Monday, September 8, 2014

KOCHA PATRIC PHIRI ASEMA KIKOSI KIPO KAMALI KWA VPL

Kocha mkuu wa timu ya soka ya Simba  Patrick Phiri amesema amelizishwa na kiwango cha timu hiyo mara baada ya kuitandika timu ya Gor mahia kutoka Kenya  kwa mabao 3 kwa 0 katika mchezo uliopigwa katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam siku ya jumamosi.
Akizungumza na mkali wa dimba tz.blogspot.com Patrick Phiri  amesema kuwa wachezaji wake wanajituma katika michezo yao na kucheza vizuri katika mechi zote anazoziongoza.

Phiri amesema wanacheza vizuri uwanjani,uwezo umeongezeka,wamecheza na timu bora kutoka kenya,kwa hiyo naweza kusema hiki ni kipimo sahihi kwa timu yangu"alisema Patrick Phiri 

Patrick Phiri amesema maandalizi waliyoyafanya visiwani Zanzibar kumewafanya wachezaji wake wawe vizuri na anafuraha kuona kikosi chake kimeimalika.

YANGA YASEMA KUFA NA KUPOMA KUHUSU SAKATA LA OKWI KUKATAA RUFAA FIFA YASEMA MPAKA KIELEKE

Uongozi wa klabu ya Yanga umesema utapinga maamuzi ya kamati ya Sheria na Hadhi ya Wachezaji  kuhusiana na maamuzi yake ya kumtangaza mchezaji wake, Emmanuel Okwi kuwa huru.
Mwenyekiti wa Kamati  ya Sheria ya Yanga, Sam Mapande amesema kuwa hawajaridhishwa na maamuzi hayo ambayo yanakinzana na shitaka zima la mchezaji huyo.
Mapande amesema kuwa kamati ya TFF imeamua sakata la Okwi kinyume na malalamiko yao kwani hakukuwa na lalamiko la mchezaji huyo wa Uganda kuhusiana na malipo ya fedha zake za usajili.
Alisema kuwa cha kushangaza, kamati hiyo ya TFF iliamua kusikiliza kesi ambayo haikuwa mbele yao na kutoa maamuzi ambayo hata wao wameshangazwa nayo.
“Kwanza kesi yenyewe ilikuwa haijamalizika, walituambia tuwasilishe vielelezo kuhusiana na kitendo cha mchezaji huyo kufanya mazungumzo na klabu ya Misri, lakini cha kushangaza maamuzi yametolewa, hili limetushangaza sana,” alisema Mapande.
Alisema kuwa mazingira yalikuwa yameandaliwa kuibeba Simba na Okwi kwani hata malalamiko yao kwa Simba hayakusikilizwa. “Malalamiko yetu yalikuwa wazi kabisa, yapo kimaandishi, hatukuwai kulalamikiwa, suala la fedha za usajili la Okwi limetoka wapi, kama lilikuwepo, mbona hatujajulishwa kimaandishi kama utaratibu ulivyo,” alisema.
Alisema kuwa Kamati hiyo kumruhusu mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo Zacharia Hans Pope ambaye pia ni mwenyekiti wakamati ya usajili ya Simba kuwemo katika kikao hicho kinyume na taratibu za Fifa kupitia kifungu namba 19 kinachoeleza mgongano wa kimaslah.

                                              MAAMUZI YA KIKAO CHA JANA
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekutana leo (Septemba 7
mwaka huu) na kupitia masuala mbalimbali ikiwemo mgogoro wa kimkataba kati ya klabu ya Yanga na mchezaji Emmanuel Okwi.

Mkataba huo ulipitiwa na Kamati ikiwemo kumsikiliza mchezaji mwenyewe pamoja na upande wa Yanga, na kuridhika kuwa mkataba kati ya pande hizo umevunjika.

Ukiwa ni mkataba wa pande mbili, Yanga ilikiuka kipengele namba 8 kuhusu malipo ya ada ya usajili.

Yanga ikiwa mwajiri, haikutekeleza kipengele hicho cha kimkataba hadi kufikia Juni 27 mwaka huu ilipoandika barua TFF kuomba mkataba huo uvunjwe. Kwa maana hiyo Okwi ni mchezaji huru, hivyo yuko huru kujiunga na timu yoyote.
Mkataba ni uhusiano kati ya mwajiri (Yanga) na mwajiriwa (Okwi), ambapo Kamati imebaini kuwa uhusiano huo haupo,hivyo hakuna mazingira ya pande hizo mbili kuendelea kufanya kazi pamoja.

Pamoja na Yanga kuwasilisha pingamizi la kuwepo mmoja wa wajumbe katika kikao kwa sababu za kimaslahi (conflict of interests), walifahamishwa kuwa kilichopo mbele ya kamati ni mgogoro wa kimkataba kati ya Yanga na Okwi, na si usajili.

Pia lilijitokeza suala la Okwi kutakiwa na klabu ya Wadi Degla ya Misri. Kamati imeiagiza Sekretarieti ya TFF kulifanyia uchunguzi suala hilo na kulitolea taarifa katika kikao kijacho.

Hata hivyo mjumbe huyo hakushiriki katika kuchangia hoja na kutoa maamuzi. Uamuzi wa kamati ulifanyika baada ya majadiliano, hivyo hakukuwa na suala la kupiga kura.

Kuhusu pingamizi la Coastal Union kwa Abdi Banda, Kamati imebaini kuwa klabu hiyo imevunja mkataba kati ya pande hizo mbili kwa kushindwa kumlipa mchezaji huyo mshahara wa miezi mitatu mfululizo kama takwa la mkataba.
Klabu ya Coastal Union iliwakilishwa na mmoja wa viongozi wake, wakati Banda aliwakilishwa na mwanasheria wake.

Vilevile Kamati imekubaliana na pingamizi la Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Morogoro (MRFA) kuhusu wachezaji waliofanyiwa uhamisho kutoka katika mkoa wake bila kulipiwa ada za usajili, hivyo klabu husika zinatakiwa kulipa ada hizo.

Pia Kamati imeagiza klabu zote zilizosajili wachezaji bila kuwafanyia uhamisho, kulipa ada za uhamisho kwa pande husika kabla ya kuanza ligi, vinginevyo leseni zao zitazuiwa hadi watakapolipa.

Mashauri mengine ya pingamizi yatasikilizwa baadaye kwa vile klabu husika hazikupata fursa ya kufika mbele ya kamati.

TFF YATUMA RAMBIRAMBI MSIBA WA MWAMUZI LUGENGE

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mwamuzi wa daraja la kwanza (class one), Luteni  David Lugenge kilichotokea jana (Septemba 7 mwaka huu) kwa ajali ya gari katika Wilaya ya Handeni mkoani Tanga.

Luteni Lugenge ambaye mwishoni mwa wiki alishiriki mitihani ya utimamu wa mwili kwa waamuzi wa Ligi Kuu alikuwa na ndugu yake Christopher Alexander Lunyungu katika gari dogo wakienda mkoani Kilimanjaro.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Handeni, Peter Juma, Luteni Lugenge alikuwa akimsindikiza mwenzake aliyekuwa anakwenda kujitambulisha kwa wakwe zake watarajiwa.
Msiba huo ni mkubwa katika familia ya mpira wa miguu kwani Luteni Lugenge alikuwa ni mmoja wa waamuzi wanaoinukia nchini, hivyo mchango wake ulikuwa bado unahitajika. Hivyo tutamkumbuka daima.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Luteni Lugenge, Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu nchini (FRAT) na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
 BONIFACE WAMBURA
KNY KATIBU MKUU
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

BRATTER ASEMA BADO NATAKA UONGOZI WA FIFA-URAIS


Sepp Blatter ambae ni raisi wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA  amethiboitisha kuwa atatetea kiti chake hicho katika uchaguzi ujao wa shirikisho hilo. Akihojiwa jijini Manchester Blatter mwenye umri wa miaka 78 alithibitisha uamuzi wake huo kuhu akidai atatoa taarifa rasmi katika mkutano mkuu wa kamati ya utendaji ya FIFA utakaofanyika Septemba 25 na 26. Tayari rais wa Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA Michel Platini ameshatangaza kutogombea nafasi hiyo ya Blatter. Blatter ambaye amekuwa katika kiti hicho cha FIFA toka mwaka 1998 amesema amechukua uamuzi huo kwasababu kazi alioianza anaona bado haijamalizika.