Monday, April 7, 2014

NGORONGORO HEROES KUINGIA KAMBINI ALHAMISI

Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngongoro Heroes) imereja nchini leo mchana (Aprili 7 mwaka huu) kutoka Kenya mechi ya michuano ya Afrika dhidi ya wenyewe, na itaingia kambini Alhamisi.
Ngorongoro Heroes ambayo imewasili saa 8.25 kwa ndege ya Kenya Airways ilitoka suluhu na Kenya katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Kanyetta uliopo katika mji wa Machakos.
Kocha John Simkoko amesema benchi lake la ufundi linafanyika kazi upunguzi uliojitokeza ili wafanye vizuri kwenye mechi ya marudiano itakayochezwa Aprili 27 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Iwapo Ngorongoro Heroes itaitoa Kenya, raundi inayofuata itacheza na Afrika Kusini. Fainali za Afrika kwa vijana chini ya miaka 20 zitafanyika mwakani nchini Senegal.

TIMU YA WATOTO WA MITAANI YATWAA UBINGWA WA DUNIA-BRAZIL

STREET_CHILD-TANZANIA_BINGWA
Timu ya Taifa ya Watoto wa Mitaani ya Tanzania imetwaa ubingwa wa Dunia wa Watoto wa Mitaani baada ya jana (Aprili 6 mwaka huu) kuilaza Burundi mabao 3-1 katika mchezo wa fainali uliochezwa jijini Rio de Janeiro, Brazil.
Mshambuliaji Frank William alifunga mabao matatu katika mechi hiyo iliyochezwa uwanja mkongwe na maarufu wa klabu ya Fluminense huku mgeni rasmi akiwa Waziri wa Fedh
a wa Uingereza, George Osborne.
STREET_CHILD
Tanzania ilipata tiketi ya kucheza fainali baada ya kuitandika Marekani mabao 6-1 ambapo hadi mapumziko ilikuwa mbele kwa mabao 4-0.
Burundi ilipata tiketi ya kucheza fainali baada ya kuifunga Pakistan mabao 4-3 katika mechi ya nusu fainali ya pili.
Timu ya Tanzania inarejea nchini Alhamisi (Aprili 10 mwaka huu) ambapo itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 10 jioni kwa ndege ya Emirates.

NGORONGORO YA KAZA MBELE YA WAKENYA, DAKIKA 90 NGOMA 0-0

Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Tanzania, Ngorongoro Heroes imejiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kwenye Fainali za Afrika mwakani nchini Senegal, baada ya kulazimisha sare ya bila kufungana na Kenya Uwanja wa Kenyatta, Machakos nchini Kenya jana katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza. Ngorongoro sasa inahitaji hata ushindi wa 1-0 katika mchezo wa marudiano Dar es Salaam ili kusonga mbele. katika mchezo vijanawa Heroes wameonekana kabisa kuwa wana kiu ya kwenda senegal mwakani baaa ya kutandaza soka la nguvu lenye kuvutia mbele ya vijana wa kenya.