Monday, December 1, 2014

SERIKALI YASEMA NI WAJIBU WA KILA SEKTA KUANDAA WATENDAJI WAO KWA KUWADHAMINI KATIKA MASOM

SERIKALI imesema ni wajibu wa kila sekta kuandaa watendaji wao kwa kuwadhamini katika masomo.
Mkurugenzi wa Idara ya Teknolojia habari na masiliano (Tehama) kutoka Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Dokta Ally Simba, amesema hayo katika hafla ya kutoa tunzo za udhamini kwa masomo ya Tehama kwa wanafunzi wa elimu ya juu mwaka 2014/2015.
Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), Ubungo jijini Dar es Salaam.
Dokta, Simba amesema kuwa ni mara ya nne kwa TCRA kutoa udhamini kwa elimu ya juu hasa kwa wale wa Tehama lengo ni kupata faida katika kizazi hiki na kijacho kikiwa na uelewa wa hali ya juu.