Wednesday, May 28, 2014

KUELEKEA MSIMU MPYA WA LIGI VP TIMU ZILIZO KAMILISHA USAJILI MPAKA SASA.


Katika harakati za kuelekea msimu mpya wa ligi kuu Vodacom Tanzania bara timu mbalimbali tayari zimekwisha anza kufanya usajili wa hapa na pale
Tukianza na Wagomga Nyundo wa jiji la mbeya Timu ya Mbeya City kutoka Mkoani Mbeya, tayari imekamilisha usajili wa
Mshambuliaji kutoka Timu ya Kagera Sugar Themi Felix na Kiungo Peter Mwalianzi kutoka timu ya JKT Mgambo.
Safu ya Ushambuliaji ya Timu hiyo iliyofanikiwa kushika Nafasi ya Tatu kwenye Ligi Kuu Vodacom, VPL, Msimu huu, itakuwa sasa na Paul Nonga, Mwagane Yeya, Saad Kipanga na Themi Felix kuanzia msimu ujao na huku Peter Mwalianzi akiongeza nguvu kwenye safu ya Kiungo inayoongozwa na Steven Mazanda.

Tuwatazame Mabingwa wapya wa VPL, Azam FC, tayari walishakamilisha usajili wa Frank Domayo na Didier Kavumbagu kutoka Yanga na kumuongeza Beki Abdallah Heri kutoka Klabu ya Zimamoto ya kule Zanzibar.
Hivyo basi kwa sasa safu ya Kiungo ya Mabingwa hao itaundwa na Hi
mid Mao, Kipre Balou, Salumu Abubakary na Domayo Frank huku Brian Umony, Gaudence Mwaikimba, John Bocco, Kipre TcheTche na Kavumbagu wakikamilisha Safu ya Ushambuliaji.

Nao Timu ya Ruvu Shooting iliyomaliza Msimu kwenye Nafasi ya Tano baada ya kupata Alama 38, tayari imekamilisha usajili wa Zuberi Dabi kutoka Klabu ya Kagera Sugar. Timu hiyo pia imefanikiwa kumsajili Chagu Chagula mshambuliaji Raia wa Tanzania ambaye amecheza sana Nchini Burundi.
Kwa upande wa Wagosi wa Kaya Baada ya kuandaa mkakati na kuachana na Wachezaji wanaotemwa na Timu za Simba na Yanga, Klabu ya Coastal Union ya Tanga tayari imekamilisha usajili wa Bright Obina ambaye aliwahi kuzichezea African Lyon na Ashanti United zote za Dar es Salaam.
Timu hiyo pia imefanikiwa kumnasa Hussein Swed ambaye Msimu uliopita alikuwa na Timu iliyoshuka Daraja ya Ashanti United na sasa wote wametua kwa Wagosi wa Kaya.
Kwa upande wa Simba wekundu msimbazi mpaka sasa bado hawaja weka hadharani majina wachezaji waliowasajili licha ya kuwa na taarifa za kuwa bado wapo katika harakati za kufanya usajili na upo uwezakoano kutwaa wachezaji kutoka kadhaa kutoka nje ya boda Uganda au Kenya ili kuweza kuimarisha kikosi hicho ambacho kwa sasa kipo katika harakati za uchaguziwa viongozi unaotaraji kufanyika Juni 29 mwaka huu.
Yanga nao washindi wa pili wa ligi kuu msimu uliopita tayari wamefanikisha kumnasa Kiungo Omega Seme aliyekuwa kwa Mkopo kwa Wajelajela Tanzania Prison pamoja na kafinikisha kumbakisha Beki Kisiki Mbuyu Twite Baada ya Kuondoka kwa aliye kuwa kiungo chumvi Frank Domayo pamoja na Mshambuliaji Didier Kavumbagu.
Kwa mujibu wa TFF, Usajili wa Wachezaji kwa hatua ya kwanza Msimu mpya wa 2014/2015 unaanza Juni 15 hadi Agosti 3 Mwaka huu wakati Kipindi cha kutangaza Wachezaji walioachwa au kusitishiwa Mikataba ni kuanzia Juni 15 hadi 30.
Kipindi cha kwanza cha Uhamisho wa Wachezaji ni kuanzia Juni 15 hadi Julai 30.
Kupitia Majina na kutangaza pingamizi ni kati ya Agosti 4 na 11 na kuthibitisha Usajili hatua ya awali ni Agosti 12 hadi 14.
Usajili hatua ya pili utakuwa kati ya Agosti 14 na 29 wakati kupitia na kutangaza Majina ya pingamizi hatua ya pili ya usajili ni kuanzia Agosti 30 hadi Septemba 4. Uthibitisho wa Usajili hatua ya pili ni Septemba 5 na 6.
Ligi Kuu ya Vodacom, VPL, inatarajiwa kuanza Agosti 24 na Ratiba inatarajiwa kutoka Mwezi mmoja kabla hapo Julai 24.