Friday, July 18, 2014
SIO NDOKI NG"O MAN CITY - TOURE NIPO SANA
MALINZI ATOA NENO KUHUSU SUALA LA UPANGAJI MATOKEO.

Malinzi ametoa kauli
hiyo katika futari aliyoandaa jana kwa wadau mbalimbali wa michezo
kikiwemo kikosi cha timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17,
Serengeti Boys katika ofisi za shirikisho hilo, Dar es Salaam. Malinzi
amesema ana uhakika kuwa balaa hilo la upangaji mechi za kimataifa
limeingia Afrika huku wanaofanya shughuli hizo wakiwashawishi viongozi,
makocha na hata wachezaji ili matokeo yapatikane wanavyotaka
wao.
Malinzi amesema sio suala la kuficha tena kuhusu janga hilo na
kuwaomba wadau na viongozi wa dini waliokuwepo katika shughuli hiyo
kuungana ili kuwakemea vijana wao kuhusu suala hilo. Mojawapo ya
viongozi mbalimbali waliohudhuria shughuli hiyo ni pamoja na Mstahiki
Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Slaa, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es
Salaam Ramadhani Madabida, Katibu Mkuu wa zamani wa TFF enzi hizo
ikiitwa FAT Said El Maamry na viongozi mbalimbali wa timu za Ligi Kuu na
Ligi Daraja la kwanza Tanzania bara.
WIKIENDI BURUDANI MWANZO MWISHO AFCON 2015-MOROCCO
RATIBA
[Saa za Bongo]
Jumamosi Julai 19
16:00 Uganda v Mauritania
16:30 Botswana v Guinea-Bissau
19:30 Sierra Leone v Seychelles
Jumapili Julai 20
16:00 Lesotho v Kenya
16:00 Tanzania v Mozambique
17:30 Congo v Rwanda
18:00 Benin v Malawi
MAKUNDI:
KUNDI A
-Nigeria
-South Africa
-Sudan
-Mshindi Congo/Rwanda
KUNDI B
-Mali
-Algeria
-Ethiopia
Mshindi Benin/Malawi
KUNDI C
-Burkina Faso
-Angola
-Gabon
-Mshindi Lesotho/Kenya
KUNDI D
-Ivory Coast
-Cameroun
-Congo DR
-Mshindi Sierra Leone/Seychelles
KUNDI E
-Ghana
-Togo
-Guinea
Mshindi Uganda/Mauritania
KUNDI F
-Zambia
-Cape Verde
-Niger
-Mshindi Tanzania/Msumbiji
KUNDI G
-Tunisia
-Egypt
-Senegal
-Mshindi Botswana/Guinea-Bissau
Jumamosi Julai 19
16:00 Uganda v Mauritania
16:30 Botswana v Guinea-Bissau
19:30 Sierra Leone v Seychelles
Jumapili Julai 20
16:00 Lesotho v Kenya
16:00 Tanzania v Mozambique
17:30 Congo v Rwanda
18:00 Benin v Malawi
MAKUNDI:
KUNDI A
-Nigeria
-South Africa
-Sudan
-Mshindi Congo/Rwanda
KUNDI B
-Mali
-Algeria
-Ethiopia
Mshindi Benin/Malawi
KUNDI C
-Burkina Faso
-Angola
-Gabon
-Mshindi Lesotho/Kenya
-Ivory Coast
-Cameroun
-Congo DR
-Mshindi Sierra Leone/Seychelles
KUNDI E
-Ghana
-Togo
-Guinea
Mshindi Uganda/Mauritania
KUNDI F
-Zambia
-Cape Verde
-Niger
-Mshindi Tanzania/Msumbiji
KUNDI G
-Tunisia
-Egypt
-Senegal
-Mshindi Botswana/Guinea-Bissau
UEFA YAWEKA HADHARANI MAJINA 10 KUWANIA MCHEZAJI BORA ULAYA!
Katika kuelekea katika michuano ya Uefa champions Ligi Jana UEFA imetoa Majina ya wanandinga 10 Wanao gombea Tuzo yao ya Mchezaji Bora wa
Mwaka na Mshindi atatangazwa hapo Agosti 28 wakati wa Droo ya Makundi ya
UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Awali Majina ya Wachezaji 35 yalipigiwa Kura na hao 10 ndio kuibuka kidedea.
Lakini Majina hayo 10 yatachujwa kwa Kura hapo Agosti 14 na kubakisha
Majina Matatu yatakayopigiwa Kura na kutangazwa Mshindi hapo Agosti 28.
WASHINDI WALIOPITA:
2010–11 Lionel Messi [Barcelona]
2011–12 Andrés Iniesta [Barcelona]
2012–13 Franck Ribéry [Bayern Munich]
Wapigaji Kura ya Tuzo hii ni Jopo la Wanahabari maalum toka Nchi zote Wanachama wa UEFA.
Miongoni mwa Majina makubwa ambayo hayamo kwenye Listi hii ya Wachezaji 10 ni yale ya Zlatan Ibrahimovic, Gareth Bale na Neymar.

Bila kustajabisha, Lionel Messi na Cristiano Ronaldo, ni miongoni mwa Wagombea.
Tuzo hii ilianzisha na UEFA Mwaka 2011 ili kuziba pengo la Ballon
d'Or ambayo iliunganishwa na Tuzo ya FIFA ya Mchezaji Bora Duniani na
pia kuibadili ile Tuzo ya zamani ya UEFA ya Mchezaji Bora wa Mwaka kwa
Klabu.
LISTI YA WAGOMBEA 10:
-Diego Costa [Spain, Atletico Madrid]
-Angel Di Maria [Argentna, Real Madrid]
-James Rodriguez [Colombia, AS Monaco]
-Luis Suarez [Liverpool (Sasa Barcelona), Uruguay]
-Philipp Lahm [Germany, Bayern Munich]
-Thomas Muller [Germany, Bayern Munich]
-Manuel Neuer [Germany, Bayern, Munich]
-Arjen Robben [Germany, Bayern Munich]
-Cristiano Ronaldo [Portugal, Real Madrid]
-Lionel Messi [Argentina, Barcelona]
KIINGILIO MECHI YA STARS, MSUMBIJI 7,000/- VITI MAALUM (VIP) 30,000/-
Viingilio kwa mechi ya Taifa Stars na Msumbiji itakayochezwa keshokutwa (Jumapili) Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ni sh. 7,000 na sh. 30,000 kwa viti maalumu 4,500 tu.
Kuanzia kesho asubuhi (Jumamosi) tiketi za kielektroniki zitauzwa pia katika magari maalumu kwenye vituo vya Buguruni Shell, Dar Live Mbagala, Ferry Magogoni, Kigamboni, OilCom Chang’ombe, OilCom Ubungo, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa (Kariakoo), TCC Club Chang’ombe na Uwanja wa Taifa.
Aidha tiketi zinapatikana kupitia M-PESA kwa kupiga *150*00# kisha
bonyeza 4, bonyeza tena 4 kisha weka namba ya kampuni 173399 kisha
ingiza 7000 kama namba ya kumbukumbu ya malipo, kisha andika tena 7000
kwenye weka kiasi, kasha weka namba ya siri na baadaye bonyeza 1
kukubali.
Utapokea ujumbe wenye orodha ya vituo vya MaxMalipo vya kuchukua tiketi ukiwa na namba ya uhakiki wa malipo yako.
Vituo vya MaxMalipo vya kuchukulia tiketi ni mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa Samora/Ohio, maduka makubwa ya Uchumi Supermarket (Quality Centre, Tabata Segerea na kituo cha daladala Makumbusho), Sheer Illussions (Millennium Tower na Mlimani City), maduka makubwa ya TSN Supermarket (City Centre, Kibo Tegeta na Upanga).
Vodashop (Ubungo na Mill Pamba), Shop Mwenge (Born to Shine), Puma Petrol Station (Mwenge na Uwanja wa Ndege), Engen Petrol Station (Mbezi Beach), Big Bon Petrol Station (Kariakoo, Sinza Mori, Mbagala na Temeke), YMCA (Posta Mpya), City Sports Lounge (Posta), Uwanja wa Taifa) na Uwanja wa Karume.

SEMINA ELEKEZI AIRTEL RISING STARS
Semina elekezi ya michuano ya Airtel Rising Stars kwa mikoa sita inafanyika kesho (Julai 19 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Washiriki wa semina hiyo ni kutoka mikoa ya Mbeya (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Mwanza (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Morogoro (Katibu), Ilala (Katibu na mwakilishi wa wanawake).
Temeke (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Kinondoni (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Dar es Salaam (Mwenyekiti na Katibu), na Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) kitakachowakilishwa na mwakilishi wa wanawake.
Washiriki wengine katika semina hiyo ambayo mgeni rasmi atakuwa Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine ni wajumbe wa Kamati ya Mpira wa Miguu wa Vijana ya TFF.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
Kuanzia kesho asubuhi (Jumamosi) tiketi za kielektroniki zitauzwa pia katika magari maalumu kwenye vituo vya Buguruni Shell, Dar Live Mbagala, Ferry Magogoni, Kigamboni, OilCom Chang’ombe, OilCom Ubungo, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa (Kariakoo), TCC Club Chang’ombe na Uwanja wa Taifa.

Utapokea ujumbe wenye orodha ya vituo vya MaxMalipo vya kuchukua tiketi ukiwa na namba ya uhakiki wa malipo yako.
Vituo vya MaxMalipo vya kuchukulia tiketi ni mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa Samora/Ohio, maduka makubwa ya Uchumi Supermarket (Quality Centre, Tabata Segerea na kituo cha daladala Makumbusho), Sheer Illussions (Millennium Tower na Mlimani City), maduka makubwa ya TSN Supermarket (City Centre, Kibo Tegeta na Upanga).
Vodashop (Ubungo na Mill Pamba), Shop Mwenge (Born to Shine), Puma Petrol Station (Mwenge na Uwanja wa Ndege), Engen Petrol Station (Mbezi Beach), Big Bon Petrol Station (Kariakoo, Sinza Mori, Mbagala na Temeke), YMCA (Posta Mpya), City Sports Lounge (Posta), Uwanja wa Taifa) na Uwanja wa Karume.

SEMINA ELEKEZI AIRTEL RISING STARS
Semina elekezi ya michuano ya Airtel Rising Stars kwa mikoa sita inafanyika kesho (Julai 19 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Washiriki wa semina hiyo ni kutoka mikoa ya Mbeya (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Mwanza (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Morogoro (Katibu), Ilala (Katibu na mwakilishi wa wanawake).
Temeke (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Kinondoni (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Dar es Salaam (Mwenyekiti na Katibu), na Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) kitakachowakilishwa na mwakilishi wa wanawake.
Washiriki wengine katika semina hiyo ambayo mgeni rasmi atakuwa Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine ni wajumbe wa Kamati ya Mpira wa Miguu wa Vijana ya TFF.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
Subscribe to:
Posts (Atom)