Sunday, February 16, 2014

JUVE WAJIHAKIKISHIA UBINGWA WAKO JUU POINTI 12 MBELE YA AS ROMA

JUVENTUS Mabingwa wa Italy wakiwa katika dimba la Nyumbani wamefanikiwa kuichapa Timu ya Chievo Verona  Bao 3-1 Mabao ya Kwadwo Asamoah, Mchezaji kutoka Ghana, na Claudio Marchisio pamoja na Fernando Llorente huku Chievo Verona ikijipatia Bao moja baada ya Juve kujifunga wenyewe wakati Stefan Lichtsteiner akiwa katika harakati za kuokoa na Mpira kumgonga Martin Caceres na kutinga wavuni
Jumamosi Februari 15
ACF Fiorentina 1 Inter Milan 2
[Saa za Bongo]
Jumapili Februari 16
Calcio Catania 3 SS Lazio 1
Atalanta BC 0 Parma FC 4
Juventus FC 3 AC Chievo Verona 1
Cagliari Calcio 1 AS Livorno Calcio 2
Genoa CFC 3 Udinese Calcio 3
US Sassuolo Calcio 0 SSC Napoli 2
2245 AS Roma v UC Sampdoria
Jumatatu Februari 17
2245 Hellas Verona FC v Torino FC

MSIMAMO-Timu za Juu:
NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 Juventus FC 24 20 3 1 59 19 40 63
2 AS Roma 22 15 6 1 45 11 34 51
3 SSC Napoli 24 15 5 4 49 27 22 50
4 ACF Fiorentina 24 13 5 6 43 26 17 44
5 Inter Milan 24 10 9 5 42 28 14 39
6 Parma FC 23 9 9 5 36 27 9 36
7 Hellas Verona 23 11 3 9 39 37 2 36
8 Torino FC 23 8 9 6 36 30 6 33
9 AC Milan 24 8 8 8 37 35 2 32

LA LIGA-REAL MADRID YAINYUKA GETAFE CF NYUMBANI 3-0

Real Madrid, ambao hawajapoteza Mechi tangu wafungwe na Barca 2-1 katika uwanja wa Nou Camp Mwezi Oktoba, Leo wakicheza dhidi ya Getafe bila ya Mshambuliaji wao Mahiri Cristiano Ronaldo, ambae yuko Kifungoni Mechi 3, walianza kufunga kwa Bao la Jese katika Dakika ya 6, kisha Dakika ya 27 Benzema akapiga Bao la Pili na Modric kupiga Bao la Tatu Dakika ya 66.
Ambapo hapo Jana, fc Barcelona waliifumua Rayo Vallecano Bao 6-0 na Atletico Madrid waliichapa Real Valladolid Bao 3-0.
RATIBA
Jumamosi Februari 15
Atletico de Madrid 3 Real Valladolid 0
Levante 1 UD Almeria 0
FC Barcelona 6 Rayo Vallecano 0
Villarreal CF 0 Celta de Vigo 2
Jumapili Februari 16
Granada CF 1 Real Betis 0
Getafe CF 0 Real Madrid 3
2100 Athletic de Bilbao v RCD Espanyol
2300 Sevilla FC v Valencia
Jumatatu Februari 17
2400 Malaga CF v Real Sociedad
MSIMAMO-Timu za Juu:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
FC Barcelona
24
19
3
2
69
17
52
60
2
Real Madrid CF
24
19
3
2
68
24
44
60
3
Atletico Madrid
24
19
3
2
59
16
43
60
4
Athletic Bilbao
23
13
5
5
42
28
14
44
5
Villarreal CF
24
12
4
8
44
29
15
40
6
Real Sociedad
23
10
7
6
42
34
8
37
7
Sevilla FC
23
8
7
8
42
41
1
31
8
Valencia
23
9
4
10
36
35
1
31

TAMBWE JEZI NAMBA 17 NA MABAO 17 MSIMBAZI SIMBA SC


Amisi Tambwe, raia wa Burundi ni moja kati ya washambiliaji mahiri mwenye kujitambua akiwa uwanjani ambapo amedhihirisha kuwa yeye ni mkali wa mabao
kutokana katika mechi 23 alizoichezea Simba SC hadi sasa za mashindano yote na kirafiki, amefunga mabao 17.
Kwa sasa, Tambwe ndiye mchezaji anayeongoza kwa mabao katika Ligi Kuu, akiwa amefunga mabao 15 na anafuatiwa kwa mbali na mshambuliaji wa AzamFC, Kipre Herman Tchetche raia wa Ivory Coast, mwenye mabao 10.
Tambwe amekuwa kipenzi cha wana Msimbazi kutokana na kuweza pia kutikisa nyavu za mahasimu, Yanga SC katika mechi mbili mfululizo baina ya timu hizo.
Tambwe alikuja Simba SC kwa pamoja na Mrundi mwenzake, beki Gilbert Kazewakitokea wote Vital’O msimu huu, baada ya kung’ara katika Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame nchini Sudan wakiiwezesha klabu yao kutwaa taji la michuano hiyo kwa mara ya kwanza katika historia yake.

Hata hivyo, Kaze amepoteza namba katika kikosi cha kwanza tangu ujio wa kocha Mcroatia, Zdravko Logarusic, ambaye amekuwa akimpanga beki Mkenya, Donald Mosoti aliyetokea naye Gor Mahia ya Kenya.  

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI

DSC00207MTOTO AFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA BARABARANI MKOANI MBEYA.
MTOTO ALIYETAMBULIKA KWA JINA LA FRED ROBERT (08) MWANAFUNZI WA DARASA LA PILI KATIKA SHULE YA MSINGI MBALIZI NA MKAZI WA MBALIZI ALIFARIKI DUNIA PAPO HAPO BAADA YA KUGONGWA NA PIKIPIKI ISIYOFAHAMIKA NAMBA ZAKE ZA USAJILI WALA DEREVA WAKE. 
TUKIO HILO LILITOKEA MNAMO TAREHE 15.02.2014 MAJIRA YA SAA 13:00HRS MCHANA HUKO MBALIZI WILAYA YA MBEYA VIJIJINI. 
CHANZO CHA AJALI NI MWENDO KASI WA PIKIPIKI HIYO. DEREVA ALIKIMBIA MARA BAADA YA TUKIO, JUHUDI ZA KUMTAFUTA ZINAENDELEA. 
MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI TEULE YA IFISI. KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI ROBERT MAYALA ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MAHALI ALIPO MTUHUMIWA WA TUKIO HILI AZITOE KWA JESHI LA POLISI ILI AKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
JESHI LA POLISI LINAWASHIKILIA WATU WAWILI WAKIWA NA SILAHA [PISTOL] BILA KIBALI.
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WAWILI 1. JACKSON MWAKALUNGWA (24) NA 2. SAIKO WAILODI (35) DEREVA WOTE WAKAZI WA MLOWO WAKIWA NA SILAHA AINA YA PISTOL ILIYOTENGENEZWA KIENYEJI NA INAYOTUMIA RISASI ZA SHOTGUN.
 WATUHUMIWA HAO WALIKAMATWA MNAMO TAREHE 14.02.2014 MAJIRA YA SAA 14:25HRS MCHANA HUKO KATIKA KIJIJI CHA MAHENGE WILAYA YA MBOZI MKOA WA MBEYA.
 MTUHUMIWA JACKSON MWAKALUNGWA ALIKAMATWA AKIWA NDANI YA GARI AINA YA TOYOTA HIACE AKIELEKEA WILAYA YA MBARALI KUFANYA UHALIFU NA ALIKIRI KUAZIMISHWA SILAHA HIYO NA MTUHUMIWA ALIYEMTAJA KWA JINA LA SAIKO WAILODI. TARATIBU ZA KISHERIA ZINAFANYWA ILI WATUHUMIWA WAFIKISHWE MAHAKAMANI. 
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI ROBERT MAYALA ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA TABIA YA KUJIMILIKISHA SILAHA BILA KIBALI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA. 
AIDHA ANATOA WITO KWA JAMII KUTOA TAARIFA KWA JESHI LA POLISI ZA MTU/WATU WANAOWATILIA MASHAKA AU PINDI WAONAPO VIASHIRIA VYA WATU KAMA HAO KATIKA MAENEO YAO ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
Signed by:
[ROBERT MAYALA – ACP]
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

AZAM FC NJE YALALA 2-0 MBELE YA WAMAKONDE WA MSUMBIJI:

Wawakilishi wa Tanzania,katika michuano ya Kombe la Shirikisho.  Barani afrika Azam FC wabwagwa katika michuano hiyo.
Azam FC imefungwa mabao 2-0 na wenyeji wake Ferreviario ya Msumbuji maarufu kama Wamakonde katika mechi iliyopigwa hii leo mjini Beira.
Katika mechi ya kwanza Azam FC ilishinda bao 1-0 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamzi jijini Dar. Mfungaji akiwa Kipre Tchetche.

Kutokana na kipigo cha leo, maana yake Azam FC imetolewa kwa jumla ya mabao 2-1 na kuifanya kutoka mapema zaidi katika michuano hiyo ndani ya misimu mitatu.

MFAHAMU KWA UZURI JACK WILSHERE ALIPOTOKA KIMICHEZO"

Jack Andrew Wilshere (amezaliwa 1 Januari 1992 katika sehemu ya Stevenage, Hertfordshire) ni mwanasoka wa Uingereza anayeichezea klabu ya Arsenal ya ligi kuu ya Uingereza. Kwa kawaida yeye hucheza kama kiungo wa kati anayeshambulia {mshambuliaji} na hutumia mguu wa kushoto sanasana.


Wasifu wa Klabu

Wilshere alijiunga na Arsenal Academy mnamo Oktoba 2001 akiwa na umri wa miaka tisa, baada ya kuwa mwanafunzi katika shule ya kandanda ya Luton Town kwa miezi miwili. Alipanda safu ya Arsenal, na alipokuwa na umri wa miaka 15 alitajwa kama nahodha wa timu ya vijana ya wasiozidi umri wa miaka 16 ya Arsenal; pia aliichezea timu ya vijana wasiozidi umri wa miaka 18. Katika majira ya jua ya mwaka wa 2007 Wilshere alishiriki katika Kombe la vijana la Mabingwa na aliporejea nchini Uingereza, kocha wa Arsenal Academy, Steve Bould alimwanzisha katika mechi ya timu ya vijana wasiozidi umri wa miaka 18 dhidi ya timu ya vijana wasiozidi umri wa miaka 18 ya Chelsea. Alifunga bao lake la kwanza dhidi ya timu ya vijana wasiozidi umri wa miaka 18 ya Aston Villa katika ushindi wa 4-1. Kisha alifunga mabao tatu dhidi ya timu ya vijana wasiozidi umri wa miaka 18 ya Watford, na kuisaidia timu yake kushinda taji la Academy la Kundi A .

Mnamo Februari 2008, alicheza mechi yake ya kwanza ya timu hifadhi ya Arsenal dhidi ya Reading na alifunga bao la kipekee la Arsenal la mechi ingawa walipoteza mechi hiyo baada ya bao la Simon Church. Aliicheza timu ya vijana wasiozidi umri wa miaka 16 ya Arsenal katika ushindi wa Kombe la Atalanta, na alitajwa kama mchezaji bora katika shindano hilo. Alikuwa sehemu muhimu katika ushindi wa Arsenal wa kombe la vijana la FA mwaka wa 2009, kwani alifunga mabao katika nusu fainali na alitajwa kama mchezaji bora wa mechi baada ya kuonyesha mchezo uliosisimua katika mechi ya kwanza ya fainali dhidi ya Liverpool kwa kuandaa pasi mbili muruwa zilizosababisha mabao na kufunga bao moja mwenyewe.

Mnamo Julai 2008, Wilshere alichaguliwa katika timu ya kwanza ya Arsenal katika mechi za kirafiki ambazo zinachezwa kabla ya msimu kuanza. Alicheza mechi yake ya kwanza ya timu kuu dhidi ya timu ya kwanza ya Barnet kama mbadala wa Henri Lansbury baada ya nusu ya kwanza ya mechi na kuandaa bao lililofungwa nanJay Simpson. Wilshere alifunga mabao yake ya kwanza mawili ya Arsenal katika ushindi wa 10-2 dhidi ya Burgenland XI, na tena baadaye siku mbili katika mechi ya kirafiki dhidi ya Stuttgart.

Meneja wa Arsenal Arsène Wenger alimpa Wilshere nafasi katika kikosi cha timu ya kwanza ya Arsenal msimu wa 2008-09, na alipewa jesi lenye namba 19. Alicheza mechi yake ya kwanza ya ushindani katika mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza dhidi ya Blackburn Rovers kaatika uga wa Ewood Park mnamo Septemba 2008, kama mbadala wa Robin van Persie katika dakika ya 84. Akiwa na umri wa miaka 16 na siku 256, alikuwa mchezaji mchanga zaidi wa Arsenal milele kucheza mechi ya ligi kuu ya Uingereza, rekodi ambayo awali ilishikiliwa na Cesc Fabregas. Siku kumi baadaye, mnamo 23 Septemba, Wilshere alifunga bao lake la kwanza la timu kuu ya Arsenal katika ushindi wa 6-0 dhidi ya Sheffield United katika kombe la Carling.

Tarehe 25 Novemba 2008, Wilshere aliingia kama mbadala katika mechi ya ligi ya mabingwa barani Ulaya dhidi ya Dynamo Kyiv na kuwa mchezaji wa tano mwenye umri wa miaka kumi na sita milele kucheza katika Ligi ya Mabingwa barani. Mnamo Januari 2009 Wilshere alisaini mkataba wake wa kwanza wa utaalamu na kuiendeleza hadi Julai mwaka huohuo.

Katika maandalizi ya msimu wa 2009-10, Wilshere alifunga mara mbili na mara mbili alitajwa kama mchezaji bora wa mechi huku Arsenal ikishinda shindano hilo la kirafiki linalojulikana kama kombe la Emirates.

Tarehe 22 Septemba 2009, Wilshere alianza mechi ya Arsenal katika ushindi wa 2-0 katika Kombe la Carling dhidi ya FC West Bromwich Albion. Katika dakika ya 37 ya mechi hiyo, alihusika katika tukio la utata na Jerome Thomas kwani Thomas aliusukuma uso wa Wilshere na kumsababisha kuonyeshwa kadi nyekundu. Baada ya tukio hilo, meneja wa West Brom, Roberto Di Matteo, alisema kuwa Wilshere alimtusi Thomas na alijishinikiza baada ya kusukumwa.

Wasifu wa Kimataifa
Tangu mwaka wa 2006, timu ya kandanda ya kitaifa ya Uingereza imeamua kumcheza Jack katika kundi la umri zaidi ya umri wake. Alipokuwa na umri wa miaka 15, aliichezea timu ya kandanda ya kitaifa ya Uingereza ya vijana wasiozidi umri wa miaka 17. Wilshere pia alikuwa na umri wa miaka 14 wakati aliichezea timu ya kandanda ya kitaifa ya Uingereza ya vijana wasiozidi umri wa miaka 16 mwaka wa 2006. Kisha alitajwa katika kikosi cha Uingereza ambacho kilishiriki katika shindano la kandanda la UEFA la vijana wasiozidi umri wa miaka 17 mwaka wa 2009 mwezi wa Mei, alianza mechi mbili za kwanza, hasa alisisimua katika mechi ya pili dhidi ya Ujerumani 2 kabla ya kuondolewa na jeraha ambayo ilimfanya asicheze mechi ya mwisho.
Pia amepokea sifa kutoka kwa meneja wa Uingereza, Fabio Capello ambaye alieleza kuwa kuna uwezekano kuwa kijana huyu wa Arsenal angejumuishwa katika kikosi cha Kombe la Dunia la mwaka wa 2010. Pia aliingia kama mbadala katika mechi yake ya kwanza ya timu ya Uingereza ya vijana wasiozidi umri wa miaka 21 dhidi ya Uholanzi.