Saturday, April 13, 2013

YANGA YAINYUKA OLJORO 3- MTUNGI HATIMAYE YAIVUA UBINGWA SIMBA""
KATIKA  dimba la Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga wameitandika JKT Oljoro kwa Bao 3-0 na kuzidi kukwea kileleni mwa VPL, Ligi Kuu Vodacom, wakiwa Pointi 6 mbele ya Timu ya Pili Azam FC.

Ushindi wa leo pia umeivua rasmi Simba Ubingwa kwa vile wana Pointi 35 na wamebakiza Mechi 5 na hata wakishinda zote watafikisha Pointi 50 ambazo Yanga wameshazipita.
WAFUNGAJI
MAGOLI:
-Dakika ya 5 Nadir Haroub ‘Cannavaro’
-Dakika ya 19 Simon Msuva
-Dakika ya 43 Hamis Kiiza
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
VPL itaendelea kesho Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kwa bigi mechi kati ya Simba na Azam FC na kipigo kwa Azam FC kitaipa nafasi Yanga kutwaa Ubingwa.
MATOKEO VPL LEO


Yanga 3-0 Jkt oljoro
T/prison 2-0 Ruvu shooting


MSIMAMO:
NA
TIMU
p
W
D
L
GD
PTS
1
YANGA
21
15
4
2
28
52
2
Azam FC
23
14
4
4
22
47
3
Kagera Sugar
22
10
7
5
7
37
4
Simba
22
9
8
4
12
36
5
Mtibwa Sugar
23
8
9
6
2
33
6
Coastal Union
22
8
8
6
3
32
7
Ruvu Shooting
21
8
6
7
2
30
8
JKT Oljoro
22
7
7
8
-1
28
9
T/prison
21
4
10
9
-11
26
10
Jkt mgambo
21
7
3
9
-6
24
11
Toto African
24
4
10
1O
-11
22
12
JKT Ruvu
22
6
4
12
-16
22
13
African lyon
23
5
4
14
-19
21
14
Polisi  moro
23
3
10
10
-10
19
MATATIZO YA KIUFUNDI YAKWAMISHA SUPER WEEK ‘LIVE’
Mechi tano kati ya sita za Super Week za Ligi Kuu ya Vodacom zilizokuwa zioneshwe moja kwa moja (live) na Kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini sasa hazitaoneshwa kutokana na matatizo ya kiufundi.
TFF_LOGO12Kwa mujibu wa Mtayarishaji Mtendaji (Executive Producer) wa SuperSport Kanda ya Afrika, Max Tshunungwa ambaye yuko nchini, wameshindwa kuonesha mechi hizo kutokana na matatizo ya kiufundi katika magari yao ya kurushia matangazo (OB van) yanayohudumia Afrika Mashariki- Kenya, Tanzania na Uganda.
Mechi hizo ni kati ya Azam na African Lyon, Yanga na Oljoro JKT, Azam na Simba, Coastal Union na JKT Ruvu na Mgambo Shooting na Yanga itakayochezwa Aprili 17 mwaka huu jijini Tanga.
Tatizo hilo pia limeathiri mechi za Ligi Kuu ya Kenya (KPL) ambazo hazitaonekana wikiendi hii. SuperSport ndiyo yenye haki za matangazo ya televisheni kwa ligi hiyo ya Kenya.
Tshunungwa amekutana na Sekretarieti ya TFF na Kamati ya Ligi kuelezea tatizo hilo. SuperSport kwa kushirikiana na Kamati ya Ligi na TFF watapanga mechi nyingine za Super Week kabla ya ligi kumalizika msimu huu.
Pia TFF, Kamati ya Ligi na SuperSport watakuwa na mkutano mfupi wa waandishi wa habari wakati wa mapumziko kwenye mechi ya leo kati ya Yanga na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)