Monday, February 17, 2014

WENGER AMJIBU MBWATUKAJI MOURINHO

Kocha wa Klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amefafanua kauli ya Jose Mourinho kumuita mtaalamu wa kushindwa kuwa ni kauli ya kijinga na iliyokosa heshima. Kauli ya hiyo ya Mourinho aliitoa kujibu kauli iliyotolewa na Wenger kuwa baadhi ya mameneja wa timu za Ligi Kuu nchini Uingereza wanadai kuwa hawana mpango na taji hilo msimu huu kutokana na uoga wao. Akihojiwa Wenger amesema hataki kuingia katika vita ya maneno na Mourinho lakini anadhani kauli yake ni aibu kwa timu yake ya Chelsea kuliko ilivyo kwake. Wenger amesema asingependa kuzungumzia kauli za kijinga na zilizokosa heshima kwasababu huwa hapendi kumzungumzia Mourinho katika mikutano yake na waandishi wa habari na hatakuja kufanya hivyo. Kocha huyo alikipongeza kikosi chake kwa kucheza vizuri katika mchezo dhidi ya Liverpool ambao uliwawezesha kukata tiketi ya robo fainali ya Kombe la FA kwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.

KAKA ASEMA NI MCHEZA NA MCHEZAJI BORA CRISTIANO RONALDO

KIUNGO Mahiri wa klabu ya AC Milan ya Italia, Kaka amebainisha kuwa Lionel Messi na Zinedine Zidane ni wachezaji bora aliokutana nao na kudai kuwa Cristiano Ronaldo ndio mchezaji bora kabisa kuwahi kucheza naye. Kiungo huyo wa kimataifa wa Brazil, amewahi kukutana na Messi mara kadhaa wakati akicheza Real Madrid ambako alikuwa akicheza sambamba na Ronaldo. Kaka aliandika katika ukurasa rasmi wa twitter wa Milan wakati akijibu maswali ya mashabiki ambapo amesema wachezaji bora aliowahi kucheza dhidi yao ni Zidane na Messi huku akimtaja Ronaldo kama mchezaji bora aliyewahi kucheza naye. Kaka pia alimtaja Paulo Maldini kama beki bora kabisa duniani kuwahi kucheza naye kabla hajaondoka Milan kwenda Madrid.

TPS KUWAWEZESHA WASICHANA WALIOKOSA FURSA

Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), imeahidi kuchangia Sh. milioni 1.7 kwa ajili ya kitengo cha wasichana waliokosa fursa.

Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa TPSF, Godfrey Simbeye, aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kitengo hicho kilichopo chini ya usimamizi wa Chama cha Wanawake Wafanyabiashara, kazi za mikono na nguo. (Tahowete).

Simbeye alisema atakwenda kuwaombea fedha hizo TPSF ili kuwasaidia wasichana hao watano katika shule ya ushonaji na kuongeza kuwa wajasiriamali wangewezeshwa kwa kuwa wakifanya biashara wanaweza na bila kuwezeshwa hawawezi kufanya jambo lolote.

Aidha alisema serikali ina mpango wa kuanzisha miradi ambayo wanataka iwawezeshe wanawake,.

Mwenyekiti wa Tawohate, Anna Matinde, alisema chama hicho kinasaidia jamii hasa wasichana wanaomaliza masomo na kukosa ajira, pamoja na wale wanaonyanyasika kijamii kwa kuanzisha miradi ambayo wasichana hao waliokatiza masomo waweze kuendelea na masomo.
Chanzo: Nipashe