Thursday, April 25, 2013

TIMU ZA HISPAIN HOI BUNDASLIGA NOMA KWELI KWELI"TAZAMA MAMBO YALIVYOKUWA"

Katika mechi ya usiku  huu mchezaji aliye katika kiwango bora kabisa Robert Lewandowski  yameipa Borussia Dortmund ushindi wa 4-1 dhidi ya Real Madrid katika Nusu Fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya nchini Ujerumani.
Mabao ya mshambuliaji huyo wa Poland yameipa  Dortmund kujiweka katika nafasi nzuri ya kutingaa fainali ya klabu za bundasliga pekee  itakayopigwa Uwanja wa Wembley mwezi ujao, kufuatia jana Bayern Munich kuichapa 4-0 Barcelona nchini Ujerumani pia.
Lewandowski alifunga bao la kwanza dakika ya nane, kabla ya Cristiano Ronaldo kuisawazishia Real dakika ya 43.
Lakini lewandowski akaonyesha makali yake katika kipindi cha pili na kufunga mabao matatu zaidi dakika za 50, 55 na 67 kwa penalti.
Kocha wa Real, Mreno Jose Mourinho ambaye hakutegemea kipigo hicho kitakatifu, sasa real madrid inatakiwa  kutengeneza mipango ya kushinda 3-0 katika mchezo wa marudiano wiki ijayo, ili kuwapiku Dortmund.




UCL-NUSU FAINALI
RATIBA:
MARUDIANO
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
Jumanne Aprili 30
Real Madrid v Borussia Dortmund [1-4]
Jumatano Mei 1
Barcelona v Bayern Munich [0-4]
FAINALI
25 Mei 2013

UWANJA wa WEMBLEY, London.