameyang
Akiba: Langerak, Friedrich, Hofmann, Jojic, Kirch, Schieber, Duksch.
REFA: MARK CLATTENBURG (ENGLAND)
Katika mtanange mwingine Paris Saint-Germain, wakiikaribisha chelsea katika nyasi za Uwanja wa nyumbaniwa Parc des Princes huko Paris, France, jana Usiku wameisasambua Chelsea ya England
Bao 3-1 katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Chelsea walisawazisha kwa Penati ya
Dakika ya 27 iliyopigwa na Eden Hazard na ilitolewa na Refa Milorad
Mazic kutoka Serbia alipoamua Sentahafu wa PSG Thiago Silva
‘kamwangusha’ Oscar.
Hadi Mapumziko Bao zilikuwa 1-1.
PSG walifunga Bao lao la 2 baada ya
Ezequiel Lavezzi kupiga Frikiki safi ambayo Kipa Petr Cech alishindwa
kuzuia na kumparaza Zlatan Ibrahimovic kisha Mchezaji wa Chelsea David
Luiz kuusindikiza wavuni.
Nchezaji alietoka Benchi, Javier
Pastore, aliipa PSG Bao la 3 katika Dakika ya 90 baada ya kupokea Mpira
wa kurushwa na kuwatoka Cesar Azpilicueta, Frank Lampard na John Terry
kisha kupiga Shuti la chini chini na kumshinda Kipa Petr Cech.
Timu hizi zitarudiana huko Stamford Bridge Jumanne Aprili 8.
VIKOSI:
PSG: Sirigu, Jallet, Alex, Thiago Silva, Maxwell, Verratti, Thiago Motta, Matuidi, Cavani, Ibrahimovic, Lavezzi.
Akiba: Douchez, Cabaye, Marquinhos, Digne, Rabiot, Pastore, Lucas Moura.
CHELSEA: Cech, Ivanovic, Cahill, Terry, Azpilicueta, Ramires, Luiz, Willian, Oscar, Hazard, Schurrle.
Akiba: Schwarzer, Lampard, Torres, Mikel, Ba, Ake, Kalas.
REFA: MILORAD MAZIC (SERBIA)
UEFA CHAMPIONZ LIGI
ROBO FAINALI
Marudiano
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
Jumanne Aprili 8
Chelsea v Paris Saint-Germain [1-3]
Borussia Dortmund v Real Madrid [0-3]
Bayern Munich v Manchester United [1-1]
Atletico Madrid v Barcelona [1-1]
-DROO YA NUSU FAINALI: 11 Aprili
-Mechi kuchezwa 22 & 23 Aprili na Marudiano 29 & 30 Aprili
-FAINALI: Estádio da Luz, Lisbon, Portugal 24 Mei 2014.
WASHINDI [Miaka ya karibu]:
MSIMU | MSHINDI | NCHI | MSHINDI WA PILI | NCHI | GOLI |
2012-13 | Bayern Munich | Germany | Borussia Dortmund | Germany | 2-1 |
2011-12 | Chelsea | England | Bayern Munich | Germany | 1-1 (4–3) |
2010-11 | Barcelona | Spain | Manchester United | England | 3-1 |
2009-10 | Internazionale | Italy | Bayern Munich | Germany | 2-0 |
2008-09 | Barcelona | Spain | Manchester United | England | 2-0 |
2007-08 | Man United | England | Chelsea | England | 1-1 (6–5) |
UEFA CHAMPIONZ LIGI
WAFUNGAJI BORA 2013/14:
C. Ronaldo-Real Madrid Goli 14
Zlatan Ibrahimovic-PSG Goli 10 [Penati 1]
Messi-Barcelona Goli 8 [Penati 2]
Diego Costa-Atletico Madrid Goli 7
Sergio Agüero-Manchester City Goli 6 [Penati 2]