KOCHA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amemtupia lawama Cristiano Ronaldo kwa kushindwa kwake kunyakuwa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati akiinoa Real Madrid.
Mourinho alijiunga na na Madrid mwaka 2010 baada ya kuisaidia Inter Milan kunyakuw ataji hilo lakini katika msimu mitatu aliyokuwa Santiago bernabeu alishindwa kabisa kupata mafanikio barani Ulaya akiwa ameambulia kuingoza timu hiyo mpaka hatua ya nusu fainali katika kipindi chote hicho.

Akihojiwa Mourinho ametamba kuwa kushinda taji la michuano hiyo mara mbili kama imefanya kazi yake hiyo kuwa ya kipekee.
Mourinho amesema amekuwepo katika nusu fainali kadhaa na baadhi imekuwa ngumu kukubali kushindwa kama goli walilofungwa na Liverpool wakati akiwa na Chelsea mwaka 2005 pamoja matuta ya mwaka 2011 wakati mchezaji wao tegemeo Ronaldo alipokosa penati ya kwanza.