Sunday, December 14, 2014

VARANE AWEKA WAZI KUWA ILIKUWA KIDOGO ATUE MAN UNITED

BEKI wa Real Madrid, Raphael Varane amabainisha kuwa ilibaki kidogo ajiunge na Manchester United kabla ya kukamilisha usajili wake Santiago Bernabeu.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa, alijiunga na Madrid akitokea klabu ya Lens mwaka 2011 kwa kitita cha euro milioni 10.
Hata hivyo, Varane amekiri kuwa alikuwa akifikiria kwenda Old Trafford lakini akaamua kwenda Maddrid kwani aliona ndio mahali pazuri kwa kuimarika kama mchezaji.

Varane amesema walikuwa wamekaribia kukubaliana na United kwnai mama yake anazungumza lugha ya kiingereza hivyo ndio alikuwa kama mkalimani lakini baada ya kufikiri sana akaona bora aende Madrid.

TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA HAPA NA PALE

Arsenal na Liverpool wanachuana Juventus katika kuwania saini ya beki wa kulia wa Barcelona Martin Montoya, mwenye 23 ambae amekosa namba kwenye kikosi cha barca.
Mshambuliaji Fernando Torres anaweza kurejea katika klabu yake ya Chelsea mwezi januari,Ac Milan wanampango wa kusitisha mkataba wake.
WENGER
Klabu yaNapol ya itali wanaangalia uwezekano wa kumsajili winga Yannick Bolasie, mwenye miaka 25 kutoka klabu ya Crystal Palace.
Brendan Rodgers
Timu ya Man United wako tayari kupamba na Real Madrid ili kuweza kupata saini ya kiungo Christoph Kramer anaekipiga na klabu ya Borussia Monchengladbach, pia kukiwa na tetesi beki.

ROGERS
Winga wa Chelsea Thorgan Hazard yuko tayari kujiunga na Borussia Monchengladbach kwa mkataba kamili baada ya kufanya vizuri katika msimu wake wa kwanza anakocheza kwa mkopo toka Chelsea.