Saturday, April 19, 2014

ASHANT,JKT OLJORO, RHINO RANGERS MKONO WA KWAHERI ZASHUKA DARAJA



Ligi kuu Vodacom Tanzania bara leo imefikia tamati baada ya timu zote kusha dimbani katika viwanja saba hapa nchini ambapo Azam FC imekabidhiwa Kombe lao huko Azam Complex, Chamazi mara baada ya Mechi yao ya kukamilisha Ratiba ambayo waliifunga JKT Ruvu Bao 1-0.
Kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es Salaam, Watani wa Jadi, Yanga na Simba nao walikutana kwenye Dabi ya Kariakoo, isiyokuwa na maan
a yeyote mbali ya kukamilisha Ratiba, na kutoka Sare ya Bao 1-1.
Kwenye Mechi hiyo, iliyohudhuriwa na Watazamaji wachache tofauti na desturi, Simba walitangulia kufunga Bao katika Dakika ya 76 Mfungaji akiwa Haruna Chanongo na Yanga kusawazisha kwa Bao la Dakika ya 86 la Simon Msuva.
Mechi pekee iliyokuwa na umuhimu mkubwa ni ile iliyochezwa Uwanja wa Jamhri huko Morogoro kati ya Tanzania Prisons na Ashanti United na Prisons kuifunga Ashanti Bao 1-0 na wao kupona na kuishusha Daraja Ashanti ambao wa
naungana na JKT Oljoro na Rhino Rangers kuporomoka Daraja.
VPL, LIGI KUU VODACOM
Mechi za mwisho za Ligi
Ratiba/Matokeo:
Jumamosi Aprili 19
Rhino Rangers v Ruvu Shooting [Ali Hassan Mwinyi, Tabora]
Mbeya City 1 Mgambo JKT 0 [Sokoine, Mbeya]
Tanzania Prisons 1 Ashanti United 0 [Jamhuri, Morogoro]
JKT Ruvu 0 Azam FC [Azam 1 Complex, Chamazi]
JKT Oljoro 1 Mtibwa Sugar 1 [Sheikh Amri Abeid, Arusha]
Coastal Union 0 Kagera Sugar 1 [Mkwakwani, Tanga]
Yanga 1 Simba 1 [National Stadium, Dar es Salaam]
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Azam FC
26
18
8
0
51
15
36
62
2
Young Africans
26
16
8
2
61
19
42
56
3
Mbeya City
26
13
10
3
33
20
13
49
4
Simba SC
26
9
11
6
41
27
14
38
5
Kagera Sugar
26
9
11
6
23
20
3
38
6
Ruvu Shooting
25
9
8
8
26
32
-6
35
7
Mtibwa Sugar
26
7
10
9
30
31
-1
31
8
JKT Ruvu
26
10
1
15
23
40
-17
31
9
Coastal Union
26
6
11
9
17
20
-3
29
10
Mgambo JKT
26
6
8
12
18
35
-17
26
11
Tanzania Prisons
26
6
10
10
26
33
-7
28
12
Ashanti United
26
6
7
13
20
39
-19
25
13
JKT Oljoro
26
3
10
13
19
37
-18
19
14
Rhino Rangers
25
3
7
15
18
37
-19
16

SIMBA YANGA HAKUNA MBABE AZAM YAKABIDHIWA NDOO.

Goli la dakika ya 86 la Simon Msuva dakika ya 86, jioni hii limeinusuru Yanga SC kulala mbele ya wapinzani wake, Simba SC baada ya kupata sare ya 1-1 katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati Uwanja wa Azam Complex, Chamazi bao la Brian Umony limeipa Azam ushindi wa 1-0 dhidi ya JKT Ruvu.

Simba SC ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Haroun Chanongo dakika ya 68 na kwa matokeo hayo, Azam inamaliza Ligi Kuu na pointi 62 wakati Yanga SC inamaliza na pointi 56 katika nafasi ya pili- ambapo sasa Azam FC ni mabingwa wapya ambao hawaja poteza mechi hata moja katika msimu wa Ligi Kuu  2013/2014.

Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ameikabidhi mkabidhi Kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni hii baada ya kuifunga bao 1-0 JKT Ruvu Uwanja wa Azam C
omplex, Chamazi, Dar es Salaam.


Mabingwa hao wakisherehekea na taji lao ambapo sherehe za ubingwa zimeanza jioni hii katika uwanja wa  Complex hadi usiku wa mana
ne

Mbali ya yotetimu zilizoshuka daraja msimu huu ni Ashanti United, Jkt Oljoro Pamoja na Rhino Rangers ambazo zimeaga mkono wa
kwaheri kuzipisha timu za Stends United ya shinyanga,Polisi Morogoro Pamoja na Ndanda fc ya Mtwara.