Katika harakati za kuelekea msimu mpya wa ligi kuu Vodacom Tanzania bara timu mbalimbali tayari zimekwisha anza kufanya usajili wa hapa na pale
Safu ya Ushambuliaji ya Timu hiyo
iliyofanikiwa kushika Nafasi ya Tatu kwenye Ligi Kuu Vodacom, VPL, Msimu huu,
itakuwa sasa na Paul Nonga, Mwagane Yeya, Saad Kipanga na Themi Felix kuanzia
msimu ujao na huku Peter Mwalianzi akiongeza nguvu kwenye safu ya Kiungo
inayoongozwa na Steven Mazanda.
Tuwatazame Mabingwa wapya wa VPL,
Azam FC, tayari walishakamilisha usajili wa Frank Domayo na Didier Kavumbagu
kutoka Yanga na kumuongeza Beki Abdallah Heri kutoka Klabu ya Zimamoto ya kule
Zanzibar.
mid Mao, Kipre Balou, Salumu Abubakary na Domayo
Frank huku Brian Umony, Gaudence Mwaikimba, John Bocco, Kipre TcheTche na
Kavumbagu wakikamilisha Safu ya Ushambuliaji.
Kwa
upande wa Wagosi wa Kaya Baada ya kuandaa mkakati na kuachana na Wachezaji
wanaotemwa na Timu za Simba na Yanga, Klabu ya Coastal Union ya Tanga tayari
imekamilisha usajili wa Bright Obina ambaye aliwahi kuzichezea African Lyon na
Ashanti United zote za Dar es Salaam.
Timu
hiyo pia imefanikiwa kumnasa Hussein Swed ambaye Msimu uliopita alikuwa na Timu
iliyoshuka Daraja ya Ashanti United na sasa wote wametua kwa Wagosi wa Kaya.
Kwa upande wa Simba
wekundu msimbazi mpaka sasa bado hawaja weka hadharani majina wachezaji
waliowasajili licha ya kuwa na taarifa za kuwa bado wapo katika harakati za
kufanya usajili na upo uwezakoano kutwaa wachezaji kutoka kadhaa kutoka nje ya
boda Uganda au Kenya ili kuweza kuimarisha kikosi hicho ambacho kwa sasa kipo
katika harakati za uchaguziwa viongozi unaotaraji kufanyika Juni 29 mwaka huu.
Kwa
mujibu wa TFF, Usajili wa Wachezaji kwa hatua ya kwanza Msimu mpya wa 2014/2015
unaanza Juni 15 hadi Agosti 3 Mwaka huu wakati Kipindi cha kutangaza Wachezaji
walioachwa au kusitishiwa Mikataba ni kuanzia Juni 15 hadi 30.
Kipindi
cha kwanza cha Uhamisho wa Wachezaji ni kuanzia Juni 15 hadi Julai 30.
Kupitia
Majina na kutangaza pingamizi ni kati ya Agosti 4 na 11 na kuthibitisha Usajili
hatua ya awali ni Agosti 12 hadi 14.
Usajili
hatua ya pili utakuwa kati ya Agosti 14 na 29 wakati kupitia na kutangaza
Majina ya pingamizi hatua ya pili ya usajili ni kuanzia Agosti 30 hadi Septemba
4. Uthibitisho wa Usajili hatua ya pili ni Septemba 5 na 6.
Ligi
Kuu ya Vodacom, VPL, inatarajiwa kuanza Agosti 24 na Ratiba inatarajiwa kutoka
Mwezi mmoja kabla hapo Julai 24.