Sunday, November 30, 2014

BENO NJOVU AWASHUKURU WANACHAMA WA CLUB YA YANGA

Katibu Mkuu wa Yanga Beno Njovu ambaye anamalizia muda wake kuitumikia Timu ya yabga amesema anawashukuru wanachama na mashabiki wa klabu hiyo.

Njovu amesema anawashukuru kwa ushirikiano wao kwa kipindi chote alichokuwa Jangwani.

Njovu amesema yanga ni klabu kubwa, changamoto ni nyingi sana. Lakini nawashukuru wanachama na mashabiki kwa ushirikiano wao.

Hata hivyo amesema ataendelea kuwa mwanachama wa Yanga tena mwaminifu. Nimejifunza mengi, lakini sasa ni wakati wa kukabili changamoto nyingine.

Njovu amekuwa mmoja wa makatibu wa Yanga waliofanya vizuri katika kipindi wakiwa madarakani.

Ameamua kutoongeza mkataba baada ya ule aliokuwa nao kwisha muda wake.