Sunday, April 6, 2014

MGAMBO YAIBAMIZA COASTAL UNION ,YANGA YAIPIGA 5-1 JKT RUVU


RATIBA/MATOKEO:
Jumapili Aprili 6
Yanga 5 vs JKT Ruvu 1
Coastal Union 0 vs Mgambo JKT 2
JKT Oljoro 2 v Tanzania Prisons 1
Rhino Rangers 0 v Mtibwa Sugar 1
Jumatano Aprili 9
Ruvu Shooting v Azam FC
MABINGWA wa VPL-Ligi Kuu Vodacom, Yanga, Leo wameweka hai matumaini yao ya kutetea Ubingwa wao baada ya kuitandika Ruvu JKT Bao 5-1 Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaa huku Straika wao, Mrisho Ngassa, akipiga Hetitriki.
Hadi Mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa Bao za Ngassa, Dakika ya 8 na 15, na Didier Kavumbagu, Dakika ya 38.
Kipindi cha Pili, Ngassa alipiga Bao jingine kwenye Dakika ya 49 na Javu kupiga Bao la 5 katika Dakika ya 52.
Bao pekee la Ruvu JKT lilifungwa na Iddi Mbaga katika Dakika 84.
Ushindi huu umeifanya Yanga iwe na Pointi 49 kwa Mechi 33 na wako Nafasi ya Pili huku Azam FC wakiendelea kuongoza Ligi wakiwa na Pointi 53 kwa Mechi 23.
Timu ya Tatu ni Mbeya City yenye Pointi 46 kwa Mechi 24.

Mgambo Shooting leo ikicheza katika mechi dhidi ya Coastal Union, imeibuka na ushindi wa mabao 2-0, hivyo kuzidi kujiweka katika nafasi nzuri ya kubaki Ligi Kuu Bara.
Kabla ya hapo, Mgambo ilizitungua Yanga na Simba kwenye uwanja huo wa Mkwakwani.
 Mechi nyingine mjini Arusha, wenyeji JKT Oljoro wamewaonyesha Prisons ‘rigwaride’ baada ya kuwachapa mabao 2-