Monday, February 17, 2014
WENGER AMJIBU MBWATUKAJI MOURINHO
KAKA ASEMA NI MCHEZA NA MCHEZAJI BORA CRISTIANO RONALDO
KIUNGO Mahiri wa klabu ya AC
Milan ya Italia, Kaka amebainisha kuwa Lionel Messi na Zinedine Zidane
ni wachezaji bora aliokutana nao na kudai kuwa Cristiano Ronaldo ndio
mchezaji bora kabisa kuwahi kucheza naye. Kiungo huyo wa kimataifa wa
Brazil, amewahi kukutana na Messi mara kadhaa wakati akicheza Real
Madrid ambako alikuwa akicheza sambamba na Ronaldo. Kaka aliandika
katika ukurasa rasmi wa twitter wa Milan wakati akijibu maswali ya
mashabiki ambapo amesema wachezaji bora aliowahi kucheza dhidi yao ni
Zidane na Messi huku akimtaja Ronaldo kama mchezaji bora aliyewahi
kucheza naye. Kaka pia alimtaja Paulo Maldini kama beki bora kabisa
duniani kuwahi kucheza naye kabla hajaondoka Milan kwenda Madrid.
TPS KUWAWEZESHA WASICHANA WALIOKOSA FURSA

Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), imeahidi kuchangia Sh. milioni 1.7 kwa ajili ya kitengo cha wasichana waliokosa fursa.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa TPSF, Godfrey Simbeye, aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kitengo hicho kilichopo chini ya usimamizi wa Chama cha Wanawake Wafanyabiashara, kazi za mikono na nguo. (Tahowete).
Simbeye alisema atakwenda kuwaombea fedha hizo TPSF ili kuwasaidia wasichana hao watano katika shule ya ushonaji na kuongeza kuwa wajasiriamali wangewezeshwa kwa kuwa wakifanya biashara wanaweza na bila kuwezeshwa hawawezi kufanya jambo lolote.
Aidha alisema serikali ina mpango wa kuanzisha miradi ambayo wanataka iwawezeshe wanawake,.
Mwenyekiti wa Tawohate, Anna Matinde, alisema chama hicho kinasaidia jamii hasa wasichana wanaomaliza masomo na kukosa ajira, pamoja na wale wanaonyanyasika kijamii kwa kuanzisha miradi ambayo wasichana hao waliokatiza masomo waweze kuendelea na masomo.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa TPSF, Godfrey Simbeye, aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kitengo hicho kilichopo chini ya usimamizi wa Chama cha Wanawake Wafanyabiashara, kazi za mikono na nguo. (Tahowete).
Simbeye alisema atakwenda kuwaombea fedha hizo TPSF ili kuwasaidia wasichana hao watano katika shule ya ushonaji na kuongeza kuwa wajasiriamali wangewezeshwa kwa kuwa wakifanya biashara wanaweza na bila kuwezeshwa hawawezi kufanya jambo lolote.
Aidha alisema serikali ina mpango wa kuanzisha miradi ambayo wanataka iwawezeshe wanawake,.
Mwenyekiti wa Tawohate, Anna Matinde, alisema chama hicho kinasaidia jamii hasa wasichana wanaomaliza masomo na kukosa ajira, pamoja na wale wanaonyanyasika kijamii kwa kuanzisha miradi ambayo wasichana hao waliokatiza masomo waweze kuendelea na masomo.
Chanzo:
Nipashe
Subscribe to:
Posts (Atom)