Friday, May 17, 2013

IFAHAMU KWA UZURI MAN UNITED KATIKA HARAKATI ZA SOKA ULIMWENGUNI

MANCHESTER UNITED
MATAJI VIKOMBE ILIVYOTWAA:
UBINGWA:
LIGI KUU:VPL
1992–93, 1993–94, 1995–96, 1996–97, 1998–99, 1999–2000, 2000–01, 2002–03, 2006–07, 2007–08, 2008–09, 2010–11, 2012–13
DARAJA LA 1:
1907–08, 1910–11, 1951–52, 1955–56, 1956–57, 1964–65, 1966–67
DARAJA LA 2:
1935–36, 1974–75
VIKOMBE:
FA CUP: 11
1908–09, 1947–48, 1962–63, 1976–77, 1982–83, 1984–85, 1989–90, 1993–94, 1995–96, 1998–99, 2003–04
LIGI CUP: 4
1991–92, 2005–06, 2008–09, 2009–10
FA CHARITY/COMMUNITY SHIELD: 19
1908, 1911, 1952, 1956, 1957, 1965, 1967, 1977, 1983, 1990, 1993, 1994, 1996, 1997, 2003, 2007, 2008, 2010, 2011
ULAYA:
EUROPEAN CUP / UEFA CHAMPIONS LEAGUE: 3
1967–68, 1998–99, 2007–08
UEFA CUP WINNERS' CUP: 1
1990–91
EUROPEAN SUPER CUP: 1
1991
DUNIA:
INTERCONTINENTAL CUP: 1
1999
FIFA CLUB WORLD CUP: 1
2008
MATAJI YAKE: SIR FERGUSON-
-PREMIER LEAGUE: 1993, 1994, 1996, 1997, 1999,
2000, 2001, 2003, 2007, 2008, 2009, 2011, 2013.
-FA CUP: 1990, 1994, 1996, 1999, 2004
-LEAGUE CUP: 1992, 2006, 2009, 2010
-UEFA CHAMPIONS LEAGUE: 1999, 2008
-UEFA CUP WINNERS CUP: 1991
-FIFA CLUB WORLD CUP: 2008
-UEFA SUPER CUP: 1992
-FIFA INTER-CONTINENTAL  CUP: 1999
-FA CHARITY/COMMUNITY SHIELD: 1990, 1993, 1994, 1996, 1997, 2003, 2007, 2008, 2010, 2011

Endelea kupata taarifa zaidi kupitia mkali wa dimba tz.blogspot.com ambayo inakuletea makala kamili kuhusu Club hii bora kabisa duniani ya manchester united kaa mkao wa kuburudika kimichezo zaidi karibu wewe mdau wa blog hii>>>>>>>

KOMBE LA DUNIA: DROGBA , YAHAYA TOURE WAWEKWA PEMBEENI

KOCHA WA IVORY COAST Sabri Lamouchi, ametangaza Kikosi chake cha Wachezaji 26 kwa ajili ya Mechi za KUNDI C la kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwaka 2014 watakazocheza Mwezi ujao dhidi ya Gambia na Tanzania na hawamo Maveterani Didier Drogba na Kolo Toure.
Drogba, mwenye Miaka 35 ambae sasa anacheza huko Uturuki na Galatasaray, pia hakuchukuliwa kwenye Kikosi cha Ivory Coast kilichocheza Mechi ya KUNDI C ya Kombe la Dunia Mwezi Machi walipocheza na Gambia.
Hadi sasa Drogba ameichezea Nchi yake Mechi 96 na kufunga Bao 60.
MSIMAMO:
KUNDI C
1 Côte d'Ivoire Mechi 3 Pointi 7
2 Tanzania Mechi 3 Pointi 6
3 Morocco Mechi 3 Pointi 2
4 Gambia Mechi 3 Pointi 1
RATIBA/MATOKEO:
02/06/12: Ivory Coast 2-0 Tanzania; Gambia 1-1 Morocco
08-12/06/12: Morocco 2-2 Ivory Coast; Tanzania 2 Gambia 1
22-26/03/13: Ivory Coast 3 Gambia 0; Tanzania 3 Morocco 1
07-11/06/13: The Gambia v Ivory Coast; Morocco v Tanzania [Juni 8]
14-18/06/13: Tanzania v Ivory Coast; Morocco v The Gambia
06-10/09/13: Ivory Coast v Morocco; Gambia v Tanzania

PEDRO ASEMA LAZIMA TUVUNJE REKODI YA REAL MADRIDI

WINGA Machachali wa klabu ya Barcelona, Pedro Rodriguez amedai kuwa yeye na wachezaji wenzake wana nia ya kufikia rekodi ya Real Madrid ya alama 100 baada ya kufanikiwa kunyakuwa taji la La Liga mwishoni mwa wiki iliyopita. Barcelona walikabidhiwa taji lao la 22 la ligi wakati mahasimu wao Madrid waliposhindwa kuwafunga Espanyol na kutoa sare ya 1-1 na wako katika nafasi nzuri ya kuvunja rekodi hiyo ya Madrid kama wakishinda mechi zao zilizobakia. Mchezaji huyo amesema kwasasa nguvu zao wanazielekeza katika kusaka alama 100 ingawa amekiri kuwa itakuwa kazi ngumu kutokana na timu watakazocheza nazo. Nyota huyo pia alisisitiza kuwa msimu huu umekuwa wa mafanikio kwao pamoja na kuenguliwa na Bayern Munich katika nusu fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

MESSI ASEMA TULICHEZA KWA WAKATI MGUMU BILA VILANOVA

MSHAMBULIAJI nyota Duniani wa kimataifa wa Argentina na klabu ya Barcelona, Lionel Messi amekiri kuwa ilikuwa ni ngumu kupambana na mazingira yaliyokuwepo wakati Tito Vilanova alipolazimika kuondoka katikati ya msimu huu. Vilanova aliondoka na kuliacha benchi la ufundi la klabu hiyo kwa zaidi ya miezi mitatu baada kukutwa na saratani ya koo Desemba 2012 ambapo Muargentina huyo anafurahia kwamba timu hiyo imeweza kunyakuwa taji pamoja na kumkosa kiongozi wao. Messi amesema amefurahi timu yake kunyakuwa taji hilo ingawa amekiri haikuwa kazi rahisi kunywakuwa taji hilo haswa kipindi ambacho walimkosa Vilanova aliyekwenda kwa matibabu kwani mabadiliko ya wazi yalionekana katika kikosi chao. Nyota huyo aliendelea kusema kuwa kutolewa kwao na Bayern Munich katika nusu fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya imekuwa ni changamoto kwao kwani watajipanga na kuhakikisha wanafanya vizuri zaidi. Amesema kwasasa timu na makocha wengi wamefanikiwa kung’amua aina ya mchezo wanaocheza hivyo kuwadhibiti lakini amedai kuwa haina maana timu hiyo inapaswa kubadilisha aina mchezo wao wa pasi nyingi kwani ndio unaowatambulisha duniani kote.

SHARAPOVA AJIWEKA PEMBENI MICHUANO YA ITALIAN OPEN.

MWANARIADHA nyota wa kike wa  mchezo wa tenisi, Maria Sharapova amejitoa katika michuano ya wazi ya Italia kabla ya mchezo wake wa robo fainali dhidi ya Sara Errani wa Italia kutokana na matatizo ya kimwili. Sharapova ambaye ni raia amejitoa mapema kwenye michuano hiyo ili aweze kupona haraka kwa ajili ya kutetea taji lake la michuano ya wazi ya Ufaransa baadae mwezi huu. Kwa upande mwingine mwanadada anayesshika namba moja katika orodha za ubora Serena Williams wa Marekani ameendeleza wimbi lake la ushindi baada ya kumchakaza bila huruma Dominika Cibulkova wa Slovakia kwa 6-0 6-1 na kutinga robo fainali ya michuano hiyo. Williams ambaye ameshinda mechi 21 mfululizo sasa atachuana na Carla Suarez Navarro wa Hispania kutafuta nafasi ya kutinga nusu fainali ya michuano hiyo.

FA YAWEKA SHERIA KALI KATIKA SUALA ZIMA LA UBAGUZI

SHIRIKISHO la Soka la Uingereza-FA linatarajia kutoa adhabu mpya ya mechi tano kwa mchezaji atakayekutwa na hatia ya kumfanyia vitendo vya kibaguzi mchezaji mwenzake msimu ujao. Katika kikao hicho cha mwaka cha FA kimedai katika taarifa yake kuwa kama mtuhumiwa akirudia kosa moja kwa moja atapewa adhabu ya mechi 10 zaidi. Klabu pia inaweza kutozwa faini ikiwa wachezaji wawili au zaidi watakutwa na hatia ya kufanya vitendo hivyo katika kipindi cha miezi 12. Mwenyekiti wa FA David Bernstein amesema wamefikia uamuzi huo kwasababu wanataka kila mchezaji acheze soka akiwa salama na katika mazingira mazuri. Beki wa Chelsea John Terry alifungiwa mechi nne na kutozwa faini ya paundi 220,000 kwa kumfanyia vitendo vya ubaguzi beki wa Queens Park Rangers Anton Ferdinand Octoba mwaka 2011 wakati mshambuliaji wa Liverpool yeye alifungiwa mechi nane na faini ya paundi 40,000 msimu uliopita kwa kumbagua Patrice Evra wa Manchester United.

PAZIA LIGI KUU YA VODACOM KUFUNGWA JUMAMOSI

Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara msimu huu (2012/2013) inafikia tamati kesho (Mei 18 mwaka huu) kwa timu zote 14 kupambana katika viwanja saba tofauti.

Mechi zote zitachezwa kuanzia saa 10 kamili jioni. Ni jukumu la kamishna wa mechi husika kuhakikisha mchezo unaanza katika muda uliopangwa, vinginevyo hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa mujibu wa Kanuni za Ligi Kuu ya Vodacom toleo la 2012.

Yanga ambayo tayari imeshatwaa ubingwa itakuwa mgeni wa Simba katika mechi namba 180 itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo mwamuzi atakuwa Martin Saanya kutoka Morogoro na Kamishna ni Emmanuel Kavenga wa Mbeya.

Mgambo Shooting vs African Lyon (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Mwamuzi ni Amon Paul wa Mara wakati Kamishna ni Ally Mkomwa kutoka Pwani), JKT Ruvu vs Mtibwa Sugar (Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam. Mwamuzi ni Israel Mujuni wa Dar es Salaam wakati Kamishna ni Salum Kikwamba kutoka Kilimanjaro).

Tanzania Prisons vs Kagera Sugar (Uwanja wa Sokoine, Mbeya. Mwamuzi ni Ibrahim Kidiwa wa Tanga wakati Kamishna ni John Kiteve kutoka Iringa), Oljoro JKT vs Azam (Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha. Mwamuzi ni Athuman Lazi wa Morogoro wakati Kamishna ni Juma Mgunda kutoka Tanga).

Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro utatumika kwa mechi kati ya Polisi Morogoro na Coastal Union ya Tanga ambapo Mwamuzi atakuwa Said Ndege wa Dar es Salaam wakati Kamishna ni Hakim Byemba kutoka Dodoma. Toto Africans itacheza na Ruvu Shooting katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ambapo mwamuzi ni Geoffrey Tumaini kutoka Dar es Salaam na Kamishna ni Josephat Magazi wa Singida.


RATIBA:


Jumamosi Mei 18
Toto Africans Vs Ruvu Shooting
Mgambo JKT Vs African Lyon
JKT Ruvu Vs Mtibwa Sugar
TZ Prisons Vs Kagera Sugar
Simba SC Vs Yanga SC
JKT Oljoro Vs Azam FC
Polisi Moro Vs Coastal Union
MSIMAMO:
***YANGA ***BINGWA
NA
TIMU
P
W
D
L
GF
GA
GD
PTS
1
YANGA
25
17
6
2
45
14
31
57
2
AZAM FC
25
15
6
4
45
20
25
51
3
SIMBA SC
25
12
9
4
38
23
15
45
4
KAGERA SUGAR
25
11
8
6
26
19
7
41
5
MTIBWA SUGAR
25
10
9
6
29
24
5
39
6
COASTAL UNION
25
8
11
6
25
23
2
35
7
RUVU SHOOTING
25
8
8
9
22
24
-2
32
8
JKT OLJORO
25
7
8
10
21
26
-5
29
9
TANZANIA PRISONS
25
7
8
10
16
22
-6
29
10
JKT RUVU
25
7
5
13
21
38
-17
26
11
MGAMBO SHOOTING
25
7
4
14
16
27
-11
25
12
POLISI MOROGORO
25
4
10
11
13
23
-10
22
13
TOTO AFRICAN
25
4
10
11
21
33
-12
22
14
AFRICAN LYON
25
5
4
16
16
38
-22
19

AFRICAN LYON IMESHUKA DARAJA
WAOWAHI KUWA MABINGWA:
1965 Sunderland (Sasa inaitwa Simba SC)
1966 Sunderland
1967 Cosmopolitan
1968 Young Africans
1969 Young Africans
1970 Young Africans
1971 Young Africans
1972 Young Africans
1973 Simba SC
1974 Young Africans
1975 Mseto SC
1976 Simba SC
1977 Simba SC
1978 Simba SC
1979 Simba SC
1980 Simba SC
1981 Young Africans
1982 Pan Africans
1983 Young Africans
1984 Simba SC
1985 Young Africans
1986 Tukuyu Stars
1987 Young Africans
1988 Coastal Union
1989 Young Africans
1990 Simba SC
1991 Young Africans
1992 Young Africans
1993 Young Africans
1994 Simba SC
1995 Simba SC
1996 Young Africans
1997 Young Africans
1998 Young Africans
1999 Mtibwa Sugar
2000 Mtibwa Sugar
2001 Simba SC
2002 Young Africans
2003 Simba SC
2004 Simba SC
2005 Young Africans
2006 Young Africans
2007 Simba SC
2007/08 Young Africans
2008/09 Young Africans
2009/2010 Simba SC
2010/2011 Young Africans
2011/2012 Simba SC
2012/2013 Young Africans


MECHI ZA MARUDIANO RCL WIKIENDI HII
Mechi za marudiano za raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) zinachezwa wikiendi hii katika viwanja kumi tofauti wakati mechi ya Flamingo ya Arusha na Machava FC ya Kilimanjaro yenyewe itachezwa Jumatatu (Mei 20 mwaka huu).

Uamuzi wa mechi hiyo kuchezwa Jumatatu ni kutokana na Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid kutumika kwa mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kesho wakati Jumapili utatumika kwa shughuli nyingine za kijamii kwa mujibu wa wamiliki wa uwanja huo (CCM Mkoa wa Arusha).

Mechi nyingine zitachezwa keshokutwa (Jumapili) ambapo Abajalo watakuwa wenyeji wa Red Coast kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam. Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara utatumika kwa mechi kati ya wenyeji Coast United na Kariakoo ya Lindi.

African Sports ya Tanga itaoneshana kazi na Techfort ya Ifakara mkoani Morogoro katika mchezo utakaochezwa Uwanja wa Mkwakwani. Nayo Simiyu United ya Simiyu itakuwa mgeni wa Magic Pressure ya Singida kwenye Uwanja wa Namfua, mjini Singida.

Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ndiyo utakaotumika kuzikutanisha timu za Polisi Jamii Bunda kutoka Mara na wenyeji UDC wakati Biharamulo FC ya Kagera na Polisi SC ya Geita zitaumana kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Milambo FC ya Tabora itakuwa mwenyeji wa Saigon FC ya Kigoma kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora huku Mbinga United ya Ruvuma ikiikaribisha Njombe Mji ya Njombe kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini Iringa utatumika kwa mechi kati ya wenyeji 841 KJ dhidi ya Kimondo SC kutoka Mbeya. Nazo Rukwa United na Katavi Warriors zitapimana ubavu kwenye Uwanja wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga.

Timu zitakazofuzu kucheza raundi ya pili zitacheza mechi zao za kwanza kati ya Mei 25 na 26 mwaka huu wakati mechi za marudiano ni kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu.

UTARATIBU WA SAFARI MECHI YA TAIFA STARS v MOROCCO
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litasaidia upatikanaji wa visa kwa waandishi wa habari na Watanzania wengine wanaotaka kwenda Morocco kushuhudia mechi kati ya Taifa Stars na Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco.

Kwa ambao wangependa kupata visa kupitia TFF wanatakiwa kuwasilisha pasipoti zao, ada ya visa ambayo ni dola 50 za Marekani pamoja na picha mbili zenye kivuli (background) ya rangi nyeupe kabla ya saa 6 kamili Mei 20 mwaka huu.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)