Monday, February 17, 2014

KAKA ASEMA NI MCHEZA NA MCHEZAJI BORA CRISTIANO RONALDO

KIUNGO Mahiri wa klabu ya AC Milan ya Italia, Kaka amebainisha kuwa Lionel Messi na Zinedine Zidane ni wachezaji bora aliokutana nao na kudai kuwa Cristiano Ronaldo ndio mchezaji bora kabisa kuwahi kucheza naye. Kiungo huyo wa kimataifa wa Brazil, amewahi kukutana na Messi mara kadhaa wakati akicheza Real Madrid ambako alikuwa akicheza sambamba na Ronaldo. Kaka aliandika katika ukurasa rasmi wa twitter wa Milan wakati akijibu maswali ya mashabiki ambapo amesema wachezaji bora aliowahi kucheza dhidi yao ni Zidane na Messi huku akimtaja Ronaldo kama mchezaji bora aliyewahi kucheza naye. Kaka pia alimtaja Paulo Maldini kama beki bora kabisa duniani kuwahi kucheza naye kabla hajaondoka Milan kwenda Madrid.