Monday, February 17, 2014

WENGER AMJIBU MBWATUKAJI MOURINHO

Kocha wa Klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amefafanua kauli ya Jose Mourinho kumuita mtaalamu wa kushindwa kuwa ni kauli ya kijinga na iliyokosa heshima. Kauli ya hiyo ya Mourinho aliitoa kujibu kauli iliyotolewa na Wenger kuwa baadhi ya mameneja wa timu za Ligi Kuu nchini Uingereza wanadai kuwa hawana mpango na taji hilo msimu huu kutokana na uoga wao. Akihojiwa Wenger amesema hataki kuingia katika vita ya maneno na Mourinho lakini anadhani kauli yake ni aibu kwa timu yake ya Chelsea kuliko ilivyo kwake. Wenger amesema asingependa kuzungumzia kauli za kijinga na zilizokosa heshima kwasababu huwa hapendi kumzungumzia Mourinho katika mikutano yake na waandishi wa habari na hatakuja kufanya hivyo. Kocha huyo alikipongeza kikosi chake kwa kucheza vizuri katika mchezo dhidi ya Liverpool ambao uliwawezesha kukata tiketi ya robo fainali ya Kombe la FA kwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.