Monday, April 7, 2014

NGORONGORO YA KAZA MBELE YA WAKENYA, DAKIKA 90 NGOMA 0-0

Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Tanzania, Ngorongoro Heroes imejiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kwenye Fainali za Afrika mwakani nchini Senegal, baada ya kulazimisha sare ya bila kufungana na Kenya Uwanja wa Kenyatta, Machakos nchini Kenya jana katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza. Ngorongoro sasa inahitaji hata ushindi wa 1-0 katika mchezo wa marudiano Dar es Salaam ili kusonga mbele. katika mchezo vijanawa Heroes wameonekana kabisa kuwa wana kiu ya kwenda senegal mwakani baaa ya kutandaza soka la nguvu lenye kuvutia mbele ya vijana wa kenya.