Monday, December 1, 2014

WAZIRI WA FEDHA AWATAKA WAHADHIRI WA VYUO KUTOA ELIMU WA WANAFUNZI KULINGANA NA SOKO LA AJIRA

 
WAZIRI wa fedha Saada Mkuya amewataka wahadhiri wa vyuo mbalimbali nchini kutoa elimu kwa wanafunzi kulingana na soko la ajira ikiwa ni pamoja na fani inayoendana na cheti alichopata ili kukabiliana na changamoto zinazojitokeza.
Waziri Mkuya ameyabainisha hayo kwenye mahafali ya 12 ya taasisi ya uhasibu (TIA) kampasi ya Mbeya yaliyofanyika katika viwanja vya taasisi hiyo mjini Mbeya ambapo waziri Mkuya aliwakilishwa na mkuu wa wilaya ya Mbeya dokta Norman Sigala.
Amesema kuwa hivi sasa kuna ushindani wa vyuo na ukosefu wa ajira nchini hivyo ni vema wahadhiri wakatoa wanafunzi wenye sifa kulingana na vyeti wanavyopata ili kukidhi soko la ajira ikiwa ni pamoja na kujiajiri wenyewe na sio kusubiri kuajiriwa.
Ameongeza kuwa wajibu wa vyuo ni kuandaa watalaam mbali mbali ili waweze kutumikia taifa na kukidhi haja ya nchi katika kujiletea maendeleo kwa wahitimu kufuata walitofundishwa madarasani na kutumia taaluma yao kupambana na changamoto zilizopo uraiani.
Kwa upande wake Afisa Mtendaji mkuu wa Tasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Dokta Joseph Kihanda,amesema katika mwaka wa masomo 2013/2014 jumla ya wanafunzi 1960 wakiwemo wanawake 947 na wanaume 1013 wamehitimu katika fani za cheti cha awali, Stashahada na stashahada ya uzamili katika kampasi ya Mbeya.