Monday, June 10, 2013

PEREIRA RASMI KUIFUNDISHA AL AHLI YA SAUDI ARABIA.

KLABU ya Al Ahli ya Saudi Arabia imethibitisha na kuweka wazi kuwa imemteua Vitor Pereira kuwa kocha mpya wa klabu hiyo baada kocha huyo kuondoka Porto mwishoni mwa msimu huu. Pereira ameifundisha Porto kwa kipindi cha misimu miwili baada ya kuchukua nafasi ya Andre Villas-Boas Juni mwaka 2011 na kuisadia klabu hiyo kushinda mataji mawili ya Ligi Kuu nchini Ureno. Katika taarifa iliyotolewa katika mtandao wa klabu hiyo, Pereira mwenye umri wa miaka 44 atajiunga rasmi na klabu hiyo Juni 27 kabla ya kuiandaa timu kwa ajili ya msimu ujao siku mbili baadae. Pia zimekuwepo taarifa kuwa atatua katika klabu hiyo na wasaidizi wake wa watatu kutoka Ureno kwa ajili ya kuimarisha benchi lake la ufundi.

MMOJA APOTEZA MAISHA KATIKAMICHUANO YA LANGALANGA YA CANADIAN.

MASHINDANO ya langalanga ya Canadian Grand Prix jana yalimalizika kwa Majonzi makubwa baada ya mmoja wa wafanyakazi mwenye umri wa miaka 38 kufariki baada ya kukanyagwa na winji. Ajali hiyo ilitokea wakati gari la dereva Esteban Gutierrez wa timu ya Sauber lilipokuwa likiondolewa barabara za Montreal baada ya kupata ajali.

Mashuhuda wanasema wakati winji hilo likijaribu kuliondoa gari hilo ndipo mfanyakazi huyo aliangusha radio yake na wakati akiiokota ndipo alipokanyagwa kwasababu dereva wa winji hakumuona. Katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter Gutierrez alituma salamu zake za rambirambi kwa familia ya mfanyakazi huyo kwa kumpoteza mtu wao karibu. Mbali na Gutierrez madereva wengine waliotoa rambirambi zao ni pamoja na Sebastian Vettel wa Red Bull aliyeshinda mbio hizo pamoja na Fernando Alonso wa Ferrari aliyeshika nafasi ya pili. Hilo ni tukio la pili kutokea katika mashindano hayo kwani mwaka jana katika michuano ya Grand Prix ya Italia mfanyakazi wa kujitolea wa zimamoto Paolo Ghislimberti alifariki kutoka na amejraha aliyopata kichwani na kifuani baada ya kupigwa na tairi lililochomoka kutoka katika gari la Heinz-Harald Frentzen wa timu ya Jordan.

TAIFA STAR YATUA NCHINI IKITOKEA NCHINI MORROCO.

TIMU ya taifa ya  Tanzania, Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imewasili  nchini leo asubuhi.
Taifa stars ilikuwa Morocco kucheza na wenyeji wao ambapo katika mchezo huo taifa star imefungwa bao 2-1 katika mechi ya Kundi C kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil.

Stars ambayo bado inashika nafasi ya pili katika kundi hilo ikiwa na pointi sita imewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Aidha katika kundi c kinara wa kundi hilo ni Ivory Coast yenye point kumi ambayo itacheza mchezo wa marudiano na Taifa Star wikiendi ijayo katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

Hata hivyo kwa upande wa kundi hilo nafasi ya tatu inashikiliwa na Morocco yenye point tano huku nafasi ya mwisho ikishiliwa na Gambia yenye point moja.
KUNDI C


Pos
Team
P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts
1
Ivory Coast
4
3
1
0
10
2
8
10
2
Tanzania
4
2
0
2
6
6
0
6
3
Morocco
4
1
2
1
6
7
-1
5
4
Gambia
4
0
1
3
2
9
-7
1