Tuesday, May 14, 2013

AL AHLY KUUMANA USO KWA USO NA USO NA MAHASIMU WAO MISRI ZAMALEK

Katika Jijini Cairo, Misri  hii leo Droo ya hatua ya Makundi ya Mashindano ya CAF ya CHAMPIONZ 
LIGI imechukua nafasi na Mabingwa Watetezi Al Ahly wataanza utetezi wa Taji lao kwa kucheza Ugenini na wenzao Mahasimu wao wakubwa wa huko Misri Zamalek ambao wamepangwa pamoja kwenye Kundi A.
Hii ni mara ya pili kwa Miaka miwili mfululizo kwa
 Miambahiyo ya Misri kupangwa Kundi moja kwenye
michuano hii na safari hii wako pamoja na Orlando
 Pirates ya SouthAfrica na Timu mpya kwenye
 Mashindano haya ACLeopards ya Congo ambayo
 Mwaka jana ilitwaa Kombe la Shirikisho.
aidha Kundi B lina Timu za Esperance ya Tunisia, ambayo ndio ilitolewa Fainali na
 Al Ahly kwenye michuano hii Mwaka jana, na nyingine ni Coton Sport ya Cameroo
n, Sewe Sport ya Ivory Coast na Recreativo de Libolo of Angola, ambao ndio
 waliwatupa nje ya michuano hii waliokuwa Mabingwa wa Tanzania, Simba SC.
hata hivyo Mechi za Makundi zitachezwa kwa Mtindo wa Ligi wa Nyumban
i na Ugenini na Washindi wawili wa juu wa kila Kundi watasonga Nusu Fainali.
Mechi za Makundi zitachezwa kuanzia Julai hadi Septemba huku Nusu Fainali
ikitarajiwa kuwa Oktoba.
DROO:
KUNDI A
Al Ahly  (Egypt)
AC Leopards (Congo)
Orlando Pirates (South Africa)
Zamalek (Egypt)
KUNDI B
Esperance (Tunisia)
Coton Sport (Cameroon)
Recreativo de Libolo (Angola)
Sewe Sport (Ivory Coast)
HABARI HII YA CHINI TULIITOA MEI 7
CAF KOMBE LA SHIRIKISHO: DROO RAUNDI YA MCHUJO YAFANYWA"
DROO YA RAUNDI YA MCHUJO:
TP Mazembe (DRC) v Liga Muculmana (Mozambique)
St George (Ethopia) v ENPPI (Egypt)
Stade Malien (Mali) v Lydia Academic (Burundi)
Enugu Rangers (Nigeria) v CS Sfaxien (Tunisia)
FUS Rabat (Morocco) v FAR Rabat (Morocco)
CA Bizertin (Tunisia) v Ismaily (Egypt)
Entente Setif (Algeria) v US Bitam (Gabon)
JSM Bejaia (Algeria) v Etoile Sahel (Tunisia)
-MECHI KUCHEZWA Mei 17-19 na Marudiano Mei 31-Jun1 2
-FAHAMU: WASHINDI 8 WA RAUNDI HII WATAINGIZWA KWENYE
 DROO KUPANGA MAKUNDI MAWILI YA TIMU 4 KILA MOJA.

VICENTE ASEMEA NEYMAR HUENDA AKAELEKEA BAYEN MUNICH

OFISA wa zamani wa klabu ya Santos ya Brazil, Vicente Cascione amedai kuwa mshambuliaji nyota wa klabu hiyo Neymar ataondoka kwenda klabu ya Bayern Munich ya Ujerumani katika kipindi cha majira ya kiangazi kuungana na kocha wa zamani wa Barcelona Pep Guardiola. Barcelona ndio wanaonekana kuwa katika nafasi nzuri ya kupata saini ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 21, ambaye amepanga kwenda Catalunya baada ya michuano ya Kombe la Shirikisho kuzungumzia uhamisho wake wakati Real Madrid nao wakimnyatia kimya kimya nyendo zake. Hata hivyo, Cascione amesisitiza kuwa Neymar atakwenda kucheza katika Ligi Kuu nchini Ujerumani, Bundesliga kwani tayari taratibu za uhamisho kwenda Allianz Arena umeshakamilika. Ofisa huyo aliandika katika blog yake kuwa amezinasa taarifa hizo akiwa wa kwanza kwamba Neymar tayari ameshamwaga wino Bayern hivyo hatakwenda Hispania kama inavyodhaniwa na wengi.

BLATTER ASEMA AS ROMA WALIYOPEWA ADHABU NDOGO KWA UBAGUZI.


RAIS wa Shirikisho ka Soka Duniani-FIFA, Sepp Blatter ameponda adhabu ya faini ya kiasi cha euro 50,000 waliyopewa klabu ya AS Roma ya Italia kwa tabia za kibaguzi walizoonyesha mashabiki wake akidai kuwa ni ndogo na haikubaliki. Blatter amesema atazungumza na Shirikisho la Soka la Italia ambalo amedai kuwa hawakufanya uchunguzi wa kutusha kuhusiana na tukio hilo la lililotokea Jumapili iliyopita katika katika mchezo kati ya AC Milan na Roma kwenye Uwanja wa San Siro. Blatter aliuambia mtandao wa FIFA kuwa ameshangazwa na kushindwa kuelewa kwanini kamati ya nidhamu ya shirikisho la soka la nchi hiyo itoe maamuzi wa kuwatoza faini Roma kwa kipindi kifupi namna hiyo bila kuchunguza tukio kwa undani. Amesema kiwango walichotozwa Roma ni kidogo sana ukilinganisha ukubwa wa tatizo lenyewe ndio maana anataka kuzungumza na shirikisho hilo kuwatahadharisha kuwa njia waliyotumia sio sahihi kama wanataka kutokomeza tatizo hilo.

MFAHAMU KWA UZURI ROBERTO MANCIN KATIKA HARAKATI ZA SOKA DUNIA

Roberto Mancini
Roberto Mancini 008.jpg
Taarifa kuhusu yeye
Full nameRoberto Mancini
Date of birth27 November 1964 (age 48)
Place of birthIesi, Italy
Height1.79 m (5 ft 10 12 in)
Playing positionAttacking midfielder/Second striker
Timu alizocheza
mwakaTimumechi (Goli)
1981–1982Bologna30(9)
1982–1997Sampdoria424(132)
1997–2001Lazio87(15)
2001Leicester City (loan)4(0)
Total545(156)
Timu ya taifa
1982–1986Italy U2126(9)
1984–1994Italy36(4)
Timu maneja
2001–2002Fiorentina
2002–2004Lazio
2004–2008Internazionale
2009–2013Manchester City


MATAJI ALIOTWAA NA TIMU HIZI

Sampdoria
Serie A (1): 1990-1991
Coppa Italia (4): 1984-85, 1987-88, 1988-89, 1993-94
Supercoppa Italiana (1): 1991
Kombe la UEFA Cup Winners '(1): 1989-1990

Lazio
Serie A (1): 1999-2000
Coppa Italia (2): 1997-98, 1999-2000
Supercoppa Italiana (1): 1998
Kombe la UEFA Cup Winners '(1): 1998-1999
UEFA Super Cup (1): 1999

TIMU MANEJA
Fiorentina
Coppa Italia (1): 2000-01
Lazio
Coppa Italia (1): 2003-04

Internazionale
Serie A (3): 2005-06, 2006-07, 2007-08
Coppa Italia (2): 2004-05, 2005-06
Supercoppa Italiana (2): 2005, 2006

Manchester City
Ligi Kuu (1): 2011-12
Kombe la FA (1): 2010-11
FA Community Shield (1): 2012

TUZO NA MAFANIKIO
Guerin d'Oro (2): 1987-88, 1990-91
Serie Mchezaji wa Mwaka (1): 1996-1997
Italia Mchezaji wa Mwaka (1): 1996-1997
Albo Panchina d'Oro (1): 2007-08
Ligi Kuu ya Meneja wa Mwezi (2): Desemba 2010, [95] Oktoba 2011 

UFAFANUZI KUHUSU LIGI YA MABINGWA MIKOA

LIGI ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) ilianza tarehe 12 Mei 2013 ikishirikisha klabu bingwa za mikoa yote ya Tanzania Bara, isipokuwa mikoa ya Pwani na Manyara ambayo kutokana na sababu tofauti ilishindwa kuwasilisha majina ya klabu zake hadi siku ya mwisho iliyowekwa na Kamati ya Mashindano, yaani tarehe 10 Mei 2013.

Suala la kukosekana kwa wawakilishi wa mikoa hiyo miwili limezua maswali mengi kiasi kwamba Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linalazimika kutoa ufafanuzi kwa faida ya wadau wote wa mpira wa miguu.

Ligi ya Mabingwa wa Mikoa, ambayo ni mpya baada ya TFF kubadilisha mfumo wa uendeshaji wa mpira wa miguu, ilipangwa kuanza tarehe 5 Mei 2013, lakini hadi tarehe ya mwisho ya kuwasilisha majina ya mabingwa wa mikoa, yaani tarehe 2 Mei 2013 mikoa michache ndiyo iliyokuwa imemaliza ligi zao na kupata mabingwa.

Kuchelewa huko kwa mikoa kumaliza ligi zao kuliilazimisha Kamati ya Mashindano ya TFF kuongeza muda wa mikoa kuwasilisha majina ya wawakilishi hao hadi tarehe 10 Mei 2013 na hivyo siku ya kuanza kwa Ligi kusogezwa mbele hadi tarehe 12 Mei 2013.

Hadi kufikia tarehe hiyo mpya ya mwisho ya kuwasilisha majina ya mabingwa wa mikoa, ni mikoa sita tu iliyofaidika na kuongezwa huko kwa muda na kupata wawakilishi wake. Mikoa hiyo ni Iringa, ambayo pamoja na kuongezwa kwa muda, iliandika barua ya kuihakikishia Kamati ya Mashindano kuwa itapata bingwa kabla ya kuisha kwa siku ya tarehe 10 Mei 2013.

Mikoa mingine ni Lindi, Mtwara, Geita, Tabora na Dodoma.
Mkoa wa Manyara haukuweza kumaliza ligi yake hadi mwisho wa siku ya tarehe 10 Mei 2013 na hivyo Kamati ya Mashindano iliyosubiri majina hadi saa 12:00 jioni siku hiyo kuamua kuwaondoa wawakilishi wa Manyara kwenye ratiba.

Awali, Kamati ya Mashindano iliamua kuwa ratiba ya mechi za Ligi ya Mabingwa wa Mikoa ipangwe tarehe 7 Mei 2013, ikishirikisha mikoa ambayo ilishapata mabingwa wake, lakini baada ya kuona baadhi ya mikoa ilikuwa haijakamilisha ligi zake, Kamati iliamua kuwa ratiba ipangwe kwa kutumia majina ya mikoa kwa matumaini kuwa hadi kufikia tarehe 10 Mei 2013, mikoa itakuwa imeshapata wawakilishi wake na kwa kuwa ratiba inahusu mikoa jirani, ingekuwa rahisi kwa timu kusafiri kutoka kituo kimoja hadi kingine.

Lakini Mkoa wa Manyara haukuweza kufanya hivyo na Kamati kulazimika kuuondoa kwenye ratiba kutokana na kushindwa kukidhi utashi huo.



Mkoa mwingine ambao uliondolewa kwenye ratiba ni Pwani ambayo pamoja na kutuma jina la mwakilishi wake, Kamati ilipokea malalamiko kutoka klabu zilizoshiriki Ligi ya Mkoa, zikidai kuwa jina la bingwa wa Pwani lililowasilishwa TFF lilikuwa batili kwa kuwa klabu ya Kiluvia United haikustahili kushiriki Ligi ya Mkoa kutokana na ukweli kuwa haijasajiliwa mkoani Pwani na wala haikushiriki ligi ya mkoa msimu uliopita. Kamati ya Mashindano iliiondoa Pwani kwenye ratiba na kulirudisha suala hilo mkoani.

Ingawa Katibu wa Pwani alijaribu kuishawishi Sekretarieti ya TFF iliangalie suala hilo kwa undani zaidi, Sekretarieti ilimjibu kuwa lilishafanyiwa uamuzi na Kamati, hivyo uamuzi huo usingeweza kutenguliwa na kumshauri katibu huyo arejee mkoani kwake kuwasiliana na viongozi wenzake kuona ni jinsi gani mkoa unaweza kunusuru hali hiyo kwa kufanya uamuzi ambao ungeuwezesha mkoa kupata mwakilishi.

Kwa mantiki hiyo, masuala ya Manyara na Pwani yalikuwa ndani ya uongozi wa mikoa husika na si Kamati ya Mashindano ya TFF kwa kuwa Kamati ilitaka ipatiwe jina la bingwa ambaye alipatikana kwa mujibu wa mfumo mpya wa Ligi ya Mikoa.

Ligi ya Mabingwa wa Mikoa inachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini na hivyo timu zilizokutana tarehe 12 Mei 2013, zitarudiana mwishoni mwa wiki hii na kupatikana timu zitakazosonga mbele kwenye raundi nyingine hadi timu tatu bora zitakazopanda daraja kwenda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zitakapopatikana.

Ligi za Mikoa, kwa mujibu wa kanuni mpya, zinatakiwa ziwe na timu kati ya 16 na 20 na zinatakiwa zicheze mechi mbili za nyumbani na ugenini, hata kama zitakuwa zinatumia uwanja mmoja.

Uamuzi wa kubadilisha mfumo huo ulifanywa ili kuhakikisha kuwa mikoa inakuwa na na mashindano kwa mwaka mzima na hivyo kuiwezesha mikoa kujikita katika kutafuta mbinu za kupata fedha na kuendeleza mchezo wa mpira wa miguu kwenye mikoa yao.

Uamuzi huo pia unasaidia kupunguza mtindo wa wachezaji kuzunguka klabu tofauti katika msimu mmoja kwa kuwa wanalazimika kutulia kwenye klabu moja hadi muda wa usajili unapofika.

Pamoja na wachezaji kutulia sehemu moja kwa muda mrefu, pia walimu wanapata fursa ya kujikita vizuri kwenye programu zao kwa kuwa wanakuwa na uwezo wa kufuatilia maendeleo ya wachezaji wao.


Pamoja na hayo yote, mfumo huo utasaidia kurudisha msisimko kwenye mikoa na hivyo kutoa fursa kwa vijana wengi wenye vipaji kuonekana na kuendelezwa.

TFF inatoa wito kwa viongozi wa mikoa kuanza kubuni sasa mikakati ya kuendesha ligi hizo msimu unaokuja kwa kuwa hakutakuwa na nafasi tena ya kuongeza muda kwa mikoa kuwasilisha majina ya wawakilishi wao.

KIINGILIO MECHI YA SIMBA, YANGA 5,000/-
Kiingilio cha chini kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Yanga itakayochezwa Jumamosi (Mei 18 mwaka huu) kitakuwa sh. 5,000. Kiingilio hicho kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648.

Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu kiingilio ni sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa itakuwa sh. 10,000, VIP C kiingilio ni sh. 15,000, VIP B itakuwa sh. 20,000 wakati VIP A yenye viti 748 tu tiketi moja itapatikana kwa sh. 30,000.  

Tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo huo utakaoanza saa 10 kamili jioni.

Mwamuzi wa mechi hiyo atakuwa Martin Saanya kutoka Morogoro ambapo atasaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha, na Jesse Erasmo kutoka Morogoro. Mwamuzi wa akiba ni Hashim Abdallah wa Dar es Salaam.

Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati mtathmini wa waamuzi (referees assessor) ni Leslie Liunda.

KOCHA KIM KUZUNGUMZIA MECHI YA MOROCCO
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya tiketi kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco. Mkutano huo utafanyika keshokutwa (Mei 16 mwaka huu) saa 5 kamili kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu kwenye jiji la Marrakech nchini Morocco. Taifa Stars ilishinda mechi yake iliyopita jijini Dar es Salaa kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Morocco.

Angetile Osiah
Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

ROBERTO MANCINI HUYOO NJE ATUPIWA VIRAGO MAN CITY


Wakisheherekea ubingwa wao Timu ya Manchester United huku ikimuaga kwa kila heri Meneja wao Sir Alex Ferguson baada ya Miaka 26 ya Utumishi uliojawa na furaha tele kwa Jumapili walikabidhiwa Kombe la Ubingwa England na Jumatatu Jioni wakizunguuka nalo Mitaa ya Jiji hilo  kwa Maandamano ya furaha kubw lakini upande wa pili wa Manchester City mekuwa na majonzi makubwa  baada ya kuukosa Ubingwa na Juzi kukosa FA CUP walitandikwa na Wigan kwenye Fainali, na hili leo kilio chao kuhitimishwa kwa  Meneja wao Roberto Mancini kutupiliwa virago katika timu hiyo.
kitu kilichopelekea kutimuliwa kazi kwa Roberto Mancini alidumu kwa Miaka mitatu na nus, tamko la Klabu lisema: manchin Ameshindwa kutimiza malengo ya Klabu Msimu huu ukiachia kufuzu kucheza UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu ujao.
Klabu hiyo imesema Meneja Msaidizi, Brian Kidd, ambae alishawahi kuwa Msaidizi wa Sir Alex Ferguson huko Man United, ndio atakaimu nafasi hiyo kwa Mechi zao mbili za BPL zilizobaki za Msimu huu na pamoja na Ziara yao ya kabla ya Msimu mpya kuanza ya huko Marekani.
MANCINI_n_BALOTELLI-MSHIKEMSHIKERoberto Mancini alitwaa kibarua Man City Desemba 2009 alipotimuliwa Mark Hughes na kuiongoza kutwaa FA CUP Mwaka 2011 na Ubingwa wa England 2012 lakini mara baada ya Jumamosi kufungwa Fainali ya FA CUP Bao 1-0 na Wigan kipigo ambacho kinafuatia kupokonywa Ubingwa wao na Mahasimu wao Man United, Mancini alionekana kukalia kuti kavu baada ya kumaliza Msimu huu mikono mitupu.
Mara baada kufungwa na Wigan kwenye FA CUP, Mancini alikurupuka na kuulaumu uongozi wa Man City kwa kutokanusha uvumi wa Pellegrini, Raia wa Chile, kuja kutwaa kazi yake.
aidha baadhi ya Wachambuzi huko England wamemponda Mancini na kudai hana haki ya kuilaumu Man City kwani hata yeye alipoteuliwa kwenda Klabu hiyo Mark Hughes alikuwa bado Meneja.
hata hivyo ingawa Mancini aliiwekea Man City historia nzuri ya kutwaa Kombe lao la kwanza baada ya
Miaka 35 walipotwaa FA CUP na kutwaa Ubingwa wao wa kwanza baada ya Miaka 44, kumaliza Msimu huu kwa ukame kunadaiwa kuwakera Wamiliki Matajiri wa Man City toka Falme za Nchi za Kiarabu ambao Jumamosi walikuwa Wembley kushuhudia Timu yao ikitwaa Kombe kwa mgongo wa ‘vibonde’ Wigan lakini wakajikuta chali baada ya kutunguliwa Bao 1-0 na Kombe la FA CUP kwenda Wigan, Timu ambayo huenda Msimu huu ikaandika Historia ya kuwa Klabu ya kwanza kutwaa FA CUP na kushushwa toka Ligi Kuu Msimu huo huo.
Kocha ambaye anatarajiwa kuchukuwa mikoba ya  manchin ni Manuel Pellegrini, Kocha wa Malaga ya Spain raia wa Chile, atapewa wadhifa wa kumrithi Mancini ingawa mwenyewe amesisitiza hayo si kweli.