Friday, December 5, 2014

MICHUANO YA WANAWAKE TAIFA CUP KUANZA DESEMBA 28.

Michuano ya Taifa ya mpira wa miguu kwa wanawake ya Proin Women Taifa Cup inaanza rasmi Desemba 28 mwaka huu kwa mechi ya ufunguzi kati ya timu za mikoa ya Mara na Mwanza itakayochezwa Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Kombaini za mpira wa miguu za mikoa yote ya Tanzania Bara zitashiriki mashindano hayo yatakayochezwa kwa raundi mbili mwanzoni, na baadaye hatua ya robo fainali hadi fainali.
Mashindano hayo yanayodhaminiwa na kampuni ya Proin Promotions Limited, kuanzia hatua ya robo fainali, mechi zote zitafanyika jijini Dar es Salaam.
Meneja Biashara wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Peter Simon Shankunkuli aliishukuru kampuni ya Proin ambao ni watengenezaji, wazalishaji na wasambazaji wa filamu za kitanzania kwa kuwezesha mashindano hayo kufanyika kwa mara ya kwanza.
Proin Promotions imekua ikivumbua vipaji mbalimbali vya uigizaji na sasa imeamua kujikita katika mpira wa miguu ili kuweza kuvumbua vipaji kwa wachezaji wa kike.
Shankunkuli alisema nafasi bado zipo kwa wadhamini watakaoguswa na mashindano hayo, kwa kuwasiliana na TFF au Proin Promotions Limited kwa maelezo zaidi.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

MTIBWA SUGAR YASEMA MAZUNGUMZO NA HASANI KESSI YANAKWENDA VIZURI.

Uongozi wa Klabu ya Mtibwa Sugar umeweka wazi kwamba upo katika hatua za mwisho za kumalizana na Simba kwa ajili wa beki  wao namba mbili Hassani Ramadhani Kessy licha ya kuripotiwa kuwepo  na ugumu wa mchakato huo wa usajili.
Hata hivyo kumekuwa na taarifa kwamba mazungumzo yako katika hatua nzuri sana na pande zote mbili, yaani Simba na Mtibwa Sugar zimekubali kwamba zimefanya mazungumzo.
Afisa Habari wa Mtibwa Sugar Tobias Kifaru ameweka wazi kuwa Simba wameonyesha nia ya kumtaka mchezajihuyo ambapo mazungumzo yanaendelea vizuri na kila kitu kinakwenda vizuri katika uwezekano wa kumsajili kukamilika ndani ya siku chache zijazo.

TFF YASEMA WACHEZAJI WATAKAO CHEZA NANI MTANI JEMBE LAZIMA WAWE WAMESAJILI RASMI

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limetangaza wachezaji watakaotumika katika mechi ya Bonanza ya Nani Mtani Jembe kati ya Simba dhidi ya Yanga lazima wawe wale waliosajiliwa kwa mujibu wa kanuni.
Yanga au Simba hazitaruhusiwa kumtumia mchezaji yoyote ambaye hayuko kwenye usajili wakati wa mechi hiyo ya Oktoba 13 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Maana yake, Simba haitaweza kumtumia kiungo wake Mgambia, Omar Mboob hadi hapo itakapomsajili.
Kama itamsajili, itawakosa mmoja kati ya Amissi Tambwe au Pierre Kwizera ambao italazimika kuwatema.
Hadi sasa inaonekana Simba bado inamjaribu, hivyo haitakuwa rahisi kupata uhakika wa kumsajili hadi Desemba.
Hata hivyo, Mboob atapata nafasi nyingine ya kuonyesha uwezo wake, kesho kwenye Uwanja wa Taifa wakati Simba itakapoivaa Express ya Uganda.

MLINZI WA ZAMANI WA SIMBA NA COAST UNION JUM NYOSSO AJIUNGA MBEYA CIT MKATABA WA MWAKA MMOJA

Mlinzi wa kati Juma Nyosso amejiunga na kikosi cha Mbeya City Fc kwa mkataba wa mwaka mmoja.


Akizungumza mara baada ya kuisaini mkataba  huo kwenye  ofisi za timu zilizopo jengo la Mkapa Hall jijini Mbeya,  Nyoso aliyewahi kucheza kwenye timu za Ashanti United, Simba na Coastal Union, alisema  amekubari kujiunga na City kwa mkataba wa mwaka mmoja kwa imani kuwa utatosha  kuushawishi uongozi wa timu kumpa mkataba mrefu zaidi mara baada ya huu wa sasa.
“City ni timu nzuri na imekuwa hivyo toka ilipoanzishwa miaka minne iliyopita, matokeo yaliyoo sasa ni sehemu ya soka ambayo timu yoyote inaweza kuyapata, nimekubari kujiunga na timu kwa  mkataba wa mwaka mmoja kwa sababu naamini uwezo wangu  uwanjani utawashawishi viongozi kunipa mkataba mrefu zaidi  pindi huu utakapo malizika na nina amini  hili linawezekana kwa sababu nataka kukaa kwenye timu hii mpaka mpira wangu utakapoisha” alisema Nyosso
Akiendelea zaidi beki huyo aliyewahi pia kucheza  kwenye kikosi cha timu ya Taifa  ‘Taifa Stars’ alisema kuwa  mafanikio iliyopata Mbeya City msimu uliopita yamekuwa sababu kubwa ya yeye kukubari kujiunga na City huku akiamini kuwa amekuja kuongeza nguvu kwenye timu bora ili kuhakikisha mafanikio ya msimu uliopita yanafanikiwa tena.
DSC_0027
K wa upande wake Katibu Mkuu wa City Emmanuel Kimbe alimshukuru Nyosso kwa kukubari kujiunga na timu hii huku akiamini kuwa uzoefu alionao mchezaji huyo utasaidia kuimarisha safu ya ulinzi kwenye kikosi cha City.
“Tunamshukuru kukubari kujiunga nasi, imani yetu kubwa kwamba uzoefu alionao utasaidia kuimarisha safu yetu ya ulinzi, hasa ukizingatia matokeo tuliyopata katika michezo saba ya mwanzo wa Ligi hii” alisema Kimbe huku   kauli yake hiyo ikiungwa mkono na Kocha Mkuu Juma Mwambusi.
Kwa sasa Nyosso tayari yuko na kikosi cha City kilichosafiri kwenda mjini Songea  kwa ajiri ya michezo ya kirafiki.

TAZAMA MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA KWA MECHI SABA.


MSIMAMO LIGI KUU TZ BARA

Standings

PWDLFAGDPts
1mtibwa_sugarMtibwa Sugar FC7430103715
2Azam_FC_Club_LogoAzam FC741284413
3young_africansYoung Africans SC741296313
4COASTAL UNIONCoastal Union732397211
5KAGERA_SUGAR_FCKagera Sugar FC724164210
6JKT RUVU STARSJKT Ruvu Stars731367-110
7simbaSimba SC71607619
8polisi_morogoroPolisi Morogoro723267-19
9jkt_mgamboMgambo Shooting730357-29
10tffStand United FC723259-49
11JKT RUVU STARSRuvu Shooting FC721447-37
12Tanzania Prisons logoTanzania Prisons713367-16
13ndanda_fcNdanda FC7205812-46
14Mbeya FC LogoMbeya City FC712426-45