Monday, December 1, 2014

ATHUMANI IDD CHUJI AWEKA WAZI KUU YEYE NI JEMBE KULIKO MBRAZIL EMRSON.

Athumani Idd Chuji  Kiungo mkabaji wa zamani wa Yanga, amesema kuwa uwezo wake kamwe hauwezi kuulinganisha na Mbrazili Emerson Roque ambae ni kiungo mpya wa timu hiyo.
Emerson tayari yuko jijini Dar es Salaam ambapo tayari ameanza mazoezi na timu ya Yanga.
Chuji alitupiwa viragoooo na Yanga katika usajili wa msimu huu wa Ligi Kuu Bara baada ya mkataba wake kumalizika kabla ya kwenda Oman kwenye majaribio na kurejea nchini kwa kile kilichoelezwa kushindwa, akiwa na Betram Mwombeki na Mkenya, Jerry Santo.

Hata hivyo Chuji kwa sasa yupo katika timu ya Mwadui FC ya shinyanga inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza ambapo ameweka wazi kuwa yeye ni jembe kuliko Emerson.