BARAZA la vyama vya mpira wa miguu
Afrika Mashariki na kati, CECAFA limeiengua rasmi klabu Yanga kushiri
kombe la Kagame 2014 na nafasi yake imechukuliwa na mabingwa wa ligi kuu
soka Tanzania bara, Azam fc.
Tangu awali, CECAFA walitoa
taarifa kuwa Azam watapewa nafasi ya upendeleo katika michuano hiyo
inayoanza kushika kasi Agosti 8 mwaka huu, mjini Kigali nchini Rwanda, lakini mpaka jana wana Lambalamba walikuwa hawana taarifa rasmi.
Yanga sc ndio walitakiwa kushiriki
michuano hiyo, lakini waliamua kupeleka kikosi B ambapo CECAFA
ilikikataa na kuitaka timu hiyo ya makutano ya Twiga na Jangwani,
Kariokoo jijini Dar es salaam ipeleke kikosi cha kwanza pamoja na kocha
mkuu, Mbrazil Marcio Maximo.
Lakini Baada ya Yanga sc kuenguliwa
kushiriki michuano ya klabu bingwa kwa ukanda wa Afrika mashariki na
kati , maarufu kama Kombe la Kagame, kwa kugoma kupelekea kikosi cha
kwanza kama walivyoagizwa, Shirikisho la soka Tanzania TFF, limesema
klabu hiyo ina haki kutoshiriki mashindano kama inaona haijajiandaa.
Boniface Wambura Afisa habari na mawasiliano wa TFF, Mgoyo huu mchana
huu ameumbia mtandao wa mkali dimba tz kuwa klabu inapokuwa bingwa, hakuna kanuni inayoibana
kwamba lazima ishiriki mashindo fulani, bali kama wanaona hawapo tayari
wanaweza kuwasiliana na TFF, halafu klabu nyingine inatafutwa.