Baada ya tarehe 17 baada ya hapo ukaja tarehe 27 na sasa usajili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania
Bara kwa wachezaji wa ndani umesogezwa mbele kwa masaa 48 kuanzia jana,
kutokana na timu kushindwa kukamilisha usajili katika muda husika jana.
Hayo ni kwa mujibu wa Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Selestine Mwesigwa ambapo amesema sababu za kusogeza mbele ni klabu zote za Ligi Kuu kushindwa kukamilisha usajili jana.

Mwesingwa amesema tff inapenda kuchukua fursa hii
kuwapongeza Kimondo kwa kumudu kuutumia mfumo huu na kuwasilisha usajili
wao ndani ya muda.
Hata hiyo Mwesigwa amesema kwamba dirisha la usajili kwa wachezaji wa kigeni
litafungwa Septemba 6, mwaka huu. “Hili dirisha la wachezaji wa kigeni
likifungwa, hakuna nyongeza ya muda tena, kwa kuwa hili lipo katika
mfumo wa kimataifa chini ya FIFA, likifungwa, limefungwa dunia nzima,
hivyo nawasihi viongozi wa klabu wahakikishe hawafanyi makoasa.