Mabingwa wa ligi kuu nchini ufaransa msimu huu Club ya Paris
Saint-Germain-PSG inajiandaa kupambana na klabu ya Real Madrid katika
kumuwania mshambuliaji nyota wa klabu ya Tottenham Hotspurs Gareth Bale
anayekisiwa kuwa na thamani ya paundi milioni 85. Mabingwa
hao wa ligi nchini Ufaransa wanataka kumchukua meneja Spurs Andres
Villas-Boas ili aweze kumshawishi nyota huyo kumfuata kwenda huko. Hatahivyo,
hata kama Villas-Boas akiamua kubakia jijini London, hilo haliwezi
kuzuia nia ya klabu hiyo tajiri nchini Ufaransa kuvunja benki na
kumsajili mchezaji huyo kwa dau kubwa. PSG
imetumia zaidi ya paundi milioni 200 katika usajili wa nyota mbalimbali
kuanzia mwaka 2011 wakati Kampuni ya Michezo inayosimamiwa na familia
ya kifalme ya Qatari ilipoinunua klabu hiyo. Kwasasa
PSG wameshakubali kuwa lazima wavunje rekodi ya usajili kama wanataka
kumng’oa nyota huyo kutoka Tottenham, rekodi ambayo bado inashikiliwa na
Cristiano Ronaldo ambaye Real Madrid walimnunua kwa paundi milioni 80
kutoka Manchester United.
Thursday, June 13, 2013
LAPORTA AMKINGIA KIFUA MKALI WA DUNIA -MESSI

FABREGAS AKANUSHA TUHUMA ZA KUREJEA JIJINI LONDON.
KIUNGO nyota wa klabu ya
Barcelona Cesc Fabregas amekanusha na kutanabaisha kuwa tuhuma za kwamba anataka kurejea jijini London
nchini Uingereza baada ya kukosa namba ya kudumu katika klabu hiyo. Nyota
huyo mwenye umri wa miaka 26, alijiunga na Barcelona mwaka 2011 lakini
Manchester United na klabu yake ya zamani ya Arsenal wanaaminika kutaka
kumchukua mchezaji huyo kutoka Camp Nou. Fabregas
amesema siku zote amekuwa na furaha Barcelona na yoyote anayesema
kwamba anataka kuondoka hamjui na hajawahi kuzungumza nae.
Kiungo huyo ametokea katika shule ya vipaji ya Barcelona akiwa na miaka 10 mpaka 16 alisajiliwa na Arsenal, na ameichezea klabu hiyo mechi 303 kwa kipindi cha miaka nane na kufanikiwa kufunga mabao 57.
Kiungo huyo ametokea katika shule ya vipaji ya Barcelona akiwa na miaka 10 mpaka 16 alisajiliwa na Arsenal, na ameichezea klabu hiyo mechi 303 kwa kipindi cha miaka nane na kufanikiwa kufunga mabao 57.
TIKETI MECHI YA STARS KUANZA KUUZWA KESHO
Wakati
timu ya Ivory Coast inatarajiwa kuwasili leo usiku (Juni 13 mwaka huu)
kwa ndege maalum, tiketi kwa ajili ya mechi kati yake na Taifa Stars
itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa zinaanza kuuzwa kesho
mchana (Juni 14 mwaka huu) kwenye vituo mbalimbali jijini Dar es
Salaam. Vituo
vitakavyotumika kwa mauzo hayo ni Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa,
Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom
Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala na BMM Salon iliyoko
Sinza Madukani. Viingilio
katika mechi hiyo ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika katika
kundi C ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani, sh. 7,000 viti vya
rangi ya bluu, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP C,
sh. 20,000 kwa VIP B wakati VIP A itakuwa sh. 30,000. Pia
viti 100 vilivyo katika sehemu ya Wageni Maalumu (VVIP) vitauzwa kwa
sh. 50,000 kila kimoja. Tiketi hizo zitauzwa katika ofisi za TFF, na
watakaonunua watapewa kadi maalumu zenye majina yao, majina ambayo pia
watayakuta katika vita watakavyokaa. Kwa maana hiyo hakutakuwa pasi
maalumu (free pass) za kuingia VVIP.
PONGEZI KWA RAIS MPYA WA ZFA
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amempongeza Rais mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA), Ravia Idarous Faina aliyechaguliwa katika uchaguzo mdogo uliofanyika hivi karibuni. Amesema ushindi aliopata Faina unaonyesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa ZFA walivyo na imani naye katika kuhakikisha maendeleo ya mpira wa miguu visiwani humo. Rais Tenga amesema ni imani yake kuwa Rais Faina ataendeleza ushirikiano uliopo kati ya TFF na ZFA kwa ajili ya ustawi wa mpira wa miguu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kumtakiwa kila kheri katika wadhifa wake huo mpya.
WAAMUZI WATATU WAFUNGIWA MIEZI MITATU
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limefungia miezi mitatu waamuzi watatu walioshindwa kuchezesha mechi namba 32 ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kati ya Mpwapwa Stars ya Dodoma na Machava FC ya Kilimanjaro iliyokuwa ichezwe Juni 2 mwaka huu Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma. TFF kupitia Kamati yake ya Waamuzi iliyokutana katika kikao chake cha Juni 12 mwaka huu kupitia taarifa mbalimbali za waamuzi wa RCL ilibaini makosa yaliyofanywa na baadhi ya waamuzi na kuyatolea uamuzi. Waamuzi hao waliofungiwa ambao wanatoka mkoani Singida ni Jilili Abdallah, Amani Mwaipaja na Theofil Tegamisho. Wamefungiwa kwa kutoripoti katika kituo walichopangiwa (Uwanja wa Jamhuri, Dodoma) na kutoa taarifa ya uongo kwa kushirikiana na Kamishna wa mechi hiyo. Kanuni iliyotumika kuwafungia ni ya 28 kifungu (d) na (g) ya Ligi za TFF, na adhabu hiyo imeanza Juni 13 mwaka huu. Waamuzi hao pamoja na kamishna badala ya kwenda Uwanja wa Jamhuri, wao walikwenda kwenye Uwanja wa Mgambo ulioko Mpwapwa na kuandika ripoti iliyoonesha kuwa timu ya Machava FC haikufika uwanjani wakati wakijua kuwa mechi hiyo ilitakiwa kuchezwa katika Uwanja wa Jamhuri.
PONGEZI KWA RAIS MPYA WA ZFA
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amempongeza Rais mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA), Ravia Idarous Faina aliyechaguliwa katika uchaguzo mdogo uliofanyika hivi karibuni. Amesema ushindi aliopata Faina unaonyesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa ZFA walivyo na imani naye katika kuhakikisha maendeleo ya mpira wa miguu visiwani humo. Rais Tenga amesema ni imani yake kuwa Rais Faina ataendeleza ushirikiano uliopo kati ya TFF na ZFA kwa ajili ya ustawi wa mpira wa miguu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kumtakiwa kila kheri katika wadhifa wake huo mpya.
WAAMUZI WATATU WAFUNGIWA MIEZI MITATU
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limefungia miezi mitatu waamuzi watatu walioshindwa kuchezesha mechi namba 32 ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kati ya Mpwapwa Stars ya Dodoma na Machava FC ya Kilimanjaro iliyokuwa ichezwe Juni 2 mwaka huu Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma. TFF kupitia Kamati yake ya Waamuzi iliyokutana katika kikao chake cha Juni 12 mwaka huu kupitia taarifa mbalimbali za waamuzi wa RCL ilibaini makosa yaliyofanywa na baadhi ya waamuzi na kuyatolea uamuzi. Waamuzi hao waliofungiwa ambao wanatoka mkoani Singida ni Jilili Abdallah, Amani Mwaipaja na Theofil Tegamisho. Wamefungiwa kwa kutoripoti katika kituo walichopangiwa (Uwanja wa Jamhuri, Dodoma) na kutoa taarifa ya uongo kwa kushirikiana na Kamishna wa mechi hiyo. Kanuni iliyotumika kuwafungia ni ya 28 kifungu (d) na (g) ya Ligi za TFF, na adhabu hiyo imeanza Juni 13 mwaka huu. Waamuzi hao pamoja na kamishna badala ya kwenda Uwanja wa Jamhuri, wao walikwenda kwenye Uwanja wa Mgambo ulioko Mpwapwa na kuandika ripoti iliyoonesha kuwa timu ya Machava FC haikufika uwanjani wakati wakijua kuwa mechi hiyo ilitakiwa kuchezwa katika Uwanja wa Jamhuri.
TAFAKARI YA LEO BARCA ILIVYOFANYA JEURI KUMTAFUTIA MESSI COMBINATION JE KWA NEYMA ITAKUWAJEEEE??

Hivyo kuwasili kwa mshambuliaji
wa Santos na timu ya taifa ya Hispania, Neymar,
katika kikosi cha Barcelona, inamaanisha kuwa Barcelona imeendelea kutumia
fedha nyingi kusaka mshambuliaji ambaye anaweza kung’ara vyema kwa pamoja na
staa wao, Lionel Messi.
Katika kipindi cha miaka
mitano iliyopita, Barcelona imetumia jumla ya Euro 205 milioni kwa ajili ya
kusaka mshambuliaji ambaye anaweza kumpunguzia Messi mzigo wa ustaa alioubeba
kwa muda mrefu klabuni hapo.
Thierry
Henry
Katika msimu wake wa
kwanza tu ndipo Henry alifikia matarajio ya mashabiki wa Barcelona. Baadaye
kuibuka kwa kinda wa Kihispaniola, Pedro Rodriguez, kulimfanya Henry apate
nafasi finyu ya kucheza katika kikosi cha kwanza na mwisho aliamua kutimkia
Marekani katika klabu ya New York Bulls.
Hata hivyo Henry
hakufikia kiwango alichokuwanacho wakati anachezea Arsenal chini ya Arsene
Wenger ingawa katika kipindi chake na Barcelona alishinda mataji kadhaa.
Zlatan
Ibrahimovich
Ukitazama hapa katika
hali ya kawaida kilikuwa kipindi kibaya katika harakati za maisha ya soka ya
Ibrahimovich. Tofauti na matarajio ya wengi, licha ya kusajiliwa kwa Euro 46
milioni huku pia Barcelona wakimtoa Samuel Eto’o kwenda Inter Milan, bado
Ibrahimovich hakutamba sana Nou Camp.
Mwishowe alijikuta
akiingia katika mgogoro mkubwa na kocha wa wakati huo, Pep Guardiola.
Ibrahimovich alimshutumu Guardiola kwamba alikuwa anampendelea zaidi Messi huku
wakati mwingine akimchezesha nafasi ya kati wakati yeye yuko benchi.
Baada ya msimu mmoja tu,
Zlatan aliondoka akarudi Italia ambako alijiunga na AC Milan.
David
Villa
Alionekana mmoja kati ya
wachezaji ambao wangeweza kumpunguzia mzigo wa mabao staa huyu wa Argentina.
Alianza vema, lakini baadaye aliumia katika michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia,
ilikuwa Desemba 2011.
Mbali na hilo tangu hapo
kasi yake imepungua uwanjani na sasa inasemekana ataondoka zake Barcelona
katika kipindi hiki cha uhamisho wa wachezaji.
LIONEL MESSI NA MZAZI WAKE WA KIUME WAINGIA MATATANI.

Mchezaji huyo kutoka Argentina na
babake, Jorge wanatuhumiwa kuibia serikali ya nchi hiyo, kwa kujaza fomu
zisizokuwa za ukweli za marejesho ya kodi kati ya mwaka wa 2007 na 2009.Hata hivyo
mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 hajasema lolote kuhusiana na madai hayo.
Messi hulipwa Euro milioni
kumi na sita kila mwaka na ndiye mchezaji anayelipwa kiasi cha juu zaidi
duniani.Lakini mwendesha mashtaka Raquel Amado, aliwasilisha nyaraka za
mahakama nyumbani kwa mchezaji huyo katika mtaa wa kifahari wa Gava mjini
Barcelona.
Jaji mjini humo ni sharti waidhinisha
malalamishi dhidi ya mshukiwa yeyote kabla hajafunguliwa mashtaka.Messi na
babake wanashukiwa kutumia kampuni katika mataifa ya ng’ambo, mjini Belize na
Uruguay kuuza haki za kutumia picha ya mchezaji huyo.
Mchezaji huyo na babake wanatuhumiwa
kutumia kampuni hizo zilizoko nje ya Hispania, ambako anaishi na kucheza soka
ya kulipwa, kukwepa kulipa kodi inayokisiwa kuwa paundi milioni tatu na nusu.
MASCHERANO AOMBA RADHI KUMPIGA TEKE DAKTARI WA TIMU:
KIUNGO nyota wa Club ya Barcelona na timu ya taifa ya Argentina Javier Mascherano ameomba radhi baada ya kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kosa la kumpiga teke daktari wakati wa mechi ya kufuzu michuano ya Kombe la Dunia kati ya timu ya taifa ya nchi yake na Ecuador.
Kiungo huyo ambaye kucheza katika vilabu vya Liverpool na West Ham United alitolewa baada ya kumpiga teke dereva wa gari maalumu la kubebea wachezaji walioumia dakika ya 87 ya mchezo huo.
Nyota huyo ambayo alikuwa nahodha katika mchezo huo aliomba radhi kwa tukio hilo na kudai kuwa alimuonya dereva kwa kwenda kasi mpaka kutaka kumdondosha ingawa amedai alichokifanya hakikubaliki.
Katika mchezo huo Argentina ilitoka sare ya bao 1-1 dhidi Ecuador na kuendelea kubakia kileleni wakiwa na alama 27 wakifuatiwa na Colombia waliopo nafasi ya pili wakiwa na alama 26 huku Ecuador wakibakia nafasi ya tatu wakiwa na alama 22.
ESSIEN ASEMA NIPOM TAYARI KUCHEZA NAFASI YOYOTE UWANJANI:
KIUNGO nyota wa Chelsea na timu ya Taifa ya Ghana Michael Essien amesema kuwa amejiandaa kucheza nafasi yoyote chini ya kocha mpya wa klabu hiyo Jose Mourinho. Kiungo huyo wa kimataifa wa Ghana alikuwa akipewa nafasi kidogo ya kucheza chini Roberto Di Matteo baada kusumbuliwa na majeraha ya mguu lakini alipata ahueni wakati Mourinho alipomwita kwa mkopo wakati akifundisha Real Madrid. Mourinho amekuwa akimchezesha Essien kama beki au kiungo wakati akiwa Santiago Bernabeu na sasa yuko tayari kucheza nafasi yoyote ambayo Mreno huyo atamchezesha. Essien mwenye umri wamiaka 30 alisajiliwa na Mourinho wakati akiwa Chelsea mwaka 2005 kwa ada ya paundi milioni 29 akitokea klabu ya Lyon ya Ufaransa.
Subscribe to:
Posts (Atom)