Monday, December 1, 2014

WATOTO OBAMA VITUKO NDANI YA SKENDO CHAFU YA MAVAZI YA UWAZI.TAZAMA PICHA ZOTE HAPA

 


Rais Barrack Obama na wanawe Sasha na Malia. Afisa mmoja wa chama cha Republican amewakosoa mavazi yao.Watoto wa rais wa Marekani Barrack Obama, Sasha na Malia wameshtumiwa kwa kukosa heshima na afisa mmoja wa chama cha Republican baada ya kuhudhuria sherehe za kutoa shukrani.
Elizabeth Lauten ,ambaye ni mkurugenzi wa mawasiliano wa mbunge Stephen Fincher alitoa matamshi yake katika mtandao wa 
facebook
 ambayo baadaye yalifutwa.

Baada ya kukosolewa Bi Lauten aliomba msamaha kwa kutoa matamshi hayo ya kukera.

Aliku akikosoa sketi fupi zilizovaliwa na wasichana hao wa Obama.Bi Lauteni 
pia
 aliwashtumu wasichana hao kwa kuonyesha uchovu wakati waliposimama na baba yao katika sherehe hiyo ya ikulu ya Whitehouse.

YACINE BRAHIMI ATWAA TUZO YA BBC YA UCHEZAJI BORA MWAKA HUU

Mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa Afrika BBC mwaka huu amepatikana. Baada ya maelfu ya kura kuhesabiwa, mchezaji wa Algeria na nyota wa Porto, Yacine Brahimi ndiye mshindi wa mwaka huu.
Hapajawahi kutokea katika miaka 23 ya historia ya shindano hilo kwa mchezaji bora kutoka Algeria kuishinda, lakini Brahimi amefanikiwa kutwaa tuzo hiyo baada ya mwaka uliokuwa na mbwembwe wa 2014.
Aliingiza bao la ushindi dhidi ya mabingwa wa Hispania Barcelona, bao lengine la kisasa katika ligi ya mabingwa wa ulaya na kisha kuwa katika msitari wa mbele wakati nchi yake iliposonga mbele katika michuano ya kombe la dunia.
Hio ilikuwa historia kwa Algeria kufika katika awamu ya muondoano katika dimba hilo.
Hii bila shaka ilikuwa nafasi nzuri kwa mashabiki wa BBC pamoja na wapenzi wa soka kumchagua kama mchezaji bora zaidi wa Afrika mwaka huu.
Aliwapiku wachezaji wengine nyota wakiwemo, Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon, Vincent Enyeama wa Nigeria, Gervinho wa Ivory Coast na hatimaye Yaya Toure - aliyenyakua ushindi mwaka jana.

EMERSON KIUNGO MBRAZIL ASAINI MKATABA MWAKA MMOJAYANGA

Kiungo Emerson De Oliveira Neves Roque leo amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia klabu ya Young Africans baada ya benchi la ufundi kuridhika na uwezo wake,na mchezaji mwenyewe kufikia makubaliano hayo ya kuwatumikia watoto wa Jangwani.
Baada ya kufanya mazoezi kwa siku nne mfululizo chini ya makocha Marcio Maximo, Leonardo Neiva na makocha wazawa Salavatory Edward, Shadrack Nsajigwa kwa pamoja wameridhiswa na uwezo wake na kuomba apewe kandarasi la kuitumikia klabu ya Young Africans.
Emerson aliyekua akichezea katika timu ya Bonsucesso iliyopo daraja la pili kwenye jimbo la Rio de Janeiro anachukua nafasi ya mshambuliaji Geilson Santos "Jaja" ambaye ameshindwa kureje nchini kutokana na matatizo ya kifamilia na kuomba klabu ya Young Africans imuache.
Kocha wa Young Africans Marcio Maximo amesema wamerizishwa na uwezo na kiungo mkabaji Emerson na kusema ataisaidia timu katika michuano mbali mbali ya Ligi na Kimataifa.
Ujio wa Emerson unafanya klabu ya Young Africans kufikisha jumla ya wachezaji watano wa kimataifa, wengine wakiwa ni Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima, Hamis Kizza na Andrey Coutinho.

SERIKALI YASEMA NI WAJIBU WA KILA SEKTA KUANDAA WATENDAJI WAO KWA KUWADHAMINI KATIKA MASOM

SERIKALI imesema ni wajibu wa kila sekta kuandaa watendaji wao kwa kuwadhamini katika masomo.
Mkurugenzi wa Idara ya Teknolojia habari na masiliano (Tehama) kutoka Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Dokta Ally Simba, amesema hayo katika hafla ya kutoa tunzo za udhamini kwa masomo ya Tehama kwa wanafunzi wa elimu ya juu mwaka 2014/2015.
Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), Ubungo jijini Dar es Salaam.
Dokta, Simba amesema kuwa ni mara ya nne kwa TCRA kutoa udhamini kwa elimu ya juu hasa kwa wale wa Tehama lengo ni kupata faida katika kizazi hiki na kijacho kikiwa na uelewa wa hali ya juu. 

BRENDAN RODGERS IPO MBIONI KUMPATIA MKATABA MPYA STEVEN GERRARD.


MENEJA wa klabu ya Liverpool Brendan Rodgers amesema timu hiyo tayari imeshamuofa mkataba mpya kiungo na nahodha wao Steven Gerrard. 
Kocha huyo pia alikanusha tetesi za kutoelewana na Gerrard ambaye mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu. 
Akizungumza kabla ya mchezo wao wa kesho wa Ligi Kuu dhidi ya Leicester, Rodgers amesema hakuna ugomvi wowote kati yake na Gerrard na kudai hayo yanayosemwa hayana ukweli wowote. 
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa Gerrard atapewa muda wa kufikiria ofa hiyo mpya lakini amedai pesa haitakuwa tatizo. 
Rodgers amesema amekuwa akifurahia kila dakika kufanya kazi na Gerrard na ni matumaini yake ataendelea kuitumikia klabu hiyo.

AVRAM GRANT KOCHA MPYA TIMU YA TAIFA YA GHANA ACHUKUWA MIKOBA YA KWESI APPIAH


KOCHA mpya wa timu ya taifa ya Ghana, Avram Grant ameanza kazi rasmi leo huku akitegemewa kuweka mikakati yake katikati ya wiki. 
Jumatano kocha huyo wa zamani wa Chelsea raia wa Israel anatarajiwa kuzungumza na wanahabari ili kuweka maono na mipango yake kwa soka la Ghana. 
Mkataba rasmi wa kocha huyo unaanza kufanya kazi leo lakini Chama cha Soka cha Ghana kimethibitisha kuwa tayari kocha huyo ameshatua na ataanza rasmi kibarua chake hicho kesho. 
Moja ya kibarua atakachokuwa nacho Grant mwenye umri wa miaka 59 ni kusaidia kujenga shule ya soka ya kitaifa na pia kusaidia mafunzo ya makocha wazawa wan chi hiyo. 
Grant ana wiki sita za kukiandaa kikosi kipya cha Ghana kwa ajili ya michuano ya Mataifa ya Afrika itakayofanyika huko Guinea ya Ikweta mapema mwakani.

KWESI APPIAH AMPA ULAJI SWAHIBA WAKE UKOCHA MSAIDIZI SUDAN.

KOCHA wa zamani wa timu ya taifa ya Ghana, Kwesi Appiah amemteua rafiki yake wa siku nyingi Prince Owusu kuwa msaidizi wake katika kibarua chake kipya huko nchini Sudan. 
Mara baada ya kuteuliwa kuwa kocha wa klabu ya Al-Khartoum Appiah aliamua kumvuta Owusu kuwa msaidizi wake baada ya wawili hao kufanya kazi pamoja kwa kipindi kirefu sasa. 
Owusu sio mgeni sana nchini Sudan kwani mara kadhaa amekuwa akiteuliwa kwenda huko kwa ajili ya mafunzo mafupi ya makocha. 
Wawili hao wanatarajiwa kusafiri kuelekea nchini Sudan Desemba 10 mwaka huu tayari kuanza kazi yao hiyo mpya. 
Al-Khartoum iko katika nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu nchini humo na wanatarajiwa kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho mwakani.

WAZIRI WA FEDHA AWATAKA WAHADHIRI WA VYUO KUTOA ELIMU WA WANAFUNZI KULINGANA NA SOKO LA AJIRA

 
WAZIRI wa fedha Saada Mkuya amewataka wahadhiri wa vyuo mbalimbali nchini kutoa elimu kwa wanafunzi kulingana na soko la ajira ikiwa ni pamoja na fani inayoendana na cheti alichopata ili kukabiliana na changamoto zinazojitokeza.
Waziri Mkuya ameyabainisha hayo kwenye mahafali ya 12 ya taasisi ya uhasibu (TIA) kampasi ya Mbeya yaliyofanyika katika viwanja vya taasisi hiyo mjini Mbeya ambapo waziri Mkuya aliwakilishwa na mkuu wa wilaya ya Mbeya dokta Norman Sigala.
Amesema kuwa hivi sasa kuna ushindani wa vyuo na ukosefu wa ajira nchini hivyo ni vema wahadhiri wakatoa wanafunzi wenye sifa kulingana na vyeti wanavyopata ili kukidhi soko la ajira ikiwa ni pamoja na kujiajiri wenyewe na sio kusubiri kuajiriwa.
Ameongeza kuwa wajibu wa vyuo ni kuandaa watalaam mbali mbali ili waweze kutumikia taifa na kukidhi haja ya nchi katika kujiletea maendeleo kwa wahitimu kufuata walitofundishwa madarasani na kutumia taaluma yao kupambana na changamoto zilizopo uraiani.
Kwa upande wake Afisa Mtendaji mkuu wa Tasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Dokta Joseph Kihanda,amesema katika mwaka wa masomo 2013/2014 jumla ya wanafunzi 1960 wakiwemo wanawake 947 na wanaume 1013 wamehitimu katika fani za cheti cha awali, Stashahada na stashahada ya uzamili katika kampasi ya Mbeya.

ATHUMANI IDD CHUJI AWEKA WAZI KUU YEYE NI JEMBE KULIKO MBRAZIL EMRSON.

Athumani Idd Chuji  Kiungo mkabaji wa zamani wa Yanga, amesema kuwa uwezo wake kamwe hauwezi kuulinganisha na Mbrazili Emerson Roque ambae ni kiungo mpya wa timu hiyo.
Emerson tayari yuko jijini Dar es Salaam ambapo tayari ameanza mazoezi na timu ya Yanga.
Chuji alitupiwa viragoooo na Yanga katika usajili wa msimu huu wa Ligi Kuu Bara baada ya mkataba wake kumalizika kabla ya kwenda Oman kwenye majaribio na kurejea nchini kwa kile kilichoelezwa kushindwa, akiwa na Betram Mwombeki na Mkenya, Jerry Santo.

Hata hivyo Chuji kwa sasa yupo katika timu ya Mwadui FC ya shinyanga inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza ambapo ameweka wazi kuwa yeye ni jembe kuliko Emerson.

TAIFA STARS MABORESHO YAINGIA KAMBI

Kikosi cha Taifa Stars Maboresho kimeingia kambini leo (Desemba 1 mwaka huu) Bulyanhulu mkoani Shinyanga kujiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Burundi itakayochezwa Desemba 9 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Ikiwa chini ya Kocha Mart Nooij, Stars Maboresho itapiga kambi mkoani humo hadi Desemba 6 mwaka huu ambapo itarejea jijini Dar es Salaam tayari kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Uwanja wa Taifa.

Wachezaji walioingia kambini ni Abubakar Ally (Coastal Union), Abubakar Ally Mohamed (White Bird), Aishi Manula (Azam), Andrew Vicent (Mtibwa Sugar), Atupele Green (Kagera Sugar), Edward Charles (Yanga) na Emmanuel Semwanda (African Lyon).

Gadiel Michael (Azam), Hashim Magoma (Stand United), Hassan Banda (Simba), Hassan Mwasapili (Mbeya City), Joram Mgeveke (Simba), Kassim Mohamed Simbaulanga (African Lyon), Kelvin Friday (Azam) na Makarani Ally (Mtibwa Sugar).

Miraji Adam (Simba), Mohamed Hussein (Simba), Muzamir Ally (Mtibwa Sugar), Omari Nyenje (Ndanda), Pato Ngonyani (Yanga), Rashid Mandawa (Kagera Sugar), Said Hamisi (Simba), Salim Hassan Mbonde (Mtibwa Sugar) na Shiza Ramadhan (Mtibwa Sugar).

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linaishukuru kampuni ya kuchimba madini ya Acacia Mining PLC (zamani African Barrick Gold PLC) kwa kufadhili kambi ya Stars kupitia mgodi wa Bulyanhulu.


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)