Sunday, May 19, 2013

MOKOCHA 20 WANAOFUNDISHA SHULE ZA SECONDARI WAPEWA MAFUNZO.

MAKOCHA 20 wanaofundisha soka shule za sekondari na msingi sambamba na wale wa timu za mitaani mkoani Rukwa wamepewa mafunzo ya awali ya ukocha ili kuwaongezea ujuzi na ufanisi.
Mafunzo hayo ambayo yanafanywa na mkufunzi kutoka Chama cha Makocha Tanzania (Tafca), George Komba, yanafadhiliwa na Chama cha Makocha Mkoa wa Rukwa, ambako yatakuwa ya siku 12, yakishirikisha washiriki kutoka wilaya zote mkoani hapa.
Akizungumza na mwandishi wa blog hii Katibu wa Tafca Rukwa, Lusungu Kihaha ameeleza kuwa lengo ni kuwanoa makocha hao ili waweze kuzielewa kwa kina kanuni zote 17 za soka.
Ameongeza  na kusema kuwa ni matarajio yake ifikapo 2013-14 kuona soka la kistaarabu likichezwa viwanjani, kwani mpira wa miguu si uwanja wa vita, bali ni kuboresha mahusiano baina ya wachezaji, pia makocha na makocha wenzao.
Katibu wa Chama cha Soka Mkoa wa Rukwa (Rurefa), Godfrey Seko, alisema kuwa mara baada ya mafunzo hayo, hakuna kocha yeyote asiye na sifa atakayeruhusiwa kuketi katika benchi la ufundi kiwanjani wakati timu yake ikicheza.
Aidha amesema ni makocha wale tu wenye cheti cha awali, ndio watakaoruhusiwa kuketi kwenye benchi la ufundi wakati timu zao zikiumana na si vinginevyo.
hata hivyo Awali akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Shule ya Sekondari Sumbawanga, Kevas Masawe, amewataka washiriki hao kuutumia ujuzi huo shuleni na katika timu za mitaani ili kuinua vipaji vya soka vya Mkoa wa Rukwa.

WALIMU MASHULENI WATAKIWA KUHIMIZA NIDHAMU KWA WANAFUNZI

WALIMU wa michezo katika shule za msingi, sekondari na vyuo wametakiwa kuhamasisha suala la nidhamu kwa wanafunzi ili kuwajengea msingi ilio bora utakaowafanya wafike mbali.
Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Tabora, Joyce Ndonda, aliyekuwa mgeni rasmi katika bonanza maalumu la mchezo wa netiboli, lililofanyika kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini  humo.
Akizungumza na wanamichezo mbalimbali walioshiriki katika bonanza hilo, Ndonda ameipongeza Chaneta Tabora kwa kuanzisha bonanza hilo na kuwataka kuendelea na utaratibu huo, kwani ni chachu ya kukuza vipaji kwa vijana na kuinua hamasa ya michezo.
Aidha kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Mkoa wa Tabora, Kulwa Kavula, amesema lengo la bonanza hilo ni kuhamasisha wasichana na wadau wengine kuupenda mchezo huo.
Hata hivyo amewaomba wadau katika halmashauri zote za Mkoa wa Tabora kuwapa ushirikiano ili waweze kufanikisha harakati za kuinua michezo huo nchini.

BPL YAFIKIA TAMATI MAN U, MAN CITY, CHELSEA, ARSENAL KUCHEZA UEFA.

MATOKEO BPL LEO

England
 - Premier League (Table) 
 18:18May 19 
 FTChelsea2 - 1Everton
 FTLiverpool1 - 0Queens Park R.
 FTManchester C.2 - 3Norwich C.
 FTNewcastle U.0 - 1Arsenal
 FTSouthampton1 - 1Stoke C.
 FTSwansea C.0 - 3Fulham
 FTTottenham H.1 - 0Sunderland
 FTWest Bromwich A.5 - 5Manchester U.
 FTWest Ham U.4 - 2Reading
 FTWigan Athletic2 - 2Aston Villa

BABA WA NEYMAE ASISITIZA MWANAE KUBAKI BRAZIL MAPAKA 2014

BABA wa mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Brazil na klabu ya Santos, Neymar kwa mara nyingine amesisitiza kuwa mwanae atabakia nchini Brazil mpaka kipindi cha majira ya kiangazi 2014. Kumekuwa na tetesi nyingi kuhusu nyota huyo kutimkia klabu ya Barcelona katika kipindi cha miezi michache ijayo huku kocha wake Tito Vilanova akithibitisha kuwa mazungumzo baina ya pande hizo mbili yamefanyika. Hata hivyo baba yake Neymar amesisitiza kuwa mwanae amepanga kumaliza mkataba wake na Santos akidai kuwa kama Barcelona na Real Madrid zina mpango ya kumsajili nyota huyo basi hawana budi kusogeza mipango yao mwakani. Mzee huyo amesema mipango iliyopo ni kuona mwanae anamaliza mkataba na Santos na kama klabu hiyo ikiamua kumuuza kabla ya mkataba wake kumaliza basi wanapaswa kutoa taarifa kabla ili aweze kuzungumza na mwanae kama yuko tayari kwenda Ulaya.

ROY AKERWA NA CHELSEA, MAN CITY VS TOTTENHAM KWENA MAREKANI.

Meneja wa England ROY HODGSON amekerwa na kitendo cha uamuzi wa Klabu za Chelsea, Manchester City na Tottenham kusafiri kwenda ya nje ya Nchi kucheza Michezo ya Kirafiki wakati ndio kwanza Msimu umemalizika.

Klabu hizi 3 zitasafiri n kuelekea Marekani kuumana  zenyewe kwa wenyewe katika Mechimbili za kirafiki huku Tottenham wakitua Visiwa vya Bahamas kucheza na Jamaica.
ZIARA:
Mei 23: Man City v Chelsea [St Louis]
Mei 25: Chelsea v Man City [New York]
Mei 23: Tottenham v Jamaica [Thomas A. Robinson National Stadium, Nassau Paradise Island, Bahamas]
England nayo inatarajiwa kucheza na Republic of Ireland, Uwanjani Wembley hapo Mei 29 na kisha kuruka kwenda Brazil kucheza Uwanja wa Maracana Jijini Rio De Janeiro na Brazil hapo Juni 2.
Kikosi cha Hodgson alichokiteua kuiwakilisha England katika Mechi hizo mbili kina Wachezaji wanane toka Timu hizo tatu.
Chelsea inasemekana imekubali kuwaruhusu Frank Lampard, Ashley Cole na Gary Cahill kuondoka baada ya Mechi yao ya kwanza ya Tarehe 23 na Man City ili kurudi London kujiunga na England.
Lakini Hodgson amesema wao walipanga Mechi zao za Kimataifa kwa makusudi ili kuwapa Wachezaji wote mapumziko ya Wiki moja baada ya Msimu wa Klabu zao kumalizika kisha kuwachukua wao kwa Wiki moja na baada ya hapo kuwaachia kwenda Vakesheni zao kabla kurudi Klabuni kwao kwa matayarisho ya Msimu mpya wa 2013/14.
Hogson amesema Ziara hizo za Klabu zitawafanya wasafiri safari ndefu kuvuka Bahari ya Atlantic na kurudi tena na hilo halitasaidia matayarisho yao.
Akimalizia Hodgson alisema: “Hii ndio hali ambayo tumejikuta tunayo na hatuwezi kulazimisha Klabu nini wafanye.”
KIKOSI KAMILI:
MAKIPA: Ben Foster, Joe Hart, Alex McCarthy.
MABEKI: Leighton Baines, Gary Cahill, Ashley Cole, Phil Jagielka, Glen Johnson, Phil Jones, Joleon Lescott, Kyle Walker.
VIUNGO: Michael Carrick, Tom Cleverley, Frank Lampard, James Milner, Alex Oxlade-Chamberlain, Theo Walcott.
MAFOWADI: Andy Carroll, Jermain Defoe, Wayne Rooney, Daniel Sturridge, Danny Welbeck.

PAMBANO LA SIMBA, YANGA LAINGIZA MIL 500/-

Pambalo la watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0 limeingiza sh. 500,390,000.

Mechi hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.

Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.

Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,708,415.12.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)