Thursday, November 27, 2014

FIFA YATOA LISTI YA UBORA DUNIANI TANZANIA YAPOROMOKA NAFASI 2 SAS YA 112.

SHIRIKISHO la soka Duniani FIFA Leo hii imetoa Listi ya Ubora Duniani na Mabingwa wa Dunia Germany wameendelea kushika Namba Moja huku Tanzania ikiporomoka Nafasi 2 na kukamata Nafasi ya 112.
Kulikuwa hamna mabadiliko yeyote ya Timu 7 za juu lakini England, iliyokuwa Nafasi ya 20, imepanda Nafasi 7 na sasa kukamata Nafasi ya 13.
Barani Afrika, Ageria imeendelea kuwa juu kabisa ikiwa Nafasi ya 18 baada kushuka Nafasi 3 ambapo Listi ya Ubora Duniani inayofuata itatolewa Tarehe 18 Desemba 2014.
20 BORA HII HAPA.
1.Germany               
2.Argentina   
3.Colombia    
4.Belgium      
5.Netherlands
6.Brazil
7.Portugal               
8.France
9.Spain          
10.Uruguay                
11.Italy           
12.Switzerland 
13.England                
14.Chile           
15.Romania                
16.Costa Rica  
17.Czech Republic      
18.Algeria       
19.Croatia       
20.Mexico

UONGOZI WA LIPULU FC YATUPIA VIRAGO BENCHI LA UFUNDI


Timu ya Lipuli FC ya Iringa kupitia uongozi wake umeamua kutitupilia virago benchi lake lote la ufundi kutokana na matokeo yasiyoridhisha ya timu yake katika Ligi Daraja la Kwanza (FDL).
          
Mwenyekiti wa timu hiyo Abuu Changawa amesema wamefikia hatua hiyo baada ya timu yao kuwa na mwendo wa konokono katika ligi hiyo wakiwa nafasi ya tatu katika msimamo wa Kundi A.

Pamoja na kwamba wapo katika nafasi ya tatu kwenye         msimamo wa kundi letu, matokeo ya timu yetu hayaridhishi. Tumekuwa tukishinda 1-0 na kutoka sare ndiyo maana tumeaona tuachane na watendaji wote wa benchi la ufundi,” amesema Majeki.

Lipuli FC, aliyowahi kuifundisha Shadrack Nsajigwa (sasa kocha msaidizi Yanga), imekusanya pointi 21 katika mechi zote 11 za raundi ya kwanza ya FDL, pointi moja nyuma ya Friends Rangers walioko nafasi ya pili na tatu nyuma ya Majimaji FC wanaoshika usukani wa kundi hilo.

Aidha, Majeki amesema kuanzia Alhamisi wataanza msako wa kukamata watu wote wanaojihusisha na biashara haramu ya kutengeneza na kuuza jezi zenye nembo ya klabu yao kwa kuwa hadi sasa hakuna kampuni wala mtu aliyeidhinishwa kutengeneza na kuuza jezi zenye 

EMERSON AANZA TIZI LA KUJIUNGA NA YANGA CHINI YA MAXIMO.

Mbrazil, Emerson Roque ambae anacheza nafasi ya Kiungo leo ameanza kujifua katika kikosi cha Yanga.

Taarifa zilizopo Emerson atafanya majaribio kwa wiki mbili, ambapo leo imekuwa siku ya kwanza.
                 
Katika mazoezi hayo ya Yanga kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam kulikuwa na ulinzi mkali.

Emerson ambaye inaelezwa atachukua nafasi ya mshambuliaji, Jaja alionekana kama vile amezoeana na wachezaji wengine wa Yanga.


Pamoja naye, kiungo Coutinho na Kocha Marcio Maximo, nao walianza mazoezi yao kwa mara ya kwanza baada ya kurejea nchini, jana.