MENEJA
wa klabu ya Liverpool, Brendan Rodgers amempigia chapuo Jordan Henderson kuziba
nafasi ya Steven Gerrard wakati nahodha huyo wa timu hiyo atakapoondoka
mwishoni msimu huu.
Gerrard mwenye umri wa miaka 34 amethibitisha Ijumaa
iliyopita kuwa hataongeza mkataba mwingine na ataondoka katika majira ya
kiangazi huku akihusishwa na kwenda kucheza soka Marekani.
Henderson amekuwa
akionyesha kiwango kizuri chini Rodgers akicheza sambamba na Gerrard na maneja
huyo anaamini kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 ataw
eza kuziba vyema nafasi
ya mkongwe huyo atapoondoka.
Akihojiwa Rodgers amesema anadhani Henderson ana
haiba ya uongozi na hiyo ndiyo sababu kubwa iliyomfanya kumpatia unahodha
msaidizi na pindi Gerrard atakapoondoka anadhani atakuja kuwa kiongozi mzuri kutokana
na uzoefu aliopata.