Kiungo mahiri wa
kimataifa wa Brazil, Luiz Gustavo anatarajiwa kukubali uhamisho wake
kwenda Arsenal ili aweze kucheza zaidi katika kikosi cha kwanza kwa
ajili ya michuano ya Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil. Kiungo
huyo mkabaji wa Bayern Munich ambaye amejikuta akishindwa kupata namba
ya moja kwa moja katika kikosi cha kwanza anakaribia kukamilisha usajili
wake wa paundi milioni 14 kwenda Emirates wiki hii. Gustavo
anaamini kuwa nafasi yake itazidi kuwa finyu chini ya kocha mpya Pep
Guardiola ambaye ameonyesha kumtumia sasa Javi Martinez ambaye naye
anacheza nafasi hiyo ndio maana anaona uhamisho wake kwenda Arsenal
unaweza kumsadia. Akihojiwa
jijini Basel kabla ya mchezo wa kirafikiwa kimataifa baina ya Brazil na
Switzerland kesho, Gustavo amesema mkataba wake na Bayern unamalizika
2015 lakini ni muhimu kwake kucheza katika kikosi cha kwanza ili aweze
kuitwa katika timu ya taifa.
Tuesday, August 13, 2013
NASRI AOMBA RADHI KUHUSU TABIA YAKE YA LAKINI ASEMA HAJAUWA MTU
Kiungo nyota wa
kimataifa wa Ufaransa, Samir Nasri ameomba radhi kwa tabia yake lakini
amesisitiza kuwa hajaua mtu hivyo anapaswa kupewa nafasi nyingine ya
kujirekebisha. Kiungo
huyo anayecheza katika klabu ya Manchester City alifungiwa mechi tatu
na Shirikisho la Soka la Ufaransa kufuatia kumtukana mwandishi katika
michuano ya Ulaya 2012 na hajaitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya
nchi hiyo toka kipindi hiko. Hatahivyo
Nasri sasa yuko tayari kurejea katika mchezo wa kirafiki kati ya
Ufaransa na Ubelgiji baada ya kocha Didier Deschamps kuridhishwa na
tabia ya mchezaji huyo. Nasri
mwenye umri wa miaka 26 aliomba radhi kwa tukio alilofanya katika
michuano hiyo mwaka jana na kudai kuwa angetakiwa kukabiliana na tatizo
hilo kwa weledi zaidi kuliko alivyofanya. Nyota
aliendelea kudai kuwa anashukuru kupewa nafasi nyingine ya
kujirekebisha na ana mategemeo yaliyotokea hayatajirudia kwasababu hivi
sasa anajua jinsi gani ya kumudu hasira zake tofauti na ilivyokuwa
kipindi cha nyuma.
KAMATI KUTANGAZA MCHAKATO WA UCHAGUZI TFF

Mwenyekiti
wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Hamidu Mbwezeleni atakutana na Waaandishi
wa Habari kwenye ofisi za TFF saa 6 kamili mchana ambapo mbali ya
mchakato utakavyokuwa anatarajia kutangaza tarehe mpya ya uchaguzi huo
ambao awali ulitarajiwa kufanyika Septemba 29 mwaka huu.
Kamati
ya Uchaguzi ya TFF ilikutana Jumapili (Agosti 11 mwaka huu) na
inatarajia kuwa na kikao kingine leo (Agosti 12 mwaka huu) ambapo pamoja
na mambo mengine itazungumzia maandalizi ya uchaguzi huo.
Mbali
ya Mbwezeleni, wajumbe wengine wa Kamati hiyo ni Moses Karuwa (Makamu
Mwenyekiti), Mohamed Sinani, Chabanga Dyamwale na Kitwana Manara.
MAGORI, LINA WAINGIA KAMATI ZA CAF
Watanzania
Crescentius Magori na Lina Kessy wameteuliwa kuwa wajumbe kwenye kamati
ndogondogo (standing committees) mpya za Shirikisho la Mpira wa Miguu
Afrika (CAF) zilizotangazwa juzi na Katibu Mkuu wa shirikisho hilo
Hicham El Amrani.
Magori
na Lina ambao ni wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF watakuwa kwenye
kamati hizo kwa kipindi cha miaka miwili (2013-2015). Magori ameteuliwa
kuwa mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mashindano ya Mpira wa Miguu wa
Ufukweni (Beach Soccer) wakati Lina ameingia kwenye Kamati ya Maandalizi
ya Mpira wa Miguu kwa Wanawake.
Makamu
wa Rais wa TFF, Athuman Nyamlani ameteuliwa tena kuwemo kwenye Bodi ya
Rufani ya CAF yenye wajumbe 12 kwa kipindi kingine cha miaka miwili.
Nyamlani alikuwepo kwenye bodi iliyopita, na itaendelea kuwa chini ya
uenyekiti wa Prosper Abega kutoka Cameroon.
Rais
wa TFF, Leodegar Tenga ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya
CAF yuko kwenye kamati tano za Shirikisho hilo. Kamati hizo ni Kamati ya
Fedha ambayo ni Makamu Mwenyekiti na Kamati ya Maandalizi ya Fainali za
Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN).
Kamati
nyingine ni Kamati ya Masoko na Televisheni ambayo ni Mwenyekiti,
Kamati ya Ufundi na Maendeleo, na Kamati ya Ushauri na Vyama Wanachama
wa CAF.
KAMATI YA SHERIA KUPITIA USAJILI
Kamati
ya Sheria na Hadhi za Wachezaji chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa
inakutana leo jioni (Agosti 13 mwaka huu) na kesho (Agosti 14 mwaka
huu) kupitia na kufanyia uamuzi usajili wa wachezaji wenye matatizo.
Hatua
ya kwanza ya usajili imeshamalizika wakati hatua ya pili ya usajili
inaanza kesho (Agosti 14 mwaka huu) ikihusisha wachezaji ambao watakuwa
hawajasajiliwa katika Ligi Kuu ya Vodacom msimu huu na wale kutoka nje
ya Tanzania.
Hivyo,
dirisha la uhamisho kwa wachezaji wa kimataifa litafungwa baada ya
hatua ya pili ya usajili kumalizika Agosti 29 mwaka huu.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Subscribe to:
Posts (Atom)