Sunday, December 7, 2014

MOURINHO AWALAUMU VIJANA WAOKOTA MIPIRA KWA KIPIGO CHA JANA

Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amelalama kuhusu upotezaji wa wakati baada ya timu yake kufungwa kwa mara ya kwanza katika msimu huu ugani Newcastle.
Mabao mawili ya Papis Cisse yaliiweka Newcastle kifua Mbele lakini baadaye mshambuliaji Didier Drogba akifungia Chelsea lakini bao hilo halikutosha.
''Kuna mambo ambayo yalikuwa yakifanyika bila refa kuona.Hawezi kumwaadhibu kijana wa kubeba mpira ambaye alitoweka ghafla,ama mashabiki ambao wakipata mpira wanakaa nao ama hata kuutupa uwanjani wakati mechi inaendelea''.,alisema Mourinho.
Kilabu ya Newcastle iliona mlinzi wake Steven Taylor akionyeshwa kadi nyekundu wakati ambao Newcastle ilikuwa juu kwa mabao 2-0 lakini wakaendelea na kuvunja rekodi ya Chelsea ya kutofungwa msimu huu.

RAIS JAKAYA KIKWETE APIGA TIZI MARA TATU KWA SIKU KUIMARISHA AFYA YAKE


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifanya mazoezi leo katika viwanja vya Ikulu kufuatia ushauri wa madaktari waliomtaka afanye hivyo mara tatu kwa siku ili kuendelea kuimarisha afya yake baada ya kufanyiwa upasuaji mwezi uliopita katika hospitali ya Johns Hopkins nchini Marekani

DIAMOND AWASILI WASHINGTON, DC TAYARI KWA SHOW YA SHEREHE YA UHURU


 Diamond akiwasili kwenye uwanja wa kimataifa wa Dulles muda huu tayari kwa makamuzi ya sherehe ya Uhuru itayofanyika muda si mrefu Sheraton, ya Downtown Silver Spring, Maryland.
 Diamond akimsalimia mwenyeji wake hayupo pichani mara tu alipowasili Dulles.

















 Kutoka kushoto ni Dj Romy Jones, Diamond na mmoja wa waratibu wa sherehe ya Uhuru Bwn. Phanuel Ligate